Baraza la Maaskofu Katoliki Angola, Sao Tome na Principe linasema, sera za utoaji mimba ni mauaji ya watu wasiokuwa na hatia, ni kinyume cha Amri za Mungu; utamaduni na utambulisho wa wananchi wa Angola. Wananchi wanakumbushwa kwamba, maisha ya
binadamu ni matakatifu tangu pale mtoto anapotungwa mimba tumboni mwa mama yake hadi mauti ya kawaida yanapomfika kadiri ya mapenzi ya Mungu.
Hakuna mtu mwenye mamlaka yanayomruhusu kuwapokonya wengine zawadi ya uhai kwa kisingizio chochote kile. Ni jukumu na dhamana na wanafamilia, wahudumu wa sekta ya afya na wanasiasa kutoruhusu wala kushabikia sera za utoaji mimba na badale yake, wawe mstari wa mbele kulinda na kutetea zawadi ya uhai kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Maaskofu wanasema kwamba, kadiri ya mila na tamaduni za wananchi wa Angola katika ujumla wao, vitendo vya utoaji mimba havikubaliki kamwe kwani ni kielelezo cha mkosi katika familia. Hii ni changamoto kwa waamini na watu wenye mapenzi mema kusimama kidete kulinda na kutetea Injili ya uhai, kwani sera dhidi ya Injili ya uhai ni kutaka kusababisha majanga katika Jamii
.
Ni matumaini ya wananchi wa Angola kwamba, wabunge wao watasimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya uhai na kamwe hawatakubali kushinikizwa ili kuunga mkono sera za utoaji na vizuia mimba.
Week Hot newz
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Tafakari masomo Dominika, ninafurahi tena kuwa nawe katika safari yetu ya Majilio tukijiandaa kwa ajili ya ujio wa Mwana wa Mungu. Ni wak...
-
Freeman Mbowe MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofa...
-
NA OSCAR ASSENGA, TANGA-Tanzania.Gazeti Mtanzania. KATIBU wa Chama cha Watu Wenye Albino Mkoa wa Tanga (TAS), Mah...
-
Baba Mtakatifu Francisko Alhamis hii 14.11.2014 majira ya saa nne, kwa mara ya kwanza tangu kuwa Papa mwezi March mwaka huu, alifanya ziar...
-
Na Paskal Linda Ninakuletea ujumbe wa Neno la Mungu, Dominika ya 25 ya mwaka B wa Kanisa. Mama Kanisa anatufundisha wajibu wa Jumuiya ...
-
Klabu za Ligi ya Premia zilitumia zaidi ya £155m siku ya mwisho ya kuhama kwa wachezaji kipindi cha majira ya joto na kufikisha jumla y...
-
Reading 1, First Corinthians 15:35-37, 42-49 35 Someone may ask: How are dead people raised, and what sort of body do the...
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya 32 ya Mwaka B wa Kan...
-
Kardinali Pietro Parolin akisalimiana na Masista wa Upend...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni