
Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko kukutana na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima.
16/02/2016 14:43Baba
Mtakatifu Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima
wamekutana na kuzungumza pamoja na kutia sahihi Tamko la shughuli za
kichungaji kwa Makanisa haya mawili, ili kuanza kuandika ukurasa mpya wa
majadiliano ya kiekumene katika Millenia ya tatu ya Ukristo!
Baba Mtakatifu akishiriki chakula cha mchana na familia ya Mungu nchini Mexico.
Baba
Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico, Jumatatu tarehe 15 Februari
2016 ametembelea Kanisa kuu la san Cristòbal de las Casa na kusali humo,
ameshiriki chakula cha mchana pamoja na wawakilishi wa Familia ya Mungu
nchini Mexico pamoja na kuzungumza na kusali nao!
Mashuhuda wa Injili ya familia!
16/02/2016 10:42Baba
Mtakatifu Francisko alipokutana na familia nchini Mexico amesikiliza
shuhuda za watu waliotelekezwa na familia zao, lakini wakapata fursa ya
kuonja huruma na upendo wa Mungu kwa njia ya Kanisa; amesikiliza
mashuhuda waliokumbatia utamaduni wa kifo, leo hii wanashuhudia Injili
ya uhai!
Iweni mashuhuda wa Injili ya familia na huruma ya Mungu!
16/02/2016 10:21Baba
Mtakatifu anawaalika wanafamilia kuwa kweli ni mashuhuda wa Injili ya
familia na vyombo vya huruma ya Mungu ili kuweza kupambana na changamoto
mbali mbali zinazojitokeza katika maisha na utume wa familia; kwa
kushinda upweke na kinzani za maisha!
Onesheni ujasiri wa kuomba msamaha!
16/02/2016 10:02Baba
Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico anasema, umefika wakati wa
kujenga na kudumisha udugu, haki, mshikamano na amani; kwa kutambua
kwamba haya ni mambo msingi yanayowaunganisha binadamu kama watoto
wateule wa Mungu dhidi ya nyanyaso, dhuluma na ubaguzi!

Maskini wanapaswa kujipanga vyema kwa
kushikamana kutetea utu na heshima yao kwa kupinga ubaguzi na nyanyaso,
ili kukuza utu na heshima yao pamoja na kujipatia mahitaji msingi ya
maisha.
Changamoto za utunzaji bora wa mazingira nyumba ya wote!
15/02/2016 10:39Kardinali
Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la haki na amani anawapongeza
wenyeji wa Mexico kwa kuonesha mwanga angavu katika kulinda na kutunza
mazingira nyumba ya wote, sanjari na kuendelea kushikamana ili kupambana
na changamoto za maisha ili kudumisha utu wao!

Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic
kukamilisha utume wake kama Balozi wa Vatican nchini Russia, ameteuliwa
kuwa mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye ofisi za UN zilizoko Geneva,
Uswiss.
Askofu mkuu Ivan Jurkovic ateuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu UN, Geneva
15/02/2016 10:24Askofu
mkuu Ivan Jurkovic ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican
kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizoko mjini Geneva ili kuchukua
nafasi ya Askofu mkuu Silvano Maria Tomasi ambaye amekuwepo huko tangu
mwaka 2003. Aliwahi kuwa Balozi wa Vatican nchini Ethiopia na Eritrea.

Baba Mtakatifu Francisko ametembelea
Hospitali ya "Federico Gomez" ili kushukuru kwa huduma makini
zinazotolewa kudumisha Injili ya uhai pamoja na kuwaombea watoto
wagonjwa katika shida na mhangaiko yao!
Papa Francisko kielelezo cha faraja na matumaini kwa wagonjwa!
15/02/2016 10:07Baba
Mtakatifu Francisko, Jumapili tarehe 14 Februari 2016 ametembelea
Hospitali ya "Federico Gomez" nchini Mexico ili kumshukuru Mungu kwa
huduma inayotelewa kwa ajili ya watoto wagonjwa pamoja na kubariki kazi
njema inayofanywa na wazazi pamoja na wahudumu wa sekta ya afya!