Wakati dirisha dogo la usajili likitarajiwa kufungwa Desemba 15, mwaka huu, Shirikisho la Soka nchini(TFF), limezikumbusha klabu zote kuheshimu kanuni na kuzingatia muda uliowekwa.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa kitendo cha klabu kupeleka mchezaji kwa mkopo katika klabu nyingine hakutoi nafasi ya kusajili mchezaji mpya.
Tamko hilo la TFF lina maana kwamba, Yanga ambayo kwa sasa tayari imeingia mikataba ya kuwasajili kipa Juma Kaseja aliyekuwa huru na kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu Shooting, haitakubaliwa kumsajili mmoja wa wachezaji hao kwani tayari ilikuwa na wachezaji 29.
"Kama klabu ilisajili wachezaji 30 maana yake ni kuwa, haina nafasi ya kuongeza wachezaji. Kwa upande wa wachezaji wa kigeni (foreign players), tunakumbusha kuwa, kuanzia msimu ujao 2014/2015 watakuwa watatu tu badala ya watano wa sasa," alisema Wambura.
Alisema mpaka jana jioni hakuna klabu hata moja iliyokuwa imeshaingia kwenye mfumo wa TMS kuomba uhamisho wa mchezaji wa kigeni na itakapofika Desemba 15, mwaka huu mfumo huo wa TMS utafungwa.
Week Hot newz
-
Mpendwa mwana wa Mungu karibuni katika kipindi cha tafakari tunapoadhimisha Dominika ya Matawi, Dominika ambayo ni mwanzo wa Ju...
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
(Vatican) Kumjua Kristu ni kutembea nae katika utendaji wote wa kila siku na si kumfahamu kinadharia au kwa kusoma tu maandishi ya...
-
Baba Mtakatifu Francisko katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani sanjari na Siku kuu ya Yesu Kristo Mfalme wa Ulimwengu anatarajiw...
-
استقبل البابا فرنسيس هذا السبت في القصر الرسولي بالفاتيكان رئيس جمهورية قبرص السيد نيكوس أناستاسيادس الذي ...
-
Ninatumaini sisi sote tumewahi kuusikia msemo huu: “Funguka macho, Angalia!” Usemi huu hauna maana kwamba mmoja ni kipofu au amefumba ma...
-
Reading 1, Micah 5:1-4 1 But you (Bethlehem) Ephrathah, the least of the clans of Judah, from you will co...
-
Short Cuts Facts Feastday: October 7 Birth: 1101 Death: 1206 Artaldus (also called Arthaud) wa...
-
Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambirambi kwa Rais Jacob Zuma wa Afrika ya kusini na wananchi wa Afrika ya Kusini ...
-
Cecafa Tusker Cup: Zanzibar v South Sudan Wednesday, 27 Nov 2013 @ 12:30 Cecafa Tusker Cup: Kenya v Ethiopia Wednesday, 27 Nov 2013 @ 15:00 ...
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni