Week Hot newz
-
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican, anabainisha kwamba, Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto wa kumi na sita kwa sasa anautumia...
-
Mpendwa mwanatafakari, kwanza ninakutakieni heri na baraka tele za kuzaliwa Mwana wa Mungu. Leo ni Krismas, ni Noeli, ni neema ya Mun...
-
The Prayer Thank You God! Dear Loving and Compassionate God, Giver of all gifts, we pray especially today for the mercy and love You give...
-
Katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, Jumamosi jioni tarehe 23 Novemba, 2013, Baba Mtakatifu Francisko kwa furaha kuu aliwapoke...
-
Freeman Mbowe MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofa...
-
Machachari is a children comedy/ adventure series that depicts the friendship bet...
-
Short Cuts Facts Feastday: September 4 Death: 1160 St. Rosalia, daughter of Sinibald, Lord of Roses and Qui...
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
TANZIA:Askofu John Simalenga afariki dunia!
Kanisa la Anglikani Tanzania limepata pigo la kufiwa na Askofu John Simalenga (60) wa Dayosisi South West Tanganyika iliyopo Njombe, Mkoani Iringa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Katibu mkuu wa Kanisa Anglikani Tanzania Canoni Dk. Dickson Chilongani alisema kuwa Kanisa limepata pigo kubwa kutokana na kifo cha Askofu Simalenga ambaye aliugua kwa muda mfupi.
Alieleza kuwa kifo cha Askofu Simalenga kimetokea Novemba, 24, 20013 muda mfupi baada ya kuruhusiwa kutoakatika hospitaliya ya kanisa hilo iliyopo Njombe. Alisema kuwa askofu alianza kuumwa alikwenda hospitali kwa ajili ya kupima afya yake na alipofika hospitali ilibainika kuwa alikuwa na maralia pamoja na sukari kupanda hadi kufikia 30 huku shinikizo la moyo kuwa juu.
Canon Dk. Chilongani alisema kuwa baada ya madaktari kubaini kwamba Askofu anasumbuliwa na matatizo hayo alipewa dawa na kuruhusiwa kwenda nyumbani wakitegemea kuwa dawa hizo zingemsaidia kutuliza magonjwa ambayo alibainika kuwa nayo. Alisema kinyume na matarajio ya madaktari, Askofu Simalenga baada ya kurudi nyumbani hali ilibadilika ghafla na kufariki dunia majira ya saa 11 alfajiri.
Marehemu Askofu John Simalenga alizaliwa tarehe 30 Novemba 1953 na kufariki dunia tarehe 24 Novemba 2013. Alisema Kanisa Anglikani linaendelea na taratibu za maandali ya utaratibu wa mazishi ya mwili wa askofu huyo ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa taarifa kwa wachungaji pamoja na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni