Padre
Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican, wakati wa hija ya Baba
Mtakatifu Francisko nchini Cuba na Mexico, Ijumaa tarehe 12 Februari
2016, kwa niaba ya waandishi wa habari 76 walioko kwenye msafara wa Baba
Mtakatifu, amemtakia heri na mafanikio mema katika hija hii ya
kihistoria. Kundi kubwa la waandishi wa habari ni wale wanaotoka Mexico
ambao wamepewa upendeleo wa pekee ili kuhakikisha kwamba, ujumbe wa Baba
Mtakatifu unawafikia walengwa.
Baba Mtakatifu amewashukuru waandishi
wa habari kwa kazi kubwa wanayoifanya hasa kwa kuzingatia kuwa hija hii
ni ndefu na ya kihistoria, kwani anapenda kukutana na kuzungumza na
ndugu yake Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima. Anapenda kwenda
kusali na kumsalimia Bikira Maria wa Guadalupe, ili kushangaa Fumbo la
upendo wa Mungu linalofumbatwa katika maisha ya wengi.
Baba Mtakatifu amechukua nafasi hii
kwa namna ya pekee kumshukuru Dr. Albeto Gasbarri ambaye kwa muda wa
miaka 47 amejisadaka kwa kazi na utume mbali mbali mjini Vatican. Kwa
muda wa miaka 37 ameratibu hija za kitume za viongozi wakuu wa Kanisa
sehemu mbali mbali za dunia. Tangu wakati huu, Monsinyo Mauricio Rueda
atakuwa mratibu mpya wa hija za kitume za viongozi wa Kanisa mjini
Vatican. Dr. Gasbarri anatarajiwa kung’atuka rasmi kutoka katika uongozi
hapo tarehe 29 Februari 2016.
Waandishi wa habari kutoka Mexico
wamemzawadia Baba Mtakatifu kofia ya kitamaduni kutoka Mexico kama
walivyofanya kwa Mtakatifu Yohane Paulo II miaka 37 iliyopita na kwa
Papa Mstaafu Benedikto XVI na sasa kwa Baba Mtakatifu Francisko. Baba
Mtakatifu amewashukuru na kuwatakia wote kazi na utume mwema wakati huu
wa hija yake ya kitume nchini Mexico.
Week Hot newz
-
Mpendwa mwana wa Mungu karibuni katika kipindi cha tafakari tunapoadhimisha Dominika ya Matawi, Dominika ambayo ni mwanzo wa Ju...
-
Burundi imepiga marufuku bodaboda au pikipiki kuingia katikati mwa mji mkuu Bujumbura katika juhudi za kujaribu kupunguza mashambulio.Pik...
-
Maaskofu Katoliki wa Ufilipino, wametoa wito wa Novena, sala na fadhila, kwa waathirika na familia zilizopigwa vikali na maaf...
-
Baba Mtakatifu Francisko katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani sanjari na Siku kuu ya Yesu Kristo Mfalme wa Ulimwengu anatarajiw...
-
Jumapili iliyopita tarehe 17 Novemba 2013 wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, waamini ...
-
Mradi wa miaka 5 kwa ajili ya huduma kwa waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi wazinduliwa nchini TanzaniaMfuko wa Msamaria mwema, unaosimamiwa na Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya kwa kushirikiana ...
-
Reading 1, Micah 5:1-4 1 But you (Bethlehem) Ephrathah, the least of the clans of Judah, from you will co...
