SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeihamisha mechi ya kuwania tiketi ya fainali za Kombe la Dunia kwa wanawake wenye umri chini ya miaka 20 kati ya Tanzania ‘Tanzanite’ na Afrika Kusini ‘Amajita’ kutoka Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza hadi Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Tanzanite inajiandaa kuikaribisha Amajita Desemba 7 katika mechi ya kwanza ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia zitakazopigwa mwakani nchini Canada, baada ya kuwang’oa Msumbiji kwa jumla ya mabao 15-1.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Saad Kawemba kwa niaba ya ofisa habari, shirikisho lake limeamua kufanya mabadiliko ya uwanja kutokana na CCM Kirumba kutokuwa na ubora stahili.
Kawemba alisema licha ya jitihada zilizofanyika katika kuufanyia marekebisho, bado jaribio la kuwahi muda sahihi kuelekea mechi hiyo haliwezi kuzaa matunda, kutokana na ubovu wa vyumba vya kuvalia na miundombinu.
“Tunaposema vyumba vya kuvalia tunajumuisha vyoo, bafu na sehemu ya kupumzikia wachezaji. Hali katika vyumba vya Kirumba ni mbaya ikiwamo ukosefu wa umeme na aina ya matangazo yasiyohitajika kwa mechi rasmi kutokana na sababu za kiudhamini,” alisema Kawemba.
Aliwataka wakazi wa Kanda ya Ziwa kuwa wavumilivu kutokana na uamuzi huo wa TFF, huku akiwataka kuvuta subira kwani safari ya Tanzanite ni ndefu na kama itafanikiwa kukitoa kikosi cha Amajita, wanaweza kurejea huko kwa mechi zijazo.
“Kama itafanikiwa kuitoa Afrika Kusini, Tanzanite itaingia raundi ya tatu na ya mwisho, wakati huo naamini maboresho Kirumba yatakuwa yamefikia pazuri, hivyo tunaweza kurejea Mwanza kwa mechi ya nyumbani,” alisisitiza Kawemba.
Amajita inayonolewa na Maqsood Chenia, ilitinga raundi ya pili baada ya kuwang’oa vijana wenzao wa Botswana kwa mabao 7-2.
Timu mbili kutoka Afrika zitafuzu kwa fainali za Dunia, zitakazofanyika mwakani kuanzia Agosti 5 hadi 24.
Week Hot newz
-
Mpendwa mwana wa Mungu, leo tunasherehekea na kushangilia sherehe ya familia Takatifu. Masiha amezaliwa ndani ya familia hii....
-
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Ted Cruz ameshinda mchujo wa chama hicho katika jimbo la Wisconsin, hilo likiwa pig...
-
Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa...
-
Baba Mtakatifu Francisco, katika mafundisho yake kwa mahujaji na wageni walio kusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu P...
-
Freeman Mbowe MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofa...
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Ndege iliyokuwa imetekwa Rubani msaidizi wa ndege ya abiria ya shir...
-
Reading 1, James 3:13-18 13 Anyone who is wise or understanding among you should f...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni