Week Hot newz

Marufuku kujisajili kwenye Ufalme wa Shetani!

Wapendwa wanafamilia ya Mungu, karibuni kwa tafakari ya Neno la Mungu, inayotujia tunapoadhimisha leo Sherehe ya Bwana wetu Yesu Kristo Mfalme. Mama Kanisa anatualika tumtafakari Kristo ambaye ni Mfalme wa Ulimwengu na pia kielelezo halisi cha Mfalme wa kweli ambaye ni tofauti na wafalme wa dunia hii.


Tofauti na miaka mingine, kwa mwaka huu adhimisho hili la Sherehe ya Kristo Mfalme linaambatana na hitimisho rasmi la Mwaka wa Imani. Hivyo ni nafasi nzuri kwetu kujikumbusha kuwa Imani ya kweli ni ile ambayo inajengeka katika Kristo Mwenyewe ambaye atatupa tuzo la kushiriki maisha katika ufalme wake wa mbinguni kadiri ile ambavyo tumejibidisha kuiishi imani yetu na kwa jinsi tulivyomruhusu awe Bwana na Mtawala wa maisha yetu.

Wakatekumeni wanaalikwa: kusikiliza kwa makini, kukutana na kutembea na Yesu!

Katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, Jumamosi jioni tarehe 23 Novemba, 2013, Baba Mtakatifu Francisko kwa furaha kuu aliwapokea waketekumeni 500 kutoka katika nchi 47 walioanza safari ya kujenga Fumbo la Mwili wa Kristo yaani Kanisa kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo. Anasema, Neno wa Mungu alifanyika mwili ili kumkomboa mwanadamu kutoka katika lindi la dhambi na mauti na kwa njia ya Ubatizo, mwamini anakufa na kufufuka pamoja na Kristo tayari kuanza hija ya maisha mapya.

Wakatekumeni hao baada ya kumtafuta Mwenyezi Mungu, sasa wako tayari kuonja huruma na upendo wake katika maisha yao na kwamba,