Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bwana Ban Ki-Moon katika salam zake za rambi rambi amesema, Afrika ya Kusini imempoteza shujaa wake; imempoteza Baba na muasisi wa taifa la Afrika ya Kusini. Jumuiya ya Kimataifa imempoteza kiongozi mashuhuri na mfano bora wa kuigwa katika kutetea na kulinda haki msingi za binadamu.
Amepambana kufa na kupona kupinga ubaguzi wa rangi, akawa ni mfano na kielelezo cha kiongozi anayetambua na kuthamini msamaha. Amesimamia usawa, uhuru, haki, amani na demokrasia ya kweli.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni