Week Hot newz

Mihadarati;Wema kunyongwa China,

Akiandika katika ukurasa wake wa Histogram, Wema alisema anachukizwa sana na kitendo hicho, kwani kinamfanya asikae kwa amani na watu walio karibu yake, na wengine wanamtenga kupitia vichwa vya habari tofauti vya magazeti, ambavyo kwa asilimia kubwa anasema vinatumika kuuzia magazeti hayo.
“Hivi karibuni kuna gazeti moja limeandika, ‘Ishu ya dawa za kulevya – Wema kunyongwa China,
aomba Watanzania kumuombea’, jamani siwezi kusema kama nina furaha, sijawahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo siku yatakuja kuandika uongo wa namna hii, kwa sababu nakaaga kimya ndio wameona ni njia ya kunionea muda wote, roho inaniuma sana,” aliandika mwanadada huyo ambaye amewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006.

Wema alifafanua kuwa kutokana na kuona hapa nchini kuna maneno mengi yasiyokuwa ya msingi, aliamua kwenda China kwa ajili ya kufanya mambo yake binafsi, lakini watu ambao hawapendi maendeleo yake wamekuwa wakimfuatilia na kuamua kumchafua katika magazeti.
“Sidhani kama nishawahi kumkosea yeyote katika maisha yangu, maskini ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu, sijawahi hata kufikiria kufanya biashara kama hii, muda uliopita niliambiwa nina pepo la ngono, leo ninalia tena kwa kuambiwa nauza madawa ya kulevya, eee Mungu nisaidie mimi,” alilalamika Wema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni