Akiandika katika ukurasa wake wa Histogram, Wema alisema anachukizwa
sana na kitendo hicho, kwani kinamfanya asikae kwa amani na watu walio
karibu yake, na wengine wanamtenga kupitia vichwa vya habari tofauti
vya magazeti, ambavyo kwa asilimia kubwa anasema vinatumika kuuzia
magazeti hayo.
“Hivi karibuni kuna gazeti moja limeandika, ‘Ishu ya dawa za kulevya –
Wema kunyongwa China,
aomba Watanzania kumuombea’, jamani siwezi
kusema kama nina furaha, sijawahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo
siku yatakuja kuandika uongo wa namna hii, kwa sababu nakaaga kimya ndio
wameona ni njia ya kunionea muda wote, roho inaniuma sana,” aliandika
mwanadada huyo ambaye amewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006.
Wema alifafanua kuwa kutokana na kuona hapa nchini kuna maneno mengi
yasiyokuwa ya msingi, aliamua kwenda China kwa ajili ya kufanya mambo
yake binafsi, lakini watu ambao hawapendi maendeleo yake wamekuwa
wakimfuatilia na kuamua kumchafua katika magazeti.
“Sidhani kama nishawahi kumkosea yeyote katika maisha yangu, maskini
ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu, sijawahi hata
kufikiria kufanya biashara kama hii, muda uliopita niliambiwa nina
pepo la ngono, leo ninalia tena kwa kuambiwa nauza madawa ya kulevya,
eee Mungu nisaidie mimi,” alilalamika Wema.
Week Hot newz
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
A Prayer for a Family O dear Jesus, I humbly implore You to grant Your special graces to our family. May ou...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kut...
-
Baba Mtakatifu Francisko wakati akirejea kutoka Armenia a...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
MOROGORO,TANZANIA. MSANII wa bongo fleva na mkali wa kurap kwa lugha 31 Batarokota, amesema tangu alipofariki mke wake mpendwa mwaka ...
-
Siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba tareehe 21/05/2016 katika jijini la mawe Mwanza (Rocky City) kutakuwa na burudani kabam...
-
Pichani juu msanii wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota akiwa katika Hoteli ya Misana aliyofikia jijini Mwanza.. MSANII wa ny...
-
KUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi. Changamoto hizo zimes...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni