Week Hot newz

Chadema wajifungia kujadili Ukuta


Freeman Mbowe
Freeman Mbowe

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema maandamano na mikutano itakayofanyika kuanzia Septemba mosi, mwaka huu kwa ajili ya kutekeleza operesheni ya Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta) haina lengo la kumjaribu mtu yeyote bali inakusudia kupinga ukiukwaji wa misingi ya Katiba na uvunjaji wa sheria za nchi.