Week Hot newz

Askofu: Mtandao umemuua Mvungi

Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,Marehemu Dk. Sengondo Mvungi
Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Sengondo Mvungi, alizikwa jana katika Kijiji cha Chanjale Juu, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro huku Askofu Rogath Kimario wa Kanisa Katoliki Jimbo la Same, akiwaeleza waombolezaji kwamba marehemu amekufa kwa kifo cha fedheha kilichotokana na kile alichokiita mauaji ya kimtandao.

20 wauawa kwa shambulio

Moja ya mashambulio nchini Somalia
Karibu watu ishirini wameuawa katika shambulio la kujitoa mhanga kwenye kituo cha polisi nchini Somalia.
Shambulio hilo limetokea katika mji wa Beledweyne karibu na mpaka na Ethiopia. Mashuhuda wameiambia BBC kuwa gari lilipiga lango kuu la kuingia kwenye jengo la polisi na kulipuka kabla ya watu wenye silaha kushuka na kushambulia jengo hilo kwa risasi. Taarifa zinasema wengi waliofariki katika shambulio hilo ni maafisa wa polisi.

Cameroon yazifuata Nigeria, Ivory Coast


Cameroon imekuwa nchi ya tatu kutoka barani Afrika kufuzu kucheza kombe la dunia nchini Brazil mwaka kesho 2014 baada ya kuifunga Tunisia siku ya jumapili kwa magoli 4 - 1 katika mechi iliyopigwa mjini Younde Cameroon.
Cameroon itashiriki fainali hizo za Kombe la Dunia kwa mara ya sita tangu mashindano hayo yalipoanza ambapo sasa itaungana na Nigeria na Ivory Coast ambazo nazo zimefuzu kushiriki mashindano hayo

Tarehe 24 Novemba 2013 Papa kukabidhi Waraka wa "Furaha ya Injili"

Baba Mtakatifu Francisko katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani sanjari na Siku kuu ya Yesu Kristo Mfalme wa Ulimwengu anatarajiwa kuwakabidhi waamini Waraka Mpya wa Kichungaji, "Evangelii Gaudium" Yaani "Furaha ya Injili" kama alama ya kudumu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani. Ibada ya Misa inatarajiwa kuanza saa 4:30 kwa saa za Ulaya.

Hayo yamesemwa na Askofu mkuu Rino Fisichella, Rais wa Baraza la Kipapa la Uhamasishaji wa Uinjilishaji mpya alipokuwa anazungumza na vyombo vya habari mjini Vatican siku ya Jumatatu, tarehe 18 Novemba 2013. Mkutano huu umehudhuriwa pia na viongozi waandamizi kutoka Baraza hili.