Week Hot newz

Ufoo Saro: Niliokoka kufa kutokana na miujiza ya Mungu

Mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro akisoma somo kwenye biblia wakati wa ibada maalumu ya shukrani kwenye Kanisa la (KKKT ) Usharika wa Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dare Salaam jana. Picha na Sanjito Msafiri.


Baba Mtakatifu atoa dawa ya maisha ya kiroho



Jumapili iliyopita tarehe 17 Novemba 2013 wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, waamini na mahujaji waliokusanyika ili kuungana na Baba Mtakatifu Francisko kwa Tafakari na Sala ya Mchana, walipewa tiba ya maisha ya kiroho, itakayowasaidia katika kumwilisha mafanikio ya Mwaka wa Imani.

Yatakayojiri wakati wa kufunga Mwaka wa Imani:

Mama Kanisa anajiandaa kufunga rasmi Mwaka wa Imani, uliotangazwa na kuzinduliwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita na kuendelezwa kwa ari na moyo mkuu na Papa Francisko hapo tarehe 24 Novemba 2013, wakati wa Sherehe ya Kristo Mfalme. Ibada hii inatarajiwa kuongozwa na Baba Mtakatifu Francisko, kuanzia saa 4:00 asubuhi kwa saa za Ulaya. Maadhimisho ya kufunga Mwaka wa Imani yataanza rasmi kwa