SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeihamisha mechi ya kuwania tiketi ya fainali za Kombe la Dunia kwa wanawake wenye umri chini ya miaka 20 kati ya Tanzania ‘Tanzanite’ na Afrika Kusini ‘Amajita’ kutoka Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza hadi Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Tanzanite inajiandaa kuikaribisha Amajita Desemba 7 katika mechi ya kwanza ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia zitakazopigwa mwakani nchini Canada, baada ya kuwang’oa Msumbiji kwa jumla ya mabao 15-1.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Saad Kawemba kwa niaba ya ofisa habari, shirikisho lake limeamua kufanya mabadiliko ya uwanja kutokana na CCM Kirumba kutokuwa na ubora stahili.
Kawemba alisema licha ya jitihada zilizofanyika katika kuufanyia marekebisho, bado jaribio la kuwahi muda sahihi kuelekea mechi hiyo haliwezi kuzaa matunda, kutokana na ubovu wa vyumba vya kuvalia na miundombinu.
“Tunaposema vyumba vya kuvalia tunajumuisha vyoo, bafu na sehemu ya kupumzikia wachezaji. Hali katika vyumba vya Kirumba ni mbaya ikiwamo ukosefu wa umeme na aina ya matangazo yasiyohitajika kwa mechi rasmi kutokana na sababu za kiudhamini,” alisema Kawemba.
Aliwataka wakazi wa Kanda ya Ziwa kuwa wavumilivu kutokana na uamuzi huo wa TFF, huku akiwataka kuvuta subira kwani safari ya Tanzanite ni ndefu na kama itafanikiwa kukitoa kikosi cha Amajita, wanaweza kurejea huko kwa mechi zijazo.
“Kama itafanikiwa kuitoa Afrika Kusini, Tanzanite itaingia raundi ya tatu na ya mwisho, wakati huo naamini maboresho Kirumba yatakuwa yamefikia pazuri, hivyo tunaweza kurejea Mwanza kwa mechi ya nyumbani,” alisisitiza Kawemba.
Amajita inayonolewa na Maqsood Chenia, ilitinga raundi ya pili baada ya kuwang’oa vijana wenzao wa Botswana kwa mabao 7-2.
Timu mbili kutoka Afrika zitafuzu kwa fainali za Dunia, zitakazofanyika mwakani kuanzia Agosti 5 hadi 24.
Week Hot newz
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
A Prayer for a Family O dear Jesus, I humbly implore You to grant Your special graces to our family. May ou...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kut...
-
Baba Mtakatifu Francisko wakati akirejea kutoka Armenia a...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
MOROGORO,TANZANIA. MSANII wa bongo fleva na mkali wa kurap kwa lugha 31 Batarokota, amesema tangu alipofariki mke wake mpendwa mwaka ...
-
Siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba tareehe 21/05/2016 katika jijini la mawe Mwanza (Rocky City) kutakuwa na burudani kabam...
-
Pichani juu msanii wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota akiwa katika Hoteli ya Misana aliyofikia jijini Mwanza.. MSANII wa ny...
-
KUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi. Changamoto hizo zimes...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni