Mahakama
moja nchini Sudan imemkuta na hatia Meriam Yahya Ibrahim Ishaq,
mwanamke mwenye umri wa miaka 27 ya kukufuru na kuzini kwa kuwa ameolewa
na raia mmoja Mkristo kutoka Sudan ya Kusini na hivyo kuhukumiwa
kuchapwa viboko mia moja na kunyongwa hadi kufa!
Adhabu hii
imewashtua watetezi wa haki msingi za binadamu, kwa kuitaka Serikali ya
Sudan kuheshimu uhuru wa kuabudu kadiri ya Katiba ya nchi iliyotungwa
kunako Mwaka 2005.
Mahakama hiyo imetumia "Sharia" za dini ya
Kiislam zilizoingizwa nchini humo kunako mwaka 1983 zinazopiga rufuku
kwa mwamini wa dini ya Kiislam kuoa au kuolewa na Mkristo. Viongozi
mbali mbali wa Jumuiya ya Kimataifa wameitaka Serikali ya Sudan
kuingilia kati ili kusitisha utekelezaji wa adhabu hii ambayo ni kinyume
cha haki msingi za binadamu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni