Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Kim Poulsen, amesema timu yake mesto wa yosso na wazoefu, iko tayari kuikabili Zambia (Chipolopolo) katika mechi yake ya kwanza ya kuwania ubingwa wa mashindano ya Kombe la Chalenji itakayofanyika kesho kwenye Uwanja wa Nyayo jijini hapa.
Akizungumza jana, Poulsen alisema wachezaji wake wote wako tayari na wamejiandaa kufanya vizuri katika mechi hiyo ya kwanza ili kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kusonga mbele.
Poulsen alisema mechi dhidi ya Chipolopolo inatarajiwa kuwa ngumu kwa sababu wachezaji wengi wa Zambia ni wauzoefu tofauti na kikosi chake ambacho mwaka huu ni mseto kutokana na kujumuisha yosso wengi aliowaita kwa mara ya kwanza, lakini anaamini watafanya vizuri.
"Tuko tayari, tumejiandaa kwa mashindano na tunaamini tutaanza vyema mechi yetu," alisema Kocha huyo raia wa Denmark.
Aliongeza kuwa, katika kundi lao ambalo linajumuisha timu ya Somalia na Burundi, hakuna mechi nyepesi kwa sababu kila moja imekuja kushindana na si kushiriki.
Naye mshambuliaji mahiri wa timu hiyo, Mrisho Ngasa, aliliambia blogu hili kuwa wamekuja Nairobi kushindana na watajituma ili kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania Bara.
Ngassa alisema anajua Watanzania wamewatuma kuiwakilisha vyema na hicho ndicho wamepanga kukitekeleza.
"Tunajua jukumu letu na tunamuomba Mungu tufanye vizuri, tuombeeni ili tufanye kile ambacho kocha ametuelekeza," alisema Ngasa.
Kilimanjaro Stars iliyoko Kundi B, ilitua jijini hapa juzi usiku na itacheza mechi yake ya pili Desemba Mosi dhidi ya Somalia huku ikimaliza hatua ya makundi kwa kuivaa Burundi hapo Desemba 4, mwaka huu.
Uganda ndiyo mabingwa watetezi wa mashindano hayo yanayofanyika kila mwaka kwa kushirikisha nchi wanachama wa Cecafa na timu alikwa.
Week Hot newz
-
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican, anabainisha kwamba, Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto wa kumi na sita kwa sasa anautumia...
-
Mpendwa mwanatafakari, kwanza ninakutakieni heri na baraka tele za kuzaliwa Mwana wa Mungu. Leo ni Krismas, ni Noeli, ni neema ya Mun...
-
The Prayer Thank You God! Dear Loving and Compassionate God, Giver of all gifts, we pray especially today for the mercy and love You give...
-
Katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, Jumamosi jioni tarehe 23 Novemba, 2013, Baba Mtakatifu Francisko kwa furaha kuu aliwapoke...
-
Machachari is a children comedy/ adventure series that depicts the friendship bet...
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
-
Kanisa linasadiki na kufundisha kwamba, Mwenyezi Mungu ambaye ni asili na kiini cha upendo amemuumba mtu kwa upendo na amemwita kupenda...
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni