Wakati dirisha dogo la usajili likitarajiwa kufungwa Desemba 15, mwaka huu, Shirikisho la Soka nchini(TFF), limezikumbusha klabu zote kuheshimu kanuni na kuzingatia muda uliowekwa.
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa kitendo cha klabu kupeleka mchezaji kwa mkopo katika klabu nyingine hakutoi nafasi ya kusajili mchezaji mpya.
Tamko hilo la TFF lina maana kwamba, Yanga ambayo kwa sasa tayari imeingia mikataba ya kuwasajili kipa Juma Kaseja aliyekuwa huru na kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu Shooting, haitakubaliwa kumsajili mmoja wa wachezaji hao kwani tayari ilikuwa na wachezaji 29.
"Kama klabu ilisajili wachezaji 30 maana yake ni kuwa, haina nafasi ya kuongeza wachezaji. Kwa upande wa wachezaji wa kigeni (foreign players), tunakumbusha kuwa, kuanzia msimu ujao 2014/2015 watakuwa watatu tu badala ya watano wa sasa," alisema Wambura.
Alisema mpaka jana jioni hakuna klabu hata moja iliyokuwa imeshaingia kwenye mfumo wa TMS kuomba uhamisho wa mchezaji wa kigeni na itakapofika Desemba 15, mwaka huu mfumo huo wa TMS utafungwa.
Week Hot newz
-
Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa...
-
MOROGORO,Tanzania NYOTA wa muziki wa Bongo fleva na Mziki wa Asili ya Kitanzania nchini Tanzania,Batarokota, amesema alianza kumpend...
-
Neno Kwaresima linatokana na neno la lugha ya kilatini Quadragesima ; maana yake, namba arobaini. Kwa hiyo, Kwaresima ni kipindi cha siku ...
-
Freeman Mbowe MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofa...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Utafiti mpya umeonesha watu wazima wengi duniani ni wanene kupita kiasi na kwamba hakuna matumaini ya kufikia lengo la kupunguza idadi...
-
Klabu za Ligi ya Premia zilitumia zaidi ya £155m siku ya mwisho ya kuhama kwa wachezaji kipindi cha majira ya joto na kufikisha jumla y...
-
Tafakari masomo Dominika, ninafurahi tena kuwa nawe katika safari yetu ya Majilio tukijiandaa kwa ajili ya ujio wa Mwana wa Mungu. Ni wak...
-
Papa Francisko akihutubia kabla ya sala ya Malaika wa Bwa...
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni