Bw Sanders alishinda Kansas na Nebraska
Bernie Sanders amemshinda Hillary Clinton katika mchujo wa chama cha Democratic uliofanyika katika jimbo la Maine.
Baada ya 91% ya kura kuhesabiwa, seneta huyo wa Vermont ana 64%, huku Clinton akiwa na 36%.Katika chama cha Republican, Marco Rubio ameshinda kwa urahisi mchujo katika eneo la Puerto Rico, na kumbwaga bilionea Donald Trump.