Week Hot newz

Braeking news:20 wafariki katika ajali ya treni


Treni
Maafisa wa huduma za treni nchini India wanasema kuwa takriban watu 20 wanahofiwa kufariki katika ajali ya gari moshi katika jimbo la Uttar Pradesh.
Treni hiyo ya kubeba abiria iligongana na treni ya jizigo iliyokuwa imeemgeshwa katika kituo cha treni cha Chureb.
Mabehewa sita ya treni hiyo ya Gorakhdham Express yaling'oka kutoka kwenye treni hiyo.
Waokozi wanajaribu kuwaokoa abiria waliokuwa ndani ya treni hiyo na ambao bado wamekwama.
Treni hiyo ilikuwa inasafiri kutoka mjini Gorakhpur hadi katika jimbo la Hisar Haryana

Bikira Maria linda familia, vijana na wazee!



Baba Mtakatifu Francisko Jumapili tarehe 25 Mei 2014 baada ya maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu kwenye Uwanja wa Pango la Mtoto Yesu mjini Bethlehemu, amesali pamoja na waamini Sala ya Malkia wa Mbingu, mahali hapa ambapo Bikira Maria alimzaa Mtoto Yesu, akapata nafasi ya kuutafakari uso wa Yesu kuliko mtu mwingine yoyote duniani. Akasaidiwa na Mtakatifu Yosefu kumlaza Mtoto Yesu katika Pango la kulishia wanyama!

Baba Mtakatifu amewaweka wananchi na wakazi wote wa eneo hili chini ya ulinzi na tunza ya Bikira Maria, ili waweze kuishi katika haki, amani na udugu. Amewaweka pia mahujaji wote wanaotoka sehemu mbali mbali duniani kuja mjini Bethlehemu ili kujichotea neema kutoka kwenye kisima cha imani ya Kikristo, chini ya ulinzi wa Bikira Maria.

Baba Mtakatifu anamwomba Bikira Maria kulinda familia, vijana na wazee; kuwasaidia wale ambao wamepoteza imani na matumaini; awafariji wagonjwa, wafungwa na wote wanaoteseka; awaimarishe viongozi wa dini na Jumuiya nzima ya waamini, ili kweli waweze kuwa ni chumvi na mwanga wa katika Nchi hii. Baba Mtakatifu anamwomba Bikira Maria alinde huduma za elimu zinazotolewa katika eneo hili, lakini zaidi kutoka Chuo Kikuu cha Bethlehemu.

Baba Mtakatifu anapotafakari kuhusu Familia Takatifu, mawazo yake yanakwenda moja kwa moja mjini Nazaret ambako anatamani kwenda kutembelea Mwenyezi Mungu akipenda wakati mwingine tena. Ameonesha upendo na mshikamano wake kwa waamini wote wanaoishi katika eneo hili. Anamwomba Bikira Maria asaidie mchakato wa ujenzi wa udugu, mshikamano na amani
!

Roho Mtakatifu ni kocha wa maisha ya kiroho!


Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican inapenda kukushirikisha utajiri wa tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya Vi ya Kipindi cha Pasaka inayomwonesha Roho Mtakatifu kuwa kweli ni kocha na mwalimu wa maisha ya kiroho! Kazi kwako!

Katika Injili NENO KUPENDA/PENDO linatawala – hivi unajisikiaje unapoambiwa nakupenda au unapohisi kuwa unapendwa? Hakika kupenda kunawajibisha - tamko hilo lasubiri jibu. Wengi wetu twafahamu fika jinsi ilivyo vigumu kupenda upeo/kweli. Upendo unadai matendo. Kinachofuata ni wajibu.


Ndicho kinachoonekana katika masomo yetu ya leo = kutii amri na kuabudu. Ndiyo maana Yesu anaweza kusema mkinipenda mtazishika amri zangu. Mtakatifu Tomas wa Akwino - sheria za Mungu ni nyepesi kwa wapendao na mzigo kwa wasiopenda.

1 Jan 4,8 yeye asiyependa hakumjua Mungu kwa maana Mungu ni upendo -hivyo ili kupenda vizuri ni lazima kumjua Mungu sababu yeye ni PENDO. Mapendo ya kweli yadai sadaka. Ili kushika amri au sheria inavyotakiwa yahitaji sadaka kubwa na inayodai utumishi.

Mt Agustino anapotafakari juu ya upendo wa Mungu anasema - umegusa mioyo yetu kwa pinde za upendo wako na akili zetu kwa mishale ya neno lako.

Baada ya utangulizi na kusikia masomo