Week Hot newz

Askari simameni kidete kulinda amani, sheria, demokrasia na haki msingi


Baba Mtakatifu Francisko akizungumza na Jeshi la Polisi Italia. - OSS_ROM
21/05/2015 15:07
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 21 Mei 2015 amekutana na kuzungumza na ndugu na jamaa ya Askari waliopoteza maisha yao wakati wakitoa huduma kwa nchi yao ya Italia. Amewashukuru kwa ushuhuda wa matumaini ya Kikristo yanayowasaidia katika utekelezaji wa dhamana yao kama Askari, huku wakitekeleza wajibu wao katika uaminifu unaolenga mafao ya wengi; ujasiri unaosaidia makuzi ya mtu na jamii inayomzunguka pamoja na kuunza mazingira yanayowawezesha watu kuishi katika uhuru na kwa kuheshimiana