Week Hot newz

Mshikamano wa upendo na Wakristo huko Mashariki ya Kati!


Ijumaa kuu Kanisa linakumbuka mateso na kifo cha Kristo Msalabani, chemchemi ya upendo na huruma ya Mungu kwa waja wake! - REUTERS

Kardinali Leonardo Sandri, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makanisa ya Mashariki anasema kuna haja ya kujenga na kudumisha utamaduni wa watu kukutana na kusaidiana ili kuondokana na mantiki ya ubinafsi na kuta za utengano ambazo hazina mashiko wala tija kwa watu wanaoishi huko Mashariki ya Kati. Misaada inayotolewa na Jumuiya ya Kimataifa haina budi kuwafikia walengwa huko: Mashariki ya Kati hasa Syria na Iraq.