Baraza la Maaskofu Katoliki Angola, Sao Tome na Principe linasema, sera za utoaji mimba ni mauaji ya watu wasiokuwa na hatia, ni kinyume cha Amri za Mungu; utamaduni na utambulisho wa wananchi wa Angola. Wananchi wanakumbushwa kwamba, maisha ya
binadamu ni matakatifu tangu pale mtoto anapotungwa mimba tumboni mwa mama yake hadi mauti ya kawaida yanapomfika kadiri ya mapenzi ya Mungu.
Hakuna mtu mwenye mamlaka yanayomruhusu kuwapokonya wengine zawadi ya uhai kwa kisingizio chochote kile. Ni jukumu na dhamana na wanafamilia, wahudumu wa sekta ya afya na wanasiasa kutoruhusu wala kushabikia sera za utoaji mimba na badale yake, wawe mstari wa mbele kulinda na kutetea zawadi ya uhai kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Maaskofu wanasema kwamba, kadiri ya mila na tamaduni za wananchi wa Angola katika ujumla wao, vitendo vya utoaji mimba havikubaliki kamwe kwani ni kielelezo cha mkosi katika familia. Hii ni changamoto kwa waamini na watu wenye mapenzi mema kusimama kidete kulinda na kutetea Injili ya uhai, kwani sera dhidi ya Injili ya uhai ni kutaka kusababisha majanga katika Jamii
.
Ni matumaini ya wananchi wa Angola kwamba, wabunge wao watasimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya uhai na kamwe hawatakubali kushinikizwa ili kuunga mkono sera za utoaji na vizuia mimba.
Week Hot newz
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
A Prayer for a Family O dear Jesus, I humbly implore You to grant Your special graces to our family. May ou...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kut...
-
Baba Mtakatifu Francisko wakati akirejea kutoka Armenia a...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
MOROGORO,TANZANIA. MSANII wa bongo fleva na mkali wa kurap kwa lugha 31 Batarokota, amesema tangu alipofariki mke wake mpendwa mwaka ...
-
Siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba tareehe 21/05/2016 katika jijini la mawe Mwanza (Rocky City) kutakuwa na burudani kabam...
-
Pichani juu msanii wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota akiwa katika Hoteli ya Misana aliyofikia jijini Mwanza.. MSANII wa ny...
-
KUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi. Changamoto hizo zimes...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni