Akiandika katika ukurasa wake wa Histogram, Wema alisema anachukizwa
sana na kitendo hicho, kwani kinamfanya asikae kwa amani na watu walio
karibu yake, na wengine wanamtenga kupitia vichwa vya habari tofauti
vya magazeti, ambavyo kwa asilimia kubwa anasema vinatumika kuuzia
magazeti hayo.
“Hivi karibuni kuna gazeti moja limeandika, ‘Ishu ya dawa za kulevya –
Wema kunyongwa China,
aomba Watanzania kumuombea’, jamani siwezi
kusema kama nina furaha, sijawahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo
siku yatakuja kuandika uongo wa namna hii, kwa sababu nakaaga kimya ndio
wameona ni njia ya kunionea muda wote, roho inaniuma sana,” aliandika
mwanadada huyo ambaye amewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006.
Wema alifafanua kuwa kutokana na kuona hapa nchini kuna maneno mengi
yasiyokuwa ya msingi, aliamua kwenda China kwa ajili ya kufanya mambo
yake binafsi, lakini watu ambao hawapendi maendeleo yake wamekuwa
wakimfuatilia na kuamua kumchafua katika magazeti.
“Sidhani kama nishawahi kumkosea yeyote katika maisha yangu, maskini
ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu, sijawahi hata
kufikiria kufanya biashara kama hii, muda uliopita niliambiwa nina
pepo la ngono, leo ninalia tena kwa kuambiwa nauza madawa ya kulevya,
eee Mungu nisaidie mimi,” alilalamika Wema.
Week Hot newz
-
Mpendwa mwana wa Mungu, leo tunasherehekea na kushangilia sherehe ya familia Takatifu. Masiha amezaliwa ndani ya familia hii....
-
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Ted Cruz ameshinda mchujo wa chama hicho katika jimbo la Wisconsin, hilo likiwa pig...
-
Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa...
-
Baba Mtakatifu Francisco, katika mafundisho yake kwa mahujaji na wageni walio kusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu P...
-
Freeman Mbowe MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofa...
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Ndege iliyokuwa imetekwa Rubani msaidizi wa ndege ya abiria ya shir...
-
Reading 1, James 3:13-18 13 Anyone who is wise or understanding among you should f...


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni