Week Hot newz

Uhaba wa dawa unavyowatesa wagonjwa wa saratani


Mtu aliyeathirika na saratani ya kinywaKUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi.
Changamoto hizo zimesababisha wagonjwa hao kukata tamaa ya kuendelea na matibabu na kuamua kukatisha dozi na kurudi majumbani mwao.
Hali hiyo hutokea baada ya kuchoka kuhangaika kutafuta fedha za kumudu gharama za dawa huku wakizidi kunyanyasika wakiwa ugenini kwa kuja hospitali ya Ocean Road (ORCI) ambayo inashughulikia tiba na uchunguzi wa ugonjwa huo.
Changamoto kubwa ambayo waathirika wengi wanaomba kusaidiwa ni pamoja na upatikanaji wa dawa aina ya Chemotherapy ambayo hupewa kama tiba katika hospitali hiyo.
Akizungumza hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa Chama cha Matumaini ya Mwanamke, mmoja wa wagonjwa hao, Bihuda Shaiza, anasema huwa wanaambiwa dawa hizo ni bure lakini wanapoziulizia mara nyingi huambiwa zimeisha hivyo hulazimika kununua kwenye maduka ya nje ambako huuzwa ghali.
“Nimelipia dozi hiyo mzunguko wa kwanza kwa shida sana kwa gharama ya Sh 200,000 baada ya kuambiwa dawa hiyo haipatikani hospitalini, hapa nilipo sijui dozi ya pili na ya tatu nitaipata vipi,”anasema Shaiza.

Batarokota: Tusimsimange Chid Benz mitandaoni

MKURUGENZI wa Batarokota Daily Gospel Newz pia msanii wa nyimbo za bongo fleva nchini Tanzania, Paskal Linda ‘Batarokota ’, amewataka wadau wa muziki, wasanii na Watanzania kwa ujumla kuacha kumsimanga msanii, Chid Benz ambaye ameathirika na matumizi ya dawa za kulevya kwa kuwa ni mambo yanayoweza kumtokea mtu yeyote.

Batarokota alisema kwa sasa msanii huyo yupo mikono salama chini yake akiwa chini ya uangalizi wa kituo cha Life And Hope Rehabilitation Organization, kilichopo Ukuni huko Bagamoyo akipambana kuachana na matumizi ya dawa za kulevya.

Batarokota alisema yeye kama mdau wa muziki wa Bongo Fleva na  anasaidia wasanii wengi ili wapate mafanikio kupitia muziki na kwenye matatizo pia anawasaidia.
“Nimechukua jukumu la kumsaidia Chid Benz, naomba Watanzania tumuombee aweze kupona na si kumchafua kupitia mitandao,” alieleza Batarokota.