Padre
Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican, wakati wa hija ya Baba
Mtakatifu Francisko nchini Cuba na Mexico, Ijumaa tarehe 12 Februari
2016, kwa niaba ya waandishi wa habari 76 walioko kwenye msafara wa Baba
Mtakatifu, amemtakia heri na mafanikio mema katika hija hii ya
kihistoria. Kundi kubwa la waandishi wa habari ni wale wanaotoka Mexico
ambao wamepewa upendeleo wa pekee ili kuhakikisha kwamba, ujumbe wa Baba
Mtakatifu unawafikia walengwa.
Baba Mtakatifu amewashukuru waandishi
wa habari kwa kazi kubwa wanayoifanya hasa kwa kuzingatia kuwa hija hii
ni ndefu na ya kihistoria, kwani anapenda kukutana na kuzungumza na
ndugu yake Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima. Anapenda kwenda
kusali na kumsalimia Bikira Maria wa Guadalupe, ili kushangaa Fumbo la
upendo wa Mungu linalofumbatwa katika maisha ya wengi.
Baba Mtakatifu amechukua nafasi hii
kwa namna ya pekee kumshukuru Dr. Albeto Gasbarri ambaye kwa muda wa
miaka 47 amejisadaka kwa kazi na utume mbali mbali mjini Vatican. Kwa
muda wa miaka 37 ameratibu hija za kitume za viongozi wakuu wa Kanisa
sehemu mbali mbali za dunia. Tangu wakati huu, Monsinyo Mauricio Rueda
atakuwa mratibu mpya wa hija za kitume za viongozi wa Kanisa mjini
Vatican. Dr. Gasbarri anatarajiwa kung’atuka rasmi kutoka katika uongozi
hapo tarehe 29 Februari 2016.
Waandishi wa habari kutoka Mexico
wamemzawadia Baba Mtakatifu kofia ya kitamaduni kutoka Mexico kama
walivyofanya kwa Mtakatifu Yohane Paulo II miaka 37 iliyopita na kwa
Papa Mstaafu Benedikto XVI na sasa kwa Baba Mtakatifu Francisko. Baba
Mtakatifu amewashukuru na kuwatakia wote kazi na utume mwema wakati huu
wa hija yake ya kitume nchini Mexico.
Week Hot newz
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
A Prayer for a Family O dear Jesus, I humbly implore You to grant Your special graces to our family. May ou...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kut...
-
Baba Mtakatifu Francisko wakati akirejea kutoka Armenia a...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
MOROGORO,TANZANIA. MSANII wa bongo fleva na mkali wa kurap kwa lugha 31 Batarokota, amesema tangu alipofariki mke wake mpendwa mwaka ...
-
Siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba tareehe 21/05/2016 katika jijini la mawe Mwanza (Rocky City) kutakuwa na burudani kabam...
-
Pichani juu msanii wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota akiwa katika Hoteli ya Misana aliyofikia jijini Mwanza.. MSANII wa ny...
-
KUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi. Changamoto hizo zimes...