Week Hot newz

Papa Francisko nchini Mexico

Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima kukutana.
Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko kukutana na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima.
Mapambazuko mapya ya majadiliano ya kiekumene!
16/02/2016 14:43Baba Mtakatifu Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima wamekutana na kuzungumza pamoja na kutia sahihi Tamko la shughuli za kichungaji kwa Makanisa haya mawili, ili kuanza kuandika ukurasa mpya wa majadiliano ya kiekumene katika Millenia ya tatu ya Ukristo!

 

 
 Baba Mtakatifu akishiriki chakula cha mchana na familia ya Mungu nchini Mexico.
Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico, Jumatatu tarehe 15 Februari 2016 ametembelea Kanisa kuu la san Cristòbal de las Casa na kusali humo, ameshiriki chakula cha mchana pamoja na wawakilishi wa Familia ya Mungu nchini Mexico pamoja na kuzungumza na  kusali nao!

 

Baba Mtakatifu Francisko akiwa Mexico amesikiliza shuhuda za Injili ya familia.
Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico amesikiliza shuhuda wa Injili ya familia.

Mashuhuda wa Injili ya familia!

16/02/2016 10:42Baba Mtakatifu Francisko alipokutana na familia nchini Mexico amesikiliza shuhuda za watu waliotelekezwa na familia zao, lakini wakapata fursa ya kuonja huruma na upendo wa Mungu kwa njia ya Kanisa; amesikiliza mashuhuda waliokumbatia utamaduni wa kifo, leo hii wanashuhudia Injili ya uhai!

 


Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wananchi wa Mexico kujikita katika ushuhuda wa tunu msingi za Injili ya furaha!
Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wananchi wa Mexico kuwa ni mashuhuda wa Injili ya familia.

Iweni mashuhuda wa Injili ya familia na huruma ya Mungu!

16/02/2016 10:21Baba Mtakatifu anawaalika wanafamilia kuwa kweli ni mashuhuda wa Injili ya familia na vyombo vya huruma ya Mungu ili kuweza kupambana na changamoto mbali mbali zinazojitokeza katika maisha na utume wa familia; kwa kushinda upweke na kinzani za maisha!
Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na wenyeji wa Chiapas, nchini Mexico
Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na wenyeji wa Chiapas, nchini Mexico.

Onesheni ujasiri wa kuomba msamaha!

16/02/2016 10:02Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico anasema, umefika wakati wa kujenga na kudumisha udugu, haki, mshikamano na amani; kwa kutambua kwamba haya ni mambo msingi yanayowaunganisha binadamu kama watoto wateule wa Mungu dhidi ya nyanyaso, dhuluma na ubaguzi!
Maskini wanapaswa kujipanga vyema zaidi ili kupambana na ubaguzi kwa kushikamana ili kudumisha utu wao na kupata mahitaji msingi!
Maskini wanapaswa kujipanga vyema kwa kushikamana kutetea utu na heshima yao kwa kupinga ubaguzi na nyanyaso, ili kukuza utu na heshima yao pamoja na kujipatia mahitaji msingi ya maisha.

Changamoto za utunzaji bora wa mazingira nyumba ya wote!

15/02/2016 10:39Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la haki na amani anawapongeza wenyeji wa Mexico kwa kuonesha mwanga angavu katika kulinda na kutunza mazingira nyumba ya wote, sanjari na kuendelea kushikamana ili kupambana na changamoto za maisha ili kudumisha utu wao!

 

Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic kukamilisha utume wake nchini Russia ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican UN, Geneva.
Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic kukamilisha utume wake kama Balozi wa Vatican nchini Russia, ameteuliwa kuwa mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye ofisi za UN zilizoko Geneva, Uswiss.

Askofu mkuu Ivan Jurkovic ateuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu UN, Geneva

15/02/2016 10:24Askofu mkuu Ivan Jurkovic ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizoko mjini Geneva ili kuchukua nafasi ya Askofu mkuu Silvano Maria Tomasi ambaye amekuwepo huko tangu mwaka 2003. Aliwahi kuwa Balozi wa Vatican nchini Ethiopia na Eritrea.

 

Baba Mtakatifu Francisko ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" Mexico kushukuru kwa huduma na kuwabariki watoto wagonjwa wa saratani!
Baba Mtakatifu Francisko ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" ili kushukuru kwa huduma makini zinazotolewa kudumisha Injili ya uhai pamoja na kuwaombea watoto wagonjwa katika shida na mhangaiko yao!

Papa Francisko kielelezo cha faraja na matumaini kwa wagonjwa!

15/02/2016 10:07Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili tarehe 14 Februari 2016 ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" nchini Mexico ili kumshukuru Mungu kwa huduma inayotelewa kwa ajili ya watoto wagonjwa pamoja na kubariki kazi njema inayofanywa na wazazi pamoja na wahudumu wa sekta ya afya!