Week Hot newz
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
"Amoris Laetitia" "Furaha ya Upendo" ndani ya familia ni Wosia wa kitume utakaozinduliwa hapo tarehe 8 Aprili 2016...
-
(Vatican) Kumjua Kristu ni kutembea nae katika utendaji wote wa kila siku na si kumfahamu kinadharia au kwa kusoma tu maandishi ya...
-
استقبل البابا فرنسيس هذا السبت في القصر الرسولي بالفاتيكان رئيس جمهورية قبرص السيد نيكوس أناستاسيادس الذي ...
-
Ninatumaini sisi sote tumewahi kuusikia msemo huu: “Funguka macho, Angalia!” Usemi huu hauna maana kwamba mmoja ni kipofu au amefumba ma...
-
SIKU chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kutoa agizo la kupunguza mishahara mikubwa ya watendaji wa mashirika ya umma, hati...
-
Pichani juu kutoka kushoto Msananii wa bongo fleva na mziki wa asili ya kitanzania Batarokota akiwa katika picha ya pamoja na Babu yake ...
-
Holy Archangel Who Strengthened Our Lord in His Agony I salute thee, holy Angel who didst comfort my Jesus in His agony, and with thee I...
-
Short Cuts Facts Feastday: October 7 Birth: 1101 Death: 1206 Artaldus (also called Arthaud) wa...
TANZIA:Askofu John Simalenga afariki dunia!
Kanisa la Anglikani Tanzania limepata pigo la kufiwa na Askofu John Simalenga (60) wa Dayosisi South West Tanganyika iliyopo Njombe, Mkoani Iringa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Katibu mkuu wa Kanisa Anglikani Tanzania Canoni Dk. Dickson Chilongani alisema kuwa Kanisa limepata pigo kubwa kutokana na kifo cha Askofu Simalenga ambaye aliugua kwa muda mfupi.
Alieleza kuwa kifo cha Askofu Simalenga kimetokea Novemba, 24, 20013 muda mfupi baada ya kuruhusiwa kutoakatika hospitaliya ya kanisa hilo iliyopo Njombe. Alisema kuwa askofu alianza kuumwa alikwenda hospitali kwa ajili ya kupima afya yake na alipofika hospitali ilibainika kuwa alikuwa na maralia pamoja na sukari kupanda hadi kufikia 30 huku shinikizo la moyo kuwa juu.
Canon Dk. Chilongani alisema kuwa baada ya madaktari kubaini kwamba Askofu anasumbuliwa na matatizo hayo alipewa dawa na kuruhusiwa kwenda nyumbani wakitegemea kuwa dawa hizo zingemsaidia kutuliza magonjwa ambayo alibainika kuwa nayo. Alisema kinyume na matarajio ya madaktari, Askofu Simalenga baada ya kurudi nyumbani hali ilibadilika ghafla na kufariki dunia majira ya saa 11 alfajiri.
Marehemu Askofu John Simalenga alizaliwa tarehe 30 Novemba 1953 na kufariki dunia tarehe 24 Novemba 2013. Alisema Kanisa Anglikani linaendelea na taratibu za maandali ya utaratibu wa mazishi ya mwili wa askofu huyo ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa taarifa kwa wachungaji pamoja na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni