Week Hot newz
-
Mpendwa mwana wa Mungu, leo tunasherehekea na kushangilia sherehe ya familia Takatifu. Masiha amezaliwa ndani ya familia hii....
-
Ndege iliyokuwa imetekwa Rubani msaidizi wa ndege ya abiria ya shir...
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
-
Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa...
-
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Ted Cruz ameshinda mchujo wa chama hicho katika jimbo la Wisconsin, hilo likiwa pig...
-
Reading 1, James 3:13-18 13 Anyone who is wise or understanding among you should f...
-
Reading 1, First Corinthians 15:35-37, 42-49 35 Someone may ask: How are dead people raised, and what sort of body do the...
-
1.1. NDUGU WADOGO KUPAMBANA HADI KUTENGANISHWA (1226-1517) 1.1.1. MWANZO WA MAPAMBANO (1226-1318) Mt. Fransisko...
-
Tunaendelea kujielimisha na masuala mbalimbali yanayohusiana na maisha mchanganyiko, tukiwa ndani ya familia ambamo kwa kawaida t...
-
Tafakari imeletwa kwako na Pd Richard Tiganya, C.PP.S. Ni siku nyingine tena tunapokutana katika meza ya Neno la Mungu. Leo ...
St. Joseph yakumbuka watoto yatima
na Paskal Linda-Dar es salaam
SHULE ya Msingi St. Joseph iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo, imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandalwa kilichopo Mbweni Vijibweni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Msaada huo wenye thamani ya sh milioni tatu uliotolewa kwa watoto 92 wanaolelewa na kituo hicho, ni chakula, sabuni, sukari, vinywaji baridi, mafuta ya kupikia na nguo.
Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa msaada huo juzi, Mkurugenzi wa shule hiyo, Christa Rweyemamu, alisema uamuzi wa kusaidia kituo hicho ulifikiwa kupitia kitengo cha klabu ya huduma ya jamii ya shule hiyo na kuwashirikisha wazazi.
“Tulishirikisha wazazi ambao waliitikia kwa moyo mmoja na tukafikia mchango wa vifaa hivi na fedha taslimu sh 600,000 ambazo zitasaidia kulipia ada za watoto,” alisema.
Akitoa shukrani, mmiliki wa kituo hicho, Halima Mpeta, alisema wamefarijika na msaada kwa watoto hao ambao umetokana na ushawishi wa watoto wenzao
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni