Jengeni
matumaini kwa Bwana, hata katika hali ngumu, Papa amehimiza wakati wa
Ibada ya Misa ya asubuhi Jumatatu hii katika Kanisa dogo la Mtakatifu
Marta mjini Vatican. Papa alisisitiza kwamba Wakristo wameitwa kufanya
maamuzi thabiti , kama yanavyo fundisha maisha ya mashahidi wa dini wa
kila wakati. Hata leo, alibainisha, kuna wake kwa waume wanao teseka kwa
sababu ya imani yao kwa Kristu. Na hivyo wao ni mfano kwetu wa kuiga,
kwa ajili ya kupata nguvu za kujikabidhi kwa Bwana bila kujibakiza.
Papa
aliendelea kufundisha kwamba, kumchagua Kristu, hakuna ukomo. Alieleza
hilo akingalisha katika somo la Kitabu cha Nabii Daniel, na Injili :
ambamo vijana Wayahudi watumwa katika mahakama ya Nebukadreza na mjane
aliyekwenda katika hekalu kumwabudu Bwana. Katika kesi zote, Papa
anaona, hapakuwa na ukomo wa hali. Mjane katika hali ya umaskini na
vijana katika hali ya utumwa, wote walijikabidhi kwa Bwana . Mjane
aliweka vyote alivyokuwa navyo katika hazina ya Hekalu, ambapo kwa
vijana walibaki aminifu kwa Bwana, hata katika hatari ya maisha.
Papa
aliendelea kusema, katika hali za wote, mjane na vijana – hawakujali
hatari za maisha zilizokuwa mbele yao. Walimchagua Bwana kwa moyo moja,
bila wasiwasi na bila upungufu. Kwao Bwana alikuwa ni juu ya yote juu.
Walitambua Bwana wao ni Mungu na kwake walijikabidhi wenyewe. Na hii
hawakufanya kwa sababu za kujitafutia sifa bandia , lakini walifanya
hivyo kwa kutambua kwamba, Bwana ndiye mkuu wa yote. Walijua kwamba
Bwana ni mwaminifu. Na ndivyo tunavyotakiwa nasi pia kufanya.
Ni
kumtegemea Bwana kwa uaminifu na imani kwamba daima yupo, kwa sababu
Bwana hawezi kubadilika kubadilika na kujikana mwenyewe. Imani hii
katika Bwana Papa Francisko aliongeza, huongoza katika maamuzi thabiti
ya kumchagua Yeye kuwa ndiye Bwana wa Yote, Yeye ni mwaminifu, katika
katika mambo yote madogo , makubwa na hata magumu.
Papa alieleza
na kuitazama historia ya kanisa kwamba, historia yake inaonyesha
wanaume, wanawake, wazee, vijana, waliofanya uchaguzi huu, kama tunavyo
sikia katika vyombo vya mawasiliano au kusoma katika magazeti juu ya
maisha ya mateso yanayokabili hata leo hii, Wakristo katika maeneo
mbalimbali duniani.
Wakristu hao wanaoishi nasi katika wakati
huu, ni mfano hai kwetu, wenye kutuhimiza pia sisi, kuiweka hazina
yetu ndani ya kanisa, ili kwamba, ambamo Bwana yumo ndani mwake.
Ushuhuda wa Wakristu hawa wateswa, unashuhudia neema ya ujasiri wa
kusonga mbele katika maisha ya Kikristo , katika hali ya kawaida ,
maisha magumu na hata katika mazingira hatarishi . Ni kuwa na Maamuzi
thabiti kwa Bwana.
Week Hot newz
-
Tunaendelea tena katika tafakari yetu masomo Dominika ya II ya Pasaka mwaka A. Ni kipindi cha furaha kwa sababu ya ushindi dhidi ...
-
Machachari is a children comedy/ adventure series that depicts the friendship bet...
-
Baba Mtakatifu Francisko katika Maadhimisho ya Siku ya Wapendanao Duniani kwa Mwaka 2014 amewataka vijana kukuza na kujenga ndani mwao ...
-
Reading 1, Colossians 1:9-14 9 That is why, ever since the day he told us, we have never failed to remem...
-
Mtayarishaji na Muigizaji wa filamu za kiswahili nchini Tanzania Nice Mohamed ‘Mtunis’pichani amesema kwamba filamu yake ya Who’s B...
-
Askofu mkuu Giancarlo Maria Bregantini wa Jimbo kuu la Campobasso- Boiano ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tume ya matatizo ya kijami...
-
Jumatatu , Baba Mtakatifu Francisko, alisema uhuru wa Mkristo hupatikana katika utulivu wa kulisikiliza Neno la Mungu na kuliishi. Papa...
-
Holy Archangel Who Strengthened Our Lord in His Agony I salute thee, holy Angel who didst comfort my Jesus in His agony, and with thee I...
-
Baraza la Kipapa la Ibada na nidhamu ya Sakramenti za Kanisa kuanzia tarehe 18 hadi 20 Februari 2014 litaadhimisha Kongamano la Kimatai...
-
Katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, Jumamosi jioni tarehe 23 Novemba, 2013, Baba Mtakatifu Francisko kwa furaha kuu aliwapoke...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni