Week Hot newz

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya 20 ya Mwaka C wa Kanisa


Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuushuhidia ukweli, ambao umekuwa ni sababu ya kugawanyika kwa walimwengu kwani wanataka kutembea katika giza la dhambi na mauti. - RV
11/08/2016 16:08
Ukweli ni uthibitisho wa kitu chochote au tukio lolote lile kadiri ya uhalisia wake. Kwa mfano ukweli kuhusiana na maji katika hali ya kimiminika ni kwamba yanapokutana na mteremko na hakuna kizuizi chochote basi yatatiririka kuelekea chini. Kwa maneno mengine ukweli unatupeleka katika kuutafakari ulimwengu huu kadiri ulivyopangwa na kuumbwa na Mwenyezi Mungu. Hivyo ukweli huo ambao huelezewa kwetu kwa njia ya neno lake unabaki daima kama ulivyo na kamwe hauwezi ukabadilika kama asemavyo Mungu kwa kinywa cha Nabii Isaya kwamba: “Majani yakauka, ua lanyauka; Bali neno la Mungu wetu litasimama milele” (Is 40:8).