Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Kim Poulsen, amesema timu yake mesto wa yosso na wazoefu, iko tayari kuikabili Zambia (Chipolopolo) katika mechi yake ya kwanza ya kuwania ubingwa wa mashindano ya Kombe la Chalenji itakayofanyika kesho kwenye Uwanja wa Nyayo jijini hapa.
Akizungumza jana, Poulsen alisema wachezaji wake wote wako tayari na wamejiandaa kufanya vizuri katika mechi hiyo ya kwanza ili kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kusonga mbele.
Poulsen alisema mechi dhidi ya Chipolopolo inatarajiwa kuwa ngumu kwa sababu wachezaji wengi wa Zambia ni wauzoefu tofauti na kikosi chake ambacho mwaka huu ni mseto kutokana na kujumuisha yosso wengi aliowaita kwa mara ya kwanza, lakini anaamini watafanya vizuri.
"Tuko tayari, tumejiandaa kwa mashindano na tunaamini tutaanza vyema mechi yetu," alisema Kocha huyo raia wa Denmark.
Aliongeza kuwa, katika kundi lao ambalo linajumuisha timu ya Somalia na Burundi, hakuna mechi nyepesi kwa sababu kila moja imekuja kushindana na si kushiriki.
Naye mshambuliaji mahiri wa timu hiyo, Mrisho Ngasa, aliliambia blogu hili kuwa wamekuja Nairobi kushindana na watajituma ili kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania Bara.
Ngassa alisema anajua Watanzania wamewatuma kuiwakilisha vyema na hicho ndicho wamepanga kukitekeleza.
"Tunajua jukumu letu na tunamuomba Mungu tufanye vizuri, tuombeeni ili tufanye kile ambacho kocha ametuelekeza," alisema Ngasa.
Kilimanjaro Stars iliyoko Kundi B, ilitua jijini hapa juzi usiku na itacheza mechi yake ya pili Desemba Mosi dhidi ya Somalia huku ikimaliza hatua ya makundi kwa kuivaa Burundi hapo Desemba 4, mwaka huu.
Uganda ndiyo mabingwa watetezi wa mashindano hayo yanayofanyika kila mwaka kwa kushirikisha nchi wanachama wa Cecafa na timu alikwa.
Week Hot newz
-
Machachari is a children comedy/ adventure series that depicts the friendship bet...
-
Nelson Mandela’s former wife Winnie Madikizela Mandela (left) and widow Graca Machel attend his memorial service in Joha...
-
Mkurugenzi mkuu wa Batarokota Social artwoks Paskal Linda amewataka watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi yao, amewataka wote ku...
-
NA OSCAR ASSENGA, TANGA-Tanzania.Gazeti Mtanzania. KATIBU wa Chama cha Watu Wenye Albino Mkoa wa Tanga (TAS), Mah...
-
1.1. NDUGU WADOGO KUPAMBANA HADI KUTENGANISHWA (1226-1517) 1.1.1. MWANZO WA MAPAMBANO (1226-1318) Mt. Fransisko...
-
For South Africans, winning the 1995 Rugby World Cup final marked the emergence of the "Rainbow Nation" -- for New Zealanders...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu Francisko anawataka wadau mbali mbali wa s...
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni