Week Hot newz

Magufuli aapisha wakuu wa Mikoa, awaonya


RAIS Dk John Pombe Magufuli amewaapisha wakuu wa mikoa aliowateua hivi karibuni na kuwapa maagizo mazito. Rais amewaambia wakafanye kazi ya kutatua kero za wananchi na sio kwenda kufanya siasa.
Katika hotuba yake fupi kwao, Rais amewapa wakurugenzi wa halmashauri siku 15 wawatoe katika Orodha ya Malipo ya Mshahara (Pay Roll) wafanyakazi hewa wote katika halmashauri zote nchini.
Ameonya kuwa halmashauri yoyote baada ya muda huo itakayokuwa na mfanyakazi hewa, mkurugenzi wake atakuwa amejifuta kazi mwenyewe.
Vilevile Rais amewaagiza mawaziri wokati wowote kuwaeleza watendaji wao wawaondoe wafanyakazi hewa wote ndani ya kipindi hicho cha siku 15 na kubainisha kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo watafukuzwa kazi kwani sheria ni msumeno.
Rais ameeleza matumaini yake kuwa kupitia kwa wakuu hao wa mikoa, kero nyingi zitamalizwa na wananchi watakuwa huru katika nchi yao. Baadhi ya kero ambazo Rais amezigusia ni migogoro ya wafugaji na wakulima, ukosefu wa usalama barabarani hadi mabasi kusindikizwa na polisi pamoja na tatizo la njaa.

Jua lanaswa na mwezi Indonesia

Raia Indonesia wameshuhudia jua likizibwa kikamilifu na mwezi.

wiki hii siku ya tarehe 9 Marchi 216 Indonesia ndio nchi pekee iliyoshuhudia tukio hilo kote duniani.
Hoteli zilizopo katika maeneo mazuri ya kushuhudiwa jua likinaswa zilijaa miezi kadhaa iliopita na katika baadhi ya maeneo ilibidi maafisa watafute nafasi za ziada kwa watalii waliokuwa kwenye maboti.
Katika kisiwa cha Belitung mamia ya wageni na watalii wa nchni walikusanyika katika fukwe za bahari kabla ya alfajiri. Wakati jua lilipoanza kunaswa na mwezi walishangilia na baadaye kunyamaza kimya kwa mshangao.
Wengi wamelielezea tukio hilo kama 'tukio la miujiza'. Kwa wengi Indonesia, tukio hilo linashirikishwa sana na dini na watu huomba, sherehe za kitamaduni na ngoma zimeandaliwa katika sehemu kubwa la eneo hilo.
Wanasayansi pia wamkuwepo hususan katika eneo la Maba katika visiwa vya Maluku ambako tukio hilo limeshuhudiwa kwa dakika tatu, ambao ni muda mrefu kuwahi kushuhudiwa jua likinaswa na mwezi.

Korea Kaskazini kufanyia majaribio nyuklia!


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametangaza kwamba taifa hilo litafanyia majaribio silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu karibuni.

Amesema majaribio hayo yataimarisha uwezo wa taifa hilo kutekeleza mashambulio ya nyuklia, vyombo vya habari vya serikali nchini humo vimeripoti.