Week Hot newz
-
Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana we...
-
A Prayer for a Family O dear Jesus, I humbly implore You to grant Your special graces to our family. May ou...
-
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican kipindi cha tafakari, ninakuleteeni tafakari ya Neno la Mungu Dominika ya tatu ya Majilio. Mas...
-
Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kut...
-
Baba Mtakatifu Francisko wakati akirejea kutoka Armenia a...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
MOROGORO,TANZANIA. MSANII wa bongo fleva na mkali wa kurap kwa lugha 31 Batarokota, amesema tangu alipofariki mke wake mpendwa mwaka ...
-
Siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba tareehe 21/05/2016 katika jijini la mawe Mwanza (Rocky City) kutakuwa na burudani kabam...
-
Pichani juu msanii wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota akiwa katika Hoteli ya Misana aliyofikia jijini Mwanza.. MSANII wa ny...
-
KUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi. Changamoto hizo zimes...
Vatican: Papa Francis hayuko hatarini
MAKAO Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani, yamekanusha vikali uvumi ulioenea kwamba Baba Mtakatifu, Francis, yuko hatarini kwa kuwa kundi la kimafia linamuwinda kumfanyia uhalifu kwa kile kilichoelezwa kuhusu uamuzi wake wa kufanya mageuzi katika kanisa hilo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari wa Vatican, Frederico Kardinali Lombard, alikiambia kituo cha habari cha ABC kwamba hakuna sababu za wazi zinazoweza kuwafanya kuwa na wasiwasi.
“Tuna utulivu wa kutosha, hakuna haja ya kuanza kuwekeana mashaka,” alisema.
Habari zilizonukuliwa hivi karibuni zilimtaja Nicola Gratteri anayeheshimika nchini Italia kwa msimamo wake kinyume na kundi hilo la Mafia akisema kuwa uamuzi wa Baba Mtakatifu kutaka kulifanyia marekebisho kanisa ulilikasirisha kundi hilo la kijasusi.
“Siwezi kusema kama Mafia wanaweza kufanya kitendo hiki, tunawajua kuwa ni watu hatari,” aliongeza Lombard.
Gratteri alilianyia uchunguzi wa kutosha kundi hilo lenye nguvu duniani lenye makazi yake Calabria, Kusini mwa Italia katika sehemu inayoitwa Ndrangheta.
Aliyaongea hayo kwenye kipindi cha televisheni alipokuwa anazindua kitabu chake cha maji matakatifu, kinachohusu Kanisa Katoliki na vikwazo linavyopata katika eneo hilo la Ndrangheta.
Grateri ananukuliwa akisema kuwa uamuzi wa Papa utaangusha nguvu ya kibiashara iliyoko katika mamlaka za Vatican ikiwemo Benki ya Vatican iliyokuwa inafanya biashara zilizolaumiwa kama ni za kiukoo kati ya makleri wa eneo hilo.
Ingawa kwa kiasi kikubwa mauaji yaliyokuwa yanapangwa na Mafia yamepungua kwa kiasi kikubwa tangu miaka ya 1990, matendo ya kihalifu bado yanafanywa na vikundi vinavyojihusisha na ukahaba na watumiaji wa dawa za kulevya, hayo ndio makundi hatari kwa ukuaji wa uchumi wa Italia.
Koo kubwa zinazopatikana Italia kwa sasa zinahusisha, Wasisili wa Cosa Nostra, Wakamora wanaotoka mji wa Napoli, na Kalabrian maarufu kama Ndrangheta, ambao unasadikiwa kuwa wenye nguvu katika matendo ya kihalifu, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa.
Tayari Baba Mtakatifu ameshatangaza kufanya mabadiliko makubwa katika kanisa, akitaka kanisa la kimaskini kwa ajili ya maskini, na ndani ya wiki hii ameshazungumza mara mbili katika misa zake za asubuhi akikemea vitendo vya rushwa na fedha chafu.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni