Week Hot newz

Historia ya Kanisa la Sabato (4)

NDUGU yangu, ninatumaini nimekufikisha mahali pazuri. Hiyo ndiyo historia ya mshazari wa Kanisa la Wasabato. Kifupi haina mashiko na mtiririko wa kimantiki. Hata hivyo baada ya kuzaliwa kimtindo namna hiyo, Kanisa la Wasabato halikubaki moja kifikra na kimtazamo. Ukilichungulia ndani, Kanisa la Wasabato ni Muungano wa Vikundi vitatu vya Waadventisti; Kikundi cha Bw. Hiram Edson, kilichosisitiza zaidi mafundisho ya huduma ya Yesu Patakatifu pa Patakatifu mbinguni, Kikundi cha Bw. Joseph Bates, kilichosisitiza zaidi kufuata Sabato ya Agano la

Mwanamke Aadhibiwa kwa kumtelekeza mume


Roseline anadaiwa kuwatelekeza watoto wake wanaoishi na baba yao
Na Paskal Linda-Kenya.
Mwanamke mmoja nchini Kenya ameamrishwa na mahakama kumlipa mumewe shilingi elfu tatu au dola 35 kama hela za kukidhi mahitaji yake na watoto wake kila mwezi.
Mwanamke huyo kwa jina Roselyn Muyonga, ambaye anatuhumiwa kwa kuwatelekeza mumewe na watoto wake watatu , huenda akafungwa miezi mitano jela au kutozwa faini ya shilingi laki mbili ikiwa atakosa kutekeleza amri ya mahakama.
Mwanamume huyo hufanya kazi za kibarua.

Kila toba ni Pentekoste Mpya!

 Na: Paskal LindaKardinali Mauro Piacenza, mhudumu mkuu wa Toba katika barua yake kwa mapadre waungamishaji anasema kwamba, kila mara Mkristo anapoungama dhambi zake na kupokea msamaha, huruma na upendo wa Mungu kutoka kwenye kiti cha maungamo, kwa Mkristo hii ni Pentekoste Mpya! Siku kuu ya Pentekoste, ili ni fursa kwa waamini kujipatanisha na Mungu pamoja na jirani zao, ili kuweza kumpokea vyema Roho Mtakatifu anayemiminwa mioyoni mwao, tayari kumtolea Mwenyezi Mungu ushuhuda wa maisha adili na matakatifu!

Neema ya Sakramenti ya Upatanisho anasema Kardinali Piacenza ni mang'amuzi mapya ya Pentekoste kwani hapa Roho Mtakatifu anaendelea kulitakasa Kanisa la Kristo kwa njia ya huduma ya maungamo inayotolewa na Padre akiwa ameungana na Yesu Kristo, ili kusikiliza na kupima, kuamua na kutoa ushauri na hatimaye, kuponya dhambi kwa kumwondolea mwamini dhambi zake. Hii ni kazi ya Roho Mtakatifu anayetenda kwa njia ya wachungaji wake wanaojisadaka katika viti vya maungamano.

Mapadre wanakumbushwa kwamba, wamechaguliwa na kuwekwa wakfu kwa ajili ya kuwahudumia watu wa Mungu si kwa mastahili yao wenyewe bali kwa njia ya neema ya Roho Mtakatifu inayowaunganisha kwa dhati kabisa na Kristo mwenyewe, ili kushiriki upendo na kazi yake ya ukombozi. Kwa sababu hii, Padre ni mhudumu wa huruma ya Mungu na daraja kati ya waungamaji na Kristo mwenyewe.

Mapadre wanachangamotishwa na Mama Kanisa kuwa wasikivu kwa Roho Mtakatifu na karama zake zinazoliwezesha Kanisa kujitakasa na kuwatakatifuza watoto wake kwa njia ya Sakramenti ya Upatanisho!

Upendo kwa Mungu na jirani!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
 
Baba Mtakatifu Francisko katika utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro amegusia mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa kwa kukazia zaidi na zaidi kanuni maadili na utu wema; utu na heshima ya binadamu; tunu msingi za maisha ya ndoa na familia: Yote haya ni kadiri ya Mafundisho ya Kanisa Katoliki na Kweli za Kiinjili na wala hakuna mabadiliko! RealAudioMP3

Baba Mtakatifu Francisko anapozungumzia masuala haya kwa unyenyekevu mkubwa kutokana na uzoefu wake katika shughuli za kichungaji kuna baadhi ya watu wanapata hisia kwamba, pengine anataka kubadilisha mafundisho na msimamo wa Kanisa Katoliki katika masuala haya, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, anachofanya ni kuendelea kukazia masuala haya kwa mwelekeo mpya zaidi!