Week Hot newz

Umefunga na nani pingu za maisha?


Tupo bado kwenye chumba cha karamu ya mwisho tukisikiliza Wosia wa Yesu. Lugha inayotumika leo ni ya kimahaba, yaani, lugha ya upendo wa dhati kama ile ya wanandoa wanaopendana. Lugha hiyo ndiyo anayoitumia Yesu anapoagana na wafuasi wake, na kuwafanya kuhamasika kumsikiliza.

Katika Wosia huo ulio katika sura tano za Injili, neno upendo linatumika mara ishirini na sita. Kwa mara ya kwanza unalikuta kwenye fasuli ya leo: “Mkinipenda, mtazishika amri zangu,” au vizuri zaidi lingetumika neno: “Kama” mkinipenda. Namna hii ya kuongea kwa upande wa Yesu ni ya kinyenyekevu, ya kuaminia, ya saburi na ya kujali, yaani inajali sana uhuru na hiari ya yule anayeambiwa; kama vile angesema: “Yote yanakutegemea wewe”.

Hiyo ni lugha huru ya Yesu aliye huru. Yesu anatumia lugha ya maelewano na ya makubaliano. Kama sote tujuavyo kwamba mambo mengine yanaweza kutendeka kirahisi, kwa ari na kwa moyo wote endapo yanafanyika kwa hiari, wasemavyo waswahili: “Ukipenda utakula nyama mbichi”.

Injili ya leo ina aya saba na kwa mara saba katika kila aya Yesu