Week Hot newz

Batarokota akerwa na Uadui Kwenye Sanaa


Staa wa Bongo fleva na mziki wa asili ya Kitanzania Batarokota



Staa wa Bongo fleva na mziki wa asili ya Kitanzania  ambae mwaka jana aliingia katika kinyanganyiro cha KTMA 2014 katika katengo ya Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya kitanzania ambao wimbo wake wa kwejanga nyangisha uliingia na kuambulia patupu  , Paskal Linda Mgundu  ‘Batarokota ’ambaye hivi karibuni ameweka wazi juu ya kukerwa na namna ushabiki  wa sanaa nchini unavyopelekwa kwenye uadui na sio ushindani  kama ilivyokuwa miaka michache iliyopita.
“Kiukweli kwenye sanaa tumeanza kwenda kwenye njia mbaya sana,aina hii ya ushabiki wa mtindo wa uadui itatupeleka pabaya sana..Mashabiki wa Ali Kiba , Wema sepetu na Diamond  wanapaswa kuliona mapema tatizo hili,” alisema mkali huyo wa bongo fleva na nyimbo asili Batarokota.
Aidha , Batarokota amewaomba mashabiki wake kujiandaa kuipokea nyimbo yake mpya ya  ccm ju ambapo ndani ya songi hiyo amewashirikisha  na wasanii  L.L. J kutoka Rwanda na Castol kutoka DRS, “Ni songi kali sana itakayowavunja mbavu na kuwafundisha  naomba muinunue itakapotoka”.