Week Hot newz

Idadi ya waamini na mahujaji waliokutana na Papa Francisko kwa Mwaka 2013 imeongezeka!

Takwimu zinaonesha kwamba, tangu Baba Mtakatifu Francisko alipochaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki hapo tarehe 13 Machi 2013, zaidi ya watu millioni sita wamekutana na kushiriki katika matukio mbali mbali yaliyoendeshwa na Baba Mtakatifu katika kipindi hiki hadi kufikia mwanzo mwa Januari 2014. Waamini, mahujaji na wageni walioshiriki katika katekesi zake zinazotolewa kila Jumatano walikuwa ni1, 548, 500.


Baba Mtakatifu alifanikiwa kukutana na kuzungumza na watu 87, 400 kwa faragha. Waamini na mahujaji wapatao 2, 282, 000 walishiriki katika Ibada mbali mbali zilizoongozwa na Baba Mtakatifu Francisko kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro na ndani ya Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican. Waamini zaidi ya 2, 706, 000 wameshiriki katika Sala ya Mchana na Baba Mtakatifu Francisko.

Takwimu hizi ni zile tu zilizokusanywa mjini Vatican na wala hazihusishi matuko kama: Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013yaliyofanyika nchini Brazil, kule Rio de Janeiro; wala safari zake za kichungaji ndani ya Italia, Lampedusa, Cagliari na Assisi hata katika baadhi ya Parokia zilizoko katika Jimbo kuu la Roma.

Kwa ujumla waamini na watu wenye mapenzi mema wapatao 6, 623, 000 wamekutana na kushiriki katika Ibada, Katekesi na Sala zilizokuwa zinaongozwa na Baba Mtakatifu Francisko. Itakumbukwa kwamba, idadi hii ya watu ni ile tu ambayo ni rasmi kwa wale watu walioomba tiketi kutoka Vatican. Kumekuwepo na umati mkubwa wa watu wanaomiminika kwenye matukio mbali mbali anayoshiriki Baba Mtakatifu Francisko, hii inatokana na mvuto alionao kwa watu!


Uraibu wa sigara wawavutia wengi


Athari za uvutaji sigara
Idadi ya wavutaji wa sigara duniani imeongezeka kwa karibu bilioni moja kwa mujibu wa takwimu mpya.
Watafiti walioandika katika jarida la Shirika la madaktari la Marekani wanasema hata hivyo kuwa idadi hiyo ni ndogo ikilinganishwa na ongezeko la watu kwa ujumla duniani na kuelezea haja ya juhudi zaidi kufanyika kuwazuia watu kuwa na tabia hiyo.
Idadi ya watu wanaovuta sigara kila siku duniani imepanda kwa kiwango cha watu takriban milioni 250 million kati ya mwaka 1980 na 2012, kwa mujibu wa ripoti .