Week Hot newz

Saratani ya mlango wa kizazi tatizo Tanzania


Rais Jakaya Kikwete, amesema Tanzania inatambulika kuwa ni moja ya nchi zenye kiwango kikubwa cha maradhi ya saratani ya mlango wa kizazi  Afrika ya Mashariki na kwamba inakadiriwa kuwa takriban wanawake 56 katika kila wanawake 100,000, hupata saratani hii.

Kadhalika, inakadiriwa pia kuwa zaidi ya watu 35,000 hupata saratani hiyo kila mwaka na zaidi ya watu 27,000 hupoteza maisha huku ripoti ikionyesha mwaka 2010 peke yake, wanawake 6,000 waligundulika kuwa na saratani ya mlango wa kizazi na  4,000 kati yao walikufa kutokana na maradhi hayo.

Rais Kikwete aliyasema hayo wakati akizungumza

Roho Mtakatifu anafundisha, anakumbusha, anasali na kufanya unabii!

Baba Mtakatifu Francisko katika maadhimisho ya Siku kuu ya Pentekoste, tarehe 8 Juni 2014 kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican wakati wa mahubiri yake anasema kwamba, Yesu aliwaahidia Mitume wake zawadi kutoka kwa Baba, yaani Roho Mtakatifu na ahadi hii inatekelezwa wakati wa Siku kuu ya Pentekoste.

Hili ni tukio endelevu linaojionesha katika maisha na utume wa Kanisa, kwani Roho Mtakatifu analihuisha Kanisa, anawafundisha, anawakumbusha na kuwasaidia waamini kuzungumza.

Papa Francisko anasema, Roho Mtakatifu ni mwalimu wa maisha yandani anayewaonesha waamini dira na njia ya maisha kama alivyofanya wakati wa Kanisa la mwanzo. Roho Mtakatifu ni njia kama alivyo Yesu mwenyewe, kwani anawasaidia waamini kumfuasa Kristo na kutembea katika nyayo zake. Roho Mtakatifu ni mwalimu wa maisha, ujuzi na maarifa katika uwepo na utume wa maisha ya Kikristo.

Roho Mtakatifu anawakumbusha waamini yale ambayo Yesu