Akiandika katika ukurasa wake wa Histogram, Wema alisema anachukizwa
sana na kitendo hicho, kwani kinamfanya asikae kwa amani na watu walio
karibu yake, na wengine wanamtenga kupitia vichwa vya habari tofauti
vya magazeti, ambavyo kwa asilimia kubwa anasema vinatumika kuuzia
magazeti hayo.
“Hivi karibuni kuna gazeti moja limeandika, ‘Ishu ya dawa za kulevya –
Wema kunyongwa China,
aomba Watanzania kumuombea’, jamani siwezi
kusema kama nina furaha, sijawahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo
siku yatakuja kuandika uongo wa namna hii, kwa sababu nakaaga kimya ndio
wameona ni njia ya kunionea muda wote, roho inaniuma sana,” aliandika
mwanadada huyo ambaye amewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006.
Wema alifafanua kuwa kutokana na kuona hapa nchini kuna maneno mengi
yasiyokuwa ya msingi, aliamua kwenda China kwa ajili ya kufanya mambo
yake binafsi, lakini watu ambao hawapendi maendeleo yake wamekuwa
wakimfuatilia na kuamua kumchafua katika magazeti.
“Sidhani kama nishawahi kumkosea yeyote katika maisha yangu, maskini
ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu, sijawahi hata
kufikiria kufanya biashara kama hii, muda uliopita niliambiwa nina
pepo la ngono, leo ninalia tena kwa kuambiwa nauza madawa ya kulevya,
eee Mungu nisaidie mimi,” alilalamika Wema.
Week Hot newz
-
Machachari is a children comedy/ adventure series that depicts the friendship bet...
-
Neno Kwaresima linatokana na neno la lugha ya kilatini Quadragesima ; maana yake, namba arobaini. Kwa hiyo, Kwaresima ni kipindi cha siku ...
-
Pichani kutoka kushoto Msanii wa bongo fleva na nyimbo asili ya Kitanzania Batarokota akiwa na mwanamziki wa nyimbo za injili Moses Josi...
-
Shamrashamra za kufunga Mwaka wa Imani sanjari na Sherehe za Kristo Mfalme zimeanza kutimua vumbi mjini Vatican baada ya Baba Mtakatifu Fr...
-
Chumba cha cha upasuaji - ANSA Serikali imezindua m...
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
-
Na Charles Kayoka CHANZO: NIPASHE Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hoseah. Ninapenda sana Takukuru i...
-
Reading 1, James 2:14-24, 26 14 How does it help, my brothers, when som...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Yaya Toure Yaya Toure ametangazwa mshindi wa tuzo ya BBC ya mwaka 2...


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni