Week Hot newz

Tafakari ya Neno la Mungu, Sherehe ya Bikira Maria Mama wa Mungu

Bikira Maria Mama wa Mungu na Kanisa. - RV
Na Paskal Linda.
Mpendwa, unayeitegea sikio Radio Vatican, leo Mama Kanisa anasherehekea sherehe ya Mama wa Mungu ambayo huja daima kila tarehe mosi ya mwezi Januari. Ni sherehe ya amani kwa maana Mama Maria ni Mama wa amani. Amemzaa Mkombozi mfalme wa amani na hivi Mama Kanisa anaona ni vema tukasali tukimwomba Mungu kwa njia ya Mama huyu kwa ajili ya amani ya ulimwengu. Sherehe hii ya kuombea amani duniani iliwekwa rasmi na Papa Paulo VI kunako mwaka 1968. Kwa namna ya pekee kabisa, Kanisa linaadhimisha Sherehe hii katika Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu. Kanisa linamkumbuka Bikira Maria kama Tabernakulo ya kwanza ya huruma na upendo wa Mungu na Sanduku la Agano kati ya Mungu na binadamu.

Salaam Mama Mtakatifu wa Mungu uliyemzaa mfalme mwenye kutawala mbingu na dunia daima na milele. Hii ndiyo salaam yetu kwa Mama mpendelevu Mama asiye na doa, katika sherehe hii tukufu tunapofungua mwaka mpya.