Akiandika katika ukurasa wake wa Histogram, Wema alisema anachukizwa
sana na kitendo hicho, kwani kinamfanya asikae kwa amani na watu walio
karibu yake, na wengine wanamtenga kupitia vichwa vya habari tofauti
vya magazeti, ambavyo kwa asilimia kubwa anasema vinatumika kuuzia
magazeti hayo.
“Hivi karibuni kuna gazeti moja limeandika, ‘Ishu ya dawa za kulevya –
Wema kunyongwa China,
aomba Watanzania kumuombea’, jamani siwezi
kusema kama nina furaha, sijawahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo
siku yatakuja kuandika uongo wa namna hii, kwa sababu nakaaga kimya ndio
wameona ni njia ya kunionea muda wote, roho inaniuma sana,” aliandika
mwanadada huyo ambaye amewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006.
Wema alifafanua kuwa kutokana na kuona hapa nchini kuna maneno mengi
yasiyokuwa ya msingi, aliamua kwenda China kwa ajili ya kufanya mambo
yake binafsi, lakini watu ambao hawapendi maendeleo yake wamekuwa
wakimfuatilia na kuamua kumchafua katika magazeti.
“Sidhani kama nishawahi kumkosea yeyote katika maisha yangu, maskini
ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu, sijawahi hata
kufikiria kufanya biashara kama hii, muda uliopita niliambiwa nina
pepo la ngono, leo ninalia tena kwa kuambiwa nauza madawa ya kulevya,
eee Mungu nisaidie mimi,” alilalamika Wema.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni