Wakati dirisha dogo la usajili likitarajiwa kufungwa Desemba 15, mwaka huu, Shirikisho la Soka nchini(TFF), limezikumbusha klabu zote kuheshimu kanuni na kuzingatia muda uliowekwa.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa kitendo cha klabu kupeleka mchezaji kwa mkopo katika klabu nyingine hakutoi nafasi ya kusajili mchezaji mpya.
Tamko hilo la TFF lina maana kwamba, Yanga ambayo kwa sasa tayari imeingia mikataba ya kuwasajili kipa Juma Kaseja aliyekuwa huru na kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu Shooting, haitakubaliwa kumsajili mmoja wa wachezaji hao kwani tayari ilikuwa na wachezaji 29.
"Kama klabu ilisajili wachezaji 30 maana yake ni kuwa, haina nafasi ya kuongeza wachezaji. Kwa upande wa wachezaji wa kigeni (foreign players), tunakumbusha kuwa, kuanzia msimu ujao 2014/2015 watakuwa watatu tu badala ya watano wa sasa," alisema Wambura.
Alisema mpaka jana jioni hakuna klabu hata moja iliyokuwa imeshaingia kwenye mfumo wa TMS kuomba uhamisho wa mchezaji wa kigeni na itakapofika Desemba 15, mwaka huu mfumo huo wa TMS utafungwa.
Week Hot newz
-
Machachari is a children comedy/ adventure series that depicts the friendship bet...
-
Nelson Mandela’s former wife Winnie Madikizela Mandela (left) and widow Graca Machel attend his memorial service in Joha...
-
Mkurugenzi mkuu wa Batarokota Social artwoks Paskal Linda amewataka watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi yao, amewataka wote ku...
-
NA OSCAR ASSENGA, TANGA-Tanzania.Gazeti Mtanzania. KATIBU wa Chama cha Watu Wenye Albino Mkoa wa Tanga (TAS), Mah...
-
1.1. NDUGU WADOGO KUPAMBANA HADI KUTENGANISHWA (1226-1517) 1.1.1. MWANZO WA MAPAMBANO (1226-1318) Mt. Fransisko...
-
For South Africans, winning the 1995 Rugby World Cup final marked the emergence of the "Rainbow Nation" -- for New Zealanders...
-
Baba Mtakatifu Francisko anawataka wadau mbali mbali wa s...
-
The first day of Lent Ash Wednesday marks the beginning of the Season of Lent. It is a season of penance, reflection, and fastin...
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni