Week Hot newz

Sheikh Hassan Bashir amwagiwa tindikali!



IMAMU wa Msikiti wa Sawiyatu Qadiria, Hassan Bashir (33) amejeruhiwa vibaya usoni na sehemu ya bega la kushoto baada ya kumwagiwa kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni tindikali.
Akizungumza na akiwa kwenye wodi ya wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru anakopatiwa matibabu, imamu huyo alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya kati ya saa 3:30 na saa 4:00 usiku karibu na Msikiti wa Tindiga, uliopo eneo la Unga Ltd.
Alisema ana maumivu makali sehemu ya uso pamoja na bega la upande wa kushoto.
Sheikh huyo ambaye alikuwa akizungumza kwa shida kutokana na maumivu makali, alisema alikumbwa na mkasa huo muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo na babu yake ambaye pia ni Mwenyekiti wa Msikiti, Ismail Olomi na Mwenyekiti wa Ujenzi, Abdalah Kaduma, juu ya maandalizi ya Maulid yanayotazamiwa kufanyika msikitini hapo.
 “Tulipomaliza kuzungumza mimi nikawa

Maaskofu KKKT Karagwe wacharuka Mchungaji Kanyiginya, kunyimwa dhamana


Mchungaji  Jackson Kanyiginya 

MAASKOFU, wachungaji na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, wamecharuka na kuvamia Kituo cha Polisi cha Karagwe wakipinga Mchungaji wao, Jackson Kanyiginya, kunyimwa dhamana katika mazingira tata na kuswekwa rumande.
Mchungaji huyo ambaye jana alipandishwa kizimbani kwa kosa la kumpiga mfanyabiashara, Joseph Gareba, alinyimwa dhamana baada ya Mwendesha Mashitaka, Meja Juma Litafa, kuzikataa barua za wadhamini hadi azifanyie uhakiki.
Akizungumza na gazeti hili kutoka Karagwe jana, Askofu mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe, Bagonza, alisema mchungaji Jackson  alikuwa kwenye mkutano na viongozi wote wa kanisa hilo kwa ajili ya kufanya mafungo.
Alisema akiwa katika kituo cha mafungo, alipata wito wa polisi wa kumtaka afike mahakamani juzi kwa ajili ya kujibu kesi iliyofunguliwa kwa siri ya

Sunday Gospel Feb 16 2014



In this week's edition of There's More in the Gospel than Meets the Eye, Jill Bevilacqua and Seàn-Patrick Lovett bring us readings and reflections for the Sixth Sunday of the Year.
Listen: RealAudioMP3

Gospel Mt 5:20-22A,27-28,33-34, 37

Jesus said to his disciples:
“I tell you, unless your righteousness surpasses
that of the scribes and Pharisees,
you will not enter the kingdom of heaven.

“You have heard that it was said to your ancestors,
You shall not kill; and whoever kills will be liable to judgment.
But I say to you,
whoever is angry with brother
will be liable to judgment.

“You have heard that it was said, You shall not commit adultery.
But I say to you,
everyone who looks at a woman with lust
has already committed adultery with her in his heart.

“Again you have heard that it was said to your ancestors,
Do not take a false oath,
but make good to the Lord all that you vow.
But I say to you, do not swear at all.
Let your ‘Yes’ mean ‘Yes,’ and your ‘No’ mean ‘No.’
Anything more is from the evil one.”



Text from page http://en.radiovaticana.va/news/2014/02/13/sunday_gospel_feb_16_2014/en1-772758
of the Vatican Radio website

Miaka 83 tangu kuanzishwa kwa Radio Vatican



Radio Vatican, Mama wa Radio zote duniani, tarehe 12 Februari 2014 imeadhimisha kumbu kumbu ya Miaka 83 tangu ilipoanzishwa. Inajivunia kuwa ni kati ya wadau wakuu wa Shirikisho la Watangazaji Barani Ulaya, EBU ambalo tarehe 13 Februari 2014 linaadhimisha Siku ya Radio Duniani. Kwa namna ya pekee, Jumuiya ya Kimataifa kwa mwaka huu, inajielekeza zaidi katika kuangalia mchango wa wanawake katika medani mbali mbali za maisha.

Watangazaji wanawake kutoka Radio Vatican wamekuwa mstari wa mbele kwa kuwa ni sauti ya wanawake wasiokuwa na sauti kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Radio Vatican katika mtandao wake imeandaa programe mbali mbali zinazoonesha mchango wa Radio Vatican katika kuwawezesha wanawake Barani Afrika, Asia na Amerika.

Hizi ni programme zinazoonesha ujasiri wa wanawake katika kukabiliana na changamoto mbali mbali za maisha: katika masuala ya maendeleo endelevu, haki na amani duniani. Ukitaka kufaidi zaidi unaweza kutembelea katika tovuti rasmi ya Radio Vatican kwa anuani ifuatayo: www.radiovaticana.va
Unaweza pia kuwashirikisha jirani zako.