Katika Injili NENO KUPENDA/PENDO linatawala – hivi unajisikiaje unapoambiwa nakupenda au unapohisi kuwa unapendwa? Hakika kupenda kunawajibisha - tamko hilo lasubiri jibu. Wengi wetu twafahamu fika jinsi ilivyo vigumu kupenda upeo/kweli. Upendo unadai matendo. Kinachofuata ni wajibu.
Ndicho kinachoonekana katika masomo yetu ya leo = kutii amri na kuabudu. Ndiyo maana Yesu anaweza kusema mkinipenda mtazishika amri zangu. Mtakatifu Tomas wa Akwino - sheria za Mungu ni nyepesi kwa wapendao na mzigo kwa wasiopenda.
1 Jan 4,8 yeye asiyependa hakumjua Mungu kwa maana Mungu ni upendo -hivyo ili kupenda vizuri ni lazima kumjua Mungu sababu yeye ni PENDO. Mapendo ya kweli yadai sadaka. Ili kushika amri au sheria inavyotakiwa yahitaji sadaka kubwa na inayodai utumishi.
Mt Agustino anapotafakari juu ya upendo wa Mungu anasema - umegusa mioyo yetu kwa pinde za upendo wako na akili zetu kwa mishale ya neno lako.
Baada ya utangulizi na kusikia masomo