TAASISI ya Bilal Muslim Mission of Tanzania imewashauri Watanzania
kujitolea damu salama ili kuokoa maisha ya wengi wanaohitaji damu
hospitalini.
Ombi hilo limetolewa juzi na Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Sibtain
Meghji, alipozungumza wakati wa utoaji damu salama, tukio
lililofadhiliwa na taasisi hiyo jijini Mwanza.
Meghji alisema utoaji damu salama unatakiwa kufanywa na kila mtu
mwenye sifa ili kuisaidia jamii iliyopo hospitalini ikihitaji huduma
hiyo muhimu.
“Sote tunajua kwamba damu ni kiungo muhimu kwa mwili wa mwanadamu…
kwa hiyo mimi naomba sana Watanzania wote tujenge hulka ya kujitolea
damu mara kwa mara kwa ajili ya ndugu zetu,” alisema Meghji.
Alisema kila mwaka taasisi hiyo ya Bilal Muslim Mission of Tanzania
kwa kushirikiana na waumini wote wa madhehebu ya Shia, wanachangia
damu, ambapo jana ilitarajiwa kupata zaidi ya watu 400.
Kwa upande wake, Ofisa Uhamasishaji wa Mpango wa Damu Salama Kanda ya
Ziwa, Vincent Muhada, alisema zaidi ya chupa 40,000 za damu salama
zinahitajika katika hospitali mbalimbali za mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Alisema mahitaji halisi ya damu salama kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa ni
chupa 70,000 lakini hadi sasa chupa 25,000 hadi 30,000 zimeshapatikana,
hivyo kusababisha upungufu wa chupa 40,000.
Week Hot newz
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Tafakari masomo Dominika, ninafurahi tena kuwa nawe katika safari yetu ya Majilio tukijiandaa kwa ajili ya ujio wa Mwana wa Mungu. Ni wak...
-
Freeman Mbowe MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofa...
-
NA OSCAR ASSENGA, TANGA-Tanzania.Gazeti Mtanzania. KATIBU wa Chama cha Watu Wenye Albino Mkoa wa Tanga (TAS), Mah...
-
Baba Mtakatifu Francisko Alhamis hii 14.11.2014 majira ya saa nne, kwa mara ya kwanza tangu kuwa Papa mwezi March mwaka huu, alifanya ziar...
-
Na Paskal Linda Ninakuletea ujumbe wa Neno la Mungu, Dominika ya 25 ya mwaka B wa Kanisa. Mama Kanisa anatufundisha wajibu wa Jumuiya ...
-
Klabu za Ligi ya Premia zilitumia zaidi ya £155m siku ya mwisho ya kuhama kwa wachezaji kipindi cha majira ya joto na kufikisha jumla y...
-
Reading 1, First Corinthians 15:35-37, 42-49 35 Someone may ask: How are dead people raised, and what sort of body do the...
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya 32 ya Mwaka B wa Kan...
-
Kardinali Pietro Parolin akisalimiana na Masista wa Upend...


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni