
Adhabu hii imewashtua watetezi wa haki msingi za binadamu, kwa kuitaka Serikali ya Sudan kuheshimu uhuru wa kuabudu kadiri ya Katiba ya nchi iliyotungwa kunako Mwaka 2005.
Mahakama hiyo imetumia "Sharia" za dini ya Kiislam zilizoingizwa nchini humo kunako mwaka 1983 zinazopiga rufuku kwa mwamini wa dini ya Kiislam kuoa au kuolewa na Mkristo. Viongozi mbali mbali wa Jumuiya ya Kimataifa wameitaka Serikali ya Sudan kuingilia kati ili kusitisha utekelezaji wa adhabu hii ambayo ni kinyume cha haki msingi za binadamu.