Week Hot newz

Upendo kwa Mungu na jirani!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
 
Baba Mtakatifu Francisko katika utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro amegusia mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa kwa kukazia zaidi na zaidi kanuni maadili na utu wema; utu na heshima ya binadamu; tunu msingi za maisha ya ndoa na familia: Yote haya ni kadiri ya Mafundisho ya Kanisa Katoliki na Kweli za Kiinjili na wala hakuna mabadiliko! RealAudioMP3

Baba Mtakatifu Francisko anapozungumzia masuala haya kwa unyenyekevu mkubwa kutokana na uzoefu wake katika shughuli za kichungaji kuna baadhi ya watu wanapata hisia kwamba, pengine anataka kubadilisha mafundisho na msimamo wa Kanisa Katoliki katika masuala haya, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, anachofanya ni kuendelea kukazia masuala haya kwa mwelekeo mpya zaidi!

Ametuacha vibaya!

Amepaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu:

Siku arobaini baadaye ….. Mt. 1,23 – Mungu yu nasi leo tena tunasikia tamko hilo la Yesu mwenyewe.Maana yake nini? Hivyo tunaadhimisha leo uwepo wa Mungu kati yetu na uwepo wa Mungu kati yetu waoneshwa na kazi za watu wake wanaomtii Roho Mtakatifu.

I. Mdo 1,1-11
II. Efe. 1,17-23
III. Mt. 28,16-20

UTANGULIZI

Sherehe ya kanisa siku 40 baada ya sherehe ya Pasaka - kupaa mbinguni Bwana wetu Yesu Kristo. Mhubiri mmoja asema hakuna awezaye kukaa peke yake mke/mume ahitaji mke/mume mwema, mwalimu ahitaji wanafunzi wa kinyume chake nini?

Hivi pia kwa mkristo leo hii yupo Roho Mtakatifu na

Rais mpya wa Malawi aapishwa rasmi


Peter Muthirika anayeongoza chama cha DPP.
Rais mpya wa Malawi Peter Mutharika ameapishwa rasmi baaada ya kucheleweshwa kwa matokeo ya uchaguzi kufuatia madai ya udanganyifu na wizi wa kura.
Mutharika aliibuka mshindi wa uchaguzi huo baada ya kujipatia zaidi ya asilimia 36 ya kura zilizopigwa.
Rais anayeondoka mamlakani Joyce Banda alikuwa katika nafasi ya tatu.
Banda amewataka wafuasi wake kuheshimu matokeo hayo.
Mahakama kuu ilipinga ombi la kura kuhesabiwa upya baada ya Banda kudai kuwa kumekuwa na udanganyifu mkubwa katika shughuli hiyo.
Peter Mutharika aliwahi kuhudumu kama

Mchawi mtanzania jela miaka 3


Vifaa walivyopatikana navyo washukiwa walipokamatwa na polisi
Mchawi kutoka Tanzania amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu nchini Kenya kwa kumlaghai mwanamke mfanyabiashara mkenya na kumuibia shilingi milioni tisa.
Mchawi huyo alimhadaa mama huyo kuwa kwa kupitia njia za kichawi angeweza kuzifanya pesa hizo kuwa maradufu yaani milioni 18.
Bwana Amos Chipeta pia ataongezwa kifungo cha miezi tatu kwa kupatikana na vifaa vinavyoumiwa kufanya uchawi kama vile chupa, visu na ngozi ya Paka.
Kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation,

Tangazeni Injili ya Furaha kwa ari kuu zaidi!


Kamati kuu ya Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Amerika ya Kusini, CELAM, imehitimisha safari yake ya kikazi mjini Vatican iliyoanza tangu tarehe 20 hadi tarehe 28 Mei 2014 kwa kukutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko kuhusu maisha na utume wa Kanisa Amerika ya Kusini.

Katika mazungumzo na Baba Mtakatifu, Kamati kuu ya Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Amerika ya Kusini, linasema kuna haja ya kuendelea kuhamasisha waamini na watu wote wenye mapenzi mema kusoma, kutafakari na kumwilisha Waraka wa Kichungaji wa Baba Mtakatifu Francisko, Injili ya Furaha, "Evangelii Gaudium" huko Amerika ya Kusini.

Imekuwa ni fursa kwa viongozi hawa kumshirikisha Baba Mtakatifu Francisko yale yatakayojadiliwa na Maaskofu katika kongamano lao la mwaka, kuhusu familia linalotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 4 hadi tarehe 9 Agosti 2014. Baba Mtakatifu Francisko kwa kuangalia changamoto zilizopo kwa sasa anasema, pengine kuna haja ya kuadhimisha tena Sinodi Maalum kwa ajili ya Maaskofu wa Amerika ya Kusini, kama Kanisa lilivyofanya kwa Maaskofu Katoliki Barani Afrika, Sinodi iliyoitishwa kwanza kabisa na Mtakatifu Yohane Paulo II na kuridhiwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI.

Kamati kuu ya Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Amerika ya Kusini na Caraibi, limepata nafasi ya kukutana na kuzungumza na viongozi wakuu mjini Vatican pamoja na kutembelea baadhi ya Mabaraza ya Kipapa kuhusu masuala ya: Mafundisho tanzu ya Kanisa, Utamaduni, Familia, Mawasiliano, Uinjilishaji Mpya pamoja na Sinodi za Maaskofu. Viongozi hawa walibahatika kuzungumza pia na Tume ya Kipapa kwa ajili ya Amerika ya Kusini pamoja na Mabalozi kutoka Amerika ya Kusini wanaoziwakilisha nchi zao mjini Vatican ambao wamekabidhiwa hati kuhusu hali ya wakimbizi huko Amerika ya Kusini!

Umefunga na nani pingu za maisha?


Tupo bado kwenye chumba cha karamu ya mwisho tukisikiliza Wosia wa Yesu. Lugha inayotumika leo ni ya kimahaba, yaani, lugha ya upendo wa dhati kama ile ya wanandoa wanaopendana. Lugha hiyo ndiyo anayoitumia Yesu anapoagana na wafuasi wake, na kuwafanya kuhamasika kumsikiliza.

Katika Wosia huo ulio katika sura tano za Injili, neno upendo linatumika mara ishirini na sita. Kwa mara ya kwanza unalikuta kwenye fasuli ya leo: “Mkinipenda, mtazishika amri zangu,” au vizuri zaidi lingetumika neno: “Kama” mkinipenda. Namna hii ya kuongea kwa upande wa Yesu ni ya kinyenyekevu, ya kuaminia, ya saburi na ya kujali, yaani inajali sana uhuru na hiari ya yule anayeambiwa; kama vile angesema: “Yote yanakutegemea wewe”.

Hiyo ni lugha huru ya Yesu aliye huru. Yesu anatumia lugha ya maelewano na ya makubaliano. Kama sote tujuavyo kwamba mambo mengine yanaweza kutendeka kirahisi, kwa ari na kwa moyo wote endapo yanafanyika kwa hiari, wasemavyo waswahili: “Ukipenda utakula nyama mbichi”.

Injili ya leo ina aya saba na kwa mara saba katika kila aya Yesu

Papa akamilisha Hija yake Mashariki ya Kati na wito wa amani

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu jioni alikamilisha hija yake Mashariki ya Kati na wito wa amani. Hija hii ya siku ya tatu 24-26 Mei 2014 kutembelea maneneo Matakatifu katika Nchi Takatifu aliikamilisha, akiwa mjini Jerusalem ambako hatua ya mwisho aliongoza Ibada ya Misa akiwa na Maaskofu wa Nchi Takatifu, katika jengo lenye Chumba cha Juu ambako Kristo, alifanya karamu ya mwisho, kinachojulikana kama “cenacolo”.

Baada ya Ibada, alielekea uwanja wa ndege wa Monte Scopes , ambako alipanda helkoputa hadi uwanja wa Ndege wa Ben Gourion wa mjini Tel Aviv, ambako aliagana na wenyeji wake, viongozi wa kanisa na serikali wakiongozwa na Rais wa Israel, Shimon Peres. Mahali hapo Papa pia kulifanyika gwaride la heshima la wanajeshi. Na kabla ya kupanda ndege alitoa salaam zake za mwisho kwa wote.

Wachambuzi wa ziara hii wanasema ,

Braeking news:20 wafariki katika ajali ya treni


Treni
Maafisa wa huduma za treni nchini India wanasema kuwa takriban watu 20 wanahofiwa kufariki katika ajali ya gari moshi katika jimbo la Uttar Pradesh.
Treni hiyo ya kubeba abiria iligongana na treni ya jizigo iliyokuwa imeemgeshwa katika kituo cha treni cha Chureb.
Mabehewa sita ya treni hiyo ya Gorakhdham Express yaling'oka kutoka kwenye treni hiyo.
Waokozi wanajaribu kuwaokoa abiria waliokuwa ndani ya treni hiyo na ambao bado wamekwama.
Treni hiyo ilikuwa inasafiri kutoka mjini Gorakhpur hadi katika jimbo la Hisar Haryana

Bikira Maria linda familia, vijana na wazee!



Baba Mtakatifu Francisko Jumapili tarehe 25 Mei 2014 baada ya maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu kwenye Uwanja wa Pango la Mtoto Yesu mjini Bethlehemu, amesali pamoja na waamini Sala ya Malkia wa Mbingu, mahali hapa ambapo Bikira Maria alimzaa Mtoto Yesu, akapata nafasi ya kuutafakari uso wa Yesu kuliko mtu mwingine yoyote duniani. Akasaidiwa na Mtakatifu Yosefu kumlaza Mtoto Yesu katika Pango la kulishia wanyama!

Baba Mtakatifu amewaweka wananchi na wakazi wote wa eneo hili chini ya ulinzi na tunza ya Bikira Maria, ili waweze kuishi katika haki, amani na udugu. Amewaweka pia mahujaji wote wanaotoka sehemu mbali mbali duniani kuja mjini Bethlehemu ili kujichotea neema kutoka kwenye kisima cha imani ya Kikristo, chini ya ulinzi wa Bikira Maria.

Baba Mtakatifu anamwomba Bikira Maria kulinda familia, vijana na wazee; kuwasaidia wale ambao wamepoteza imani na matumaini; awafariji wagonjwa, wafungwa na wote wanaoteseka; awaimarishe viongozi wa dini na Jumuiya nzima ya waamini, ili kweli waweze kuwa ni chumvi na mwanga wa katika Nchi hii. Baba Mtakatifu anamwomba Bikira Maria alinde huduma za elimu zinazotolewa katika eneo hili, lakini zaidi kutoka Chuo Kikuu cha Bethlehemu.

Baba Mtakatifu anapotafakari kuhusu Familia Takatifu, mawazo yake yanakwenda moja kwa moja mjini Nazaret ambako anatamani kwenda kutembelea Mwenyezi Mungu akipenda wakati mwingine tena. Ameonesha upendo na mshikamano wake kwa waamini wote wanaoishi katika eneo hili. Anamwomba Bikira Maria asaidie mchakato wa ujenzi wa udugu, mshikamano na amani
!

Roho Mtakatifu ni kocha wa maisha ya kiroho!


Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican inapenda kukushirikisha utajiri wa tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya Vi ya Kipindi cha Pasaka inayomwonesha Roho Mtakatifu kuwa kweli ni kocha na mwalimu wa maisha ya kiroho! Kazi kwako!

Katika Injili NENO KUPENDA/PENDO linatawala – hivi unajisikiaje unapoambiwa nakupenda au unapohisi kuwa unapendwa? Hakika kupenda kunawajibisha - tamko hilo lasubiri jibu. Wengi wetu twafahamu fika jinsi ilivyo vigumu kupenda upeo/kweli. Upendo unadai matendo. Kinachofuata ni wajibu.


Ndicho kinachoonekana katika masomo yetu ya leo = kutii amri na kuabudu. Ndiyo maana Yesu anaweza kusema mkinipenda mtazishika amri zangu. Mtakatifu Tomas wa Akwino - sheria za Mungu ni nyepesi kwa wapendao na mzigo kwa wasiopenda.

1 Jan 4,8 yeye asiyependa hakumjua Mungu kwa maana Mungu ni upendo -hivyo ili kupenda vizuri ni lazima kumjua Mungu sababu yeye ni PENDO. Mapendo ya kweli yadai sadaka. Ili kushika amri au sheria inavyotakiwa yahitaji sadaka kubwa na inayodai utumishi.

Mt Agustino anapotafakari juu ya upendo wa Mungu anasema - umegusa mioyo yetu kwa pinde za upendo wako na akili zetu kwa mishale ya neno lako.

Baada ya utangulizi na kusikia masomo

Papa Francisko aanza hija yake ya kichungaji Nchi Takatifu

Baba Mtakatifu Francisko ameondoka mjini Roma asubuhi, tarehe 24 Mei 2014 tayari kwa hija ya kitume huko Yordani, Palestina na Israeli kama kilele cha maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana, akazungumza na kusali pamoja na Patriaki Anathegoras wa Yerusalemu, huu ukawa ni mwanzo mpya wa mchakato wa majadiliano ya kiekumene.

Baba Mtakatifu katika Uwanja wa ndege wa Fiumicino, Roma amesindikizwa na viongozi mbali mbali wa Kanisa na Serikali ya Italia. Ametumia nafasi hii kuwasalimia mmoja mmoja na kuwatakia kheri na baraka. Kama desturi, Baba Mtakatifu alibeba mkoba wake mweusi tayari kuanza safari ya kitume Nchi Takatifu.

Baba Mtakatifu amewaandikia wakuu wa Nchi ya Italia, Ugiriki, Cyprus na Israeli ujumbe wa matashi mema wakati alipokuwa anasafiri kuelekea mjini Amman, kituo cha kwanza cha hija yake ya kitume! Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe aliomwandikia Rais Giorgio Napolitano wa Italia, anamwambia kwamba, anaelekea Nchi Takatifu ili kuadhimisha Jubilee ya Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana na Patriaki Anathegoras wa Yerusalem pamoja na kusali kwa ajili ya kuombea haki, amani pamoja na kukoleza majadiliano ya kiekumene na kidini. Anawatakia kheri na baraka wananchi wa Italia, anawaomba pia kumkumbuka katika sala zao.

Naye Rais Giorgio Napolitano wa Italia amemshukuru Baba Mtakatifu Francisko na kwamba, Jumuiya ya Kimataifa ina matumaini makubwa katika hija hii ya kitume huko Nchi Takatifu, mahali ambapo kuna kinzani kubwa katika historia yake na ulimwengu kwa ujumla. Ni matumaini ya Rais Napolitano kwamba, hija hii itakuwa ni cheche za matumaini kwa wale wanaotaka kusimama kidete kuendeleza amani na utulivu. Rais Napolitano anamtakia mafanikio mema katika hija hii ya kitume.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa Rais Karolos Paoulias wa Ugiriki anamtakia mafanikio mema katika kukuza na kudumisha misingi ya haki na amani, anawaombea baraka tele kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Baba Mtakatifu Francisko akimwandikia Rais Nicos Anastasides wa Ugriki anasema, anawatakia kheri na baraka tele wananchi wa Ugiriki na kwamba, anawaombea furaha na amani kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Mwishoni, Baba Mtakatifu Francisko amemwandikia pia ujumbe Rais Shimon Peres wa Israel kwa kumtakia matashi mema na wananchi wote wa Israeli na kwamba, ana matumaini ya kukutana naye Nchi Takatifu wakati wa hija yake ya kichungaji. Anawatakia wote baraka tele!




Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya 6 ya Kipindi cha Pasaka


Karibuni ndugu msikilizaji wa Radio Vatican katika kipindi cha Liturujia ya Neno la Mungu, tukiwa tayari Dominika VI ya Kipindi cha Pasaka, ambamo tunasikia na kuona Bwana mfufuka akihaidi zawadi ya Roho Mtakatifu. RealAudioMP3

Mpendwa mwana wa Mungu, katika somo la kwanza (Mdo, 8: 5-8, 14-17) tunakutana na Filipo ambaye yuko mji wa Samaria akihubiri habari njema huko. Katika mahubiri yake hayo au tuseme kazi zake za kichungaji atatenda ishara nyingi na mojawapo ya ishara hizi ni watu kunasuliwa toka pepo wachafu, waliopooza kuponywa na ishara nyingine kama hizo zilengazo kuleta uhuru katika maisha ya watu.

Kwa hakika watu walifurahi kama mwandishi anavyosema “ikawa furaha kuu katika mji ule”. Mitume waliposikia kuwa Samaria wamepokea Neno la Mungu waliwatuma Petro na Yohane ili wawawekee mikono kwa ajili ya kushukiwa na Roho Mtakatifu, maana walikuwa wamebatizwa tu kwa jin

Papa Francisko ajikabidhi chini ya ulinzi wa Bikira Maria!

Baba Mtakatifu Francisko Ijumaa, tarehe 23 Mei 2014 asubuhi na mapema, aliondoka kutoka mjini Vatican na kwenda kusali kwenye Kanisa kuu la Bikira Maria mkuu lililoko mjini Vatican, kuomba ulinzi na tunza ya Bikira Maria kabla ya kuanza hija yake ya kichungaji Nchi Takatifu itakayomwezesha kutembelea: Yordan, Palestina na Israeli kama sehemu ya maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana, akazungumza na kusali na Patriaki Anathegoras wa Yerusalemu.

Baba Mtakatifu Francisko alipokuwa anatangaza hija hii ya kitume aliwaambia waamini waliokuwa kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican kwamba, hija hii itafikia kilele chake wakati viongozi wawakilishi wa Makanisa watakaposali kwa pamoja kwenye Kaburi Takatifu, mwendelezo wa mchakato wa majadiliano ya kiekumene, ili wote wawe wamoja!


Kumekucha!

Ili wote wawe wamoja ndiyo kauli mbiu inayoongoza Hija ya kitume ya baba Mtakatifu Francisko katika Nchi Takatifu kuanzia tarehe 24 hadi tarehe 26 Mei 2014, kama sehemu ya Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana na kusali pamoja na Patriaki Anathegoras wa Yerusalemu, tarehe 5 Januari 1964. RealAudioMP3

Baba Mtakatifu anatarajiwa kuondoka mjini Roma, Jumamosi, tarehe 24 Mei 2014 majira ya Saa 2:15 asubuhi na kuwasili Amman, Yordani saa 7:00 mchana na baadaye yatafuatia mapokezi ya heshima yatakayofanyika kwenye Jumba la Mfalme Al – Husseini majira ya Saa 7: 45. Baba Mtakatifu anatarajiwa kukutana na kuzungumza na viongozi wa Serikali ya Yordani majira ya saa 8:20 na baadaye Saa 10: 00 anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye uwanja wa Kimataifa wa Amman. Jioni Baba Mtakatifu atatembelea kwenye eneo la Ubatizo wa Yesu, Ng’ambo ya Mto Yordan. Baadaye atakutana na kuzungumza na wakimbizi, wahamiaji na vijana walemavu.

Jumapili tarehe 25 Mei 2014, Baba Mtakatifu

Jengeni utamaduni wa watu kukutana na kudumisha amani!

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 19 Mei 2014 amekutana na kuzungumza na Baraza la Maaskofu Katoliki Mexico kwa kuwataka kujenga na kudumisha utamaduni wa watu kukutana pamoja na kujenga amani. Ili Kanisa liweze kuendelea kuwajengea watu imani na matumaini, halina budi kushikamana na wahanga wa biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na maskini!

Baba Mtakatifu anasema, hakuna sababu ya Kanisa kuogopa au kutishwa na nguvu za giza, bali linapaswa kusimama kidete na kwa ujasiri pamoja na watu wanaoendelea kuteseka, kwa kutetea haki zao msingi pamoja na kushiriki katika mchakato wa kuwaletea maendeleo endelevu yanayomlenga mtu mzima: kiroho na kimwili. Mambo haya yanajikita katika mchakato wa Uinjilishaji pamoja na kutafuta mafao ya wengi.

Barua ya Papa Francisko kwa ajili ya Familia

Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Sinodi Maalum ya Maaskofu kwa ajili ya Familia itakayoadhimishwa Mwezi Oktoba 2014 hapa mjini Vatican, kwa kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kuhusu familia mintarafu Uinjilishaji" ameandika barua kwa familia zote duniani ili kukazia dhamana ya Kanisa kuendelea kutangaza Injili kwa kukabiliana kinaga ubaga na changamoto mpya zinazohusu familia.

Baba Mtakatifu anasema, maandalizi haya yanawahusu Watu wote wa Mungu kwa kuhakikisha kwamba, wanashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo pamoja na kusindikiza mchakato mzima kwa njia ya sala, jambo muhimu sana kutoka kwa familia zote. Sinodi hii ni maalum kwa ajili ya: wito na utume wa Kanisa na Jamii; matatizo yanayowakabili wanandoa; maisha ya kifamilia, elimu na malezi kwa watoto; dhamana na utume wa familia katika maisha ya Kanisa.

Baba Mtakatifu anazialika familia kusali na kumwomba Roho Mtakatifu ili aweze kuwaangazia Mababa wa Sinodi katika kutekeleza wajibu wao huu nyeti. Sinodi hii maalum, itafuatiwa tena na Sinodi ya kawaida ya Maaskofu itakayojadili kuhusu tema ya familia mwaka 2015 sanjari na Maadhimisho ya Siku ya Familia Kimataifa itakayofanyika mwezi septemba, mjini Philadelphia, nchini Marekani.

Baba Mtakatifu anawaalika wanafamilia pamoja na watu wote wenye mapenzi mema kusali kwa ajili ya kufanikisha matukio haya makuu ndani ya Kanisa, ili liweze kung'amua na kupata mikakati itakayosaidia familia ili kukabiliana na changamoto kadiri ya mwanga na nguvu ya Kiinjili.

Baba Mtakatifu Francisko anasema, ameitunga barua hii wakati Mama Kanisa alipokuwa anaadhimisha Siku kuu ya kutolewa Bwana Hekaluni. Ni tukio ambalo liliwakutanisha Mzee Simeoni na Anna kwa nguvu ya Roho Mtakatifu wakamtambua Yesu kuwa ni Masiha. Mzee Simeoni akamshukuru Mungu kwa kuwa ameuona wokovu na Anna kwa upande wake akasimulia matendo makuu ya Mungu licha ya uzee wake.

Inafurahisha kuona kwamba, wazee wawili na vijana wawili wanakutanishwa na Yesu. Hii inaonesha kwamba, Yesu ana uwezo wa kukutanisha na kuunganisha vizazi, kwani Yeye ni chemchemi ya upendo inayovuka ubinafsi, upweke na masikitiko. Baba Mtakatifu anasema, familia katika hija ya maisha yao wanashirikishana na kumegeana mambo mengi mema: chakula na mapumziko; kazi za nyumbani, starehe, sala, safari na hija ya maisha ya kiroho pamoja na matendo ya huruma.

Pale panapokosekana upendo, hapo kutakosekana furaha na kwamba, upendo wa kweli unabubujika kutoka kwa Kristo kwa njia ya Neno lake ambalo ni mwanga katika mapito ya waamini; anawapatia Mkate wa maisha ya uzima wa milele, unaowasaidia waamini kupambana na changamoto za maisha ya kila siku.

Baba Mtakatifu anahitimisha barua yake kwa familia kwa kuhimiza kwamba, mchango wao wa sala ni muhimu sana katika Maadhimisho ya Sinodi ya Maaskofu kuhusu Familia. Anawaomba pia kumwombea ili aweze kuwahudumia Watu wa Mungu katika ukweli na upendo. Baba Mtakatifu anawaombea ulinzi na tunza kutoka kwa Bikira Maria na Mtakatifu Yosefu, ili waweze kutembea huku wakiwa wameshikamana katika upendo na huduma.


Papa Francisko: Jengeni umoja na mshikamano; saidieni familia na maskini!

Kwa mara ya kwanza katika historia ya Baraza la Maaskofu Katoliki Italia, Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu, tarehe 19 Mei 2014 amefungua mkutano wa sitini na sita kwa kuwataka kutambua kwamba, wao ni wachungaji wa Jumuiya ya Kristo Mfufuka. Wao ni wachungaji wa Fumbo la Mwili wa Kristo yaani Kanisa, wachungaji wanaoendeleza ujio wa Ufalme wa Mungu kati ya watu kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa familia, maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.

Baba Mtakatifu Francisko katika hotuba yake ya ufunguzi amewataka Maaskofu Katoliki Italia kushikamana na Kristo pamoja na Kanisa lake, ili aweze kuwaimarisha katika imani, matumaini na mapendo, kwa kuendelea pia kuwa ni waaminifu katika utekelezaji wa mapenzi ya Mungu katika maisha na utume wao.

Kanisa ni Jumuiya ya Kristo Mfufuka inayojikita katika imani ambayo inarutubishwa kwa Neno na Sakramenti za Kanisa, changamoto na mwaliko wa kuepukana na vishawishi vinavyoweza kuwasonga na hivyo kushindwa kutekeleza wajibu wao kikamilifu: kwa kutokuwa na mikakati makini ya kichungaji, kwa kujiamini sana na kutoona umuhimu wa kumtegemea Kristo katika maisha na utume ndani ya Kanisa. Baba Mtakatifu anawaalika Maaskofu kumtegemea Kristo na kumkaribisha ili aweze kutenda pamoja nao, ili waweze kuwa kwelini watakatifu na mifano bora ya kuigwa.

Maaskofu ni wachungaji wa Kanisa ambalo ni Fumbo la Mwili wa Kristo, linalowashirikisha kwa namna ya pekee Fumbo la Pasaka na huduma inayowawajibisha kujenga na kudumisha umoja, upendo, mshikamano na ukarimu, bila kumezwa na malimwengu wala kuwadharau wengine. Huu ndio mfano bora uliooneshwa na Watakatifu Yohane XXIII na Yohane Paulo II.

Mama Kanisa anapojiandaa kumtangaza Mtumishi wa Mungu Papa Paulo VI hapo tarehe 29 Oktoba 2014 kuwa Mwenyeheri, Maaskofu wanakumbushwa maneno yake aliyowataka Maaskofu Katoliki Italia kujisadaka kwa ajili ya ujenzi wa umoja wa kitaifa, kwa kuondokana na udhaifu unaoweza kujitokeza kwa kutokuwa na mawasiliano makini, kwani kinzani na utengano ndani ya Kanisa ni kashfa kubwa na hakuna mtu anayeweza kuhalalisha kitendo hiki.

Baba Mtakatifu anawakumbusha kwamba, umoja na mshikamano wao unapata chimbuko lake katika maadhimisho ya Fumbo la Ekaristi Takatifu; kwa kujenda na kudumisha amani na utulivu hata katika nyakati ngumu. Tasahufi ya Ekaristi takatifu inajenga mshikamano, majadiliano, udugu, uhuru na uwezo wa mtu kuchangia kadiri ya Roho Mtakatifu anavyowakirimia. Baraza la Maaskofu linapaswa kuwa ni kwa ajili ya huduma ya umoja, mahusiano ya dhati, mahali pa kubadilishana na kushirikishana mang'amuzi na changamoto katika shughuli za kichungaji.

Baba Mtakatifu anawataka Maaskofu kuwa karibu na Mapadre wao katika maisha na utume wao; kwa kuwapatia majiundo makini ya awali na endelevu katika maisha ya kiutu, kitamaduni, kiroho na kimahusiano. Mkutano mkuu wa Baraza la Maaskofu utakaofanyika mwezi Novemba, 2014 utajikita katika maisha ya Mapadre, changamoto ya kufanya maandalizi makini.

Maaskofu wawasaidie watawa kutekeleza utume wao ndani ya Kanisa na kuishi kadiri ya kweli za Kiinjili, ili waweze kuwa ni mashahidi wa Injili ya Furaha. Maaskofu wajenge utamaduni wa kusikiliza watu wao, wawaimarishe katika imani, wawasaidie waamini walei katika maisha na utume wao wa kuyatakatifuza malimwengu. Wawapatie mikakati itakayowawezesha waamini walei kutangaza Neno la Mungu kwa njia ya ushuhuda wa maisha yao na Katekesi. Utume wa Kanisa unajikita katika umoja na upatanisho kama kielelezo cha unabii katika ujenzi wa Ufalme wa Mungu.

Baba Mtakatifu Francisko anasema, matendo ya huruma ni muhimu sana katika ujenzi wa Ufalme wa Mungu kati ya watu. Kanisa liguswe na matatizo yanayowakabili watu katika hija ya maisha yao hapa duniani, lisaidie kupambana na ukosefu wa haki msingi za binadamu. Kanisa linatumwa kutangaza ukweli kuhusu Kristo na huruma kwa waja wake, kwa kutambua kwamba, upendo katika ukweli ni kikolezo cha maendeleo endelevu katika familia ya binadamu, tunu zinazopaswa kumwilishwa katika matendo!

Maaskofu wawe ni wachungaji wasiomezwa na malimwengu, watu wanaopenda na kuishi ufukara, kwa kuonesha huruma na unyenyekevu katika maisha. Wawe ni watu huru wanaweza kuwakaribia watu kwa upendo na kuwasindikiza wale wanaotembea katika upweke na giza la uvuli wa maisha, ili hatimaye watu hawa waweze kuonja tena utu, matumaini pamoja na kuwa na maisha mapya.

Hapa Familia zinapaswa kupewa kipaumbele cha pekee katika maisha na utume wa Kanisa, kwa kusimama kidete kulinda, kutetea na kudumisha tunu bora za maisha ya kifamilia. Familia ni kiini cha Jamii na ushuhuda wa uzuri wa maisha. Hapa ni mahali ambapo watu wanapaswa kufundishwa namna ya kukumbatia Injili ya Uhai, kwa kuwasaidia wazazi katika mchakato wa malezi ya watoto wao, kwa kuwaganga wale waliopoteza dira na mwelekeo wa maisha.

Baba Mtakatifu Francisko anawaambia Maaskofu wa Italia kwamba, waoneshe mshikamano wa upendo na watu wasiokuwa na fursa za ajira au wale ambao wamepoteza ajira kutokana na sababu mbali mbali, watu ambao kwa sasa maisha na utu wao uko mashakani. Wawafungulie milango wakimbizi na wahamiaji wanaotafuta faraja na kutaka kusalimisha maisha yao kutoka kwenye vita, nyanyaso na dhuluma, kwani upendo ni kielelezo kikuu cha ushuhuda wa ukarimu, kwani hii Injili itaenea sehemu mbali mbali kwa kuonesha mvuto na mashiko!

Baba Mtakatifu anasema kuna haja ya kuwa na sera mbadala katika mikakati ya maendeleo ya kiuchumi kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa binadamu na mahitaji yake msingi, kwa kulinda na kuboresha mazingira sanjari na kuwajengea watu matumaini wakati huu wanapopambana na athari za myumbo wa uchumi kimataifa; mmong'onyoko wa kimaadili na utu wema pamoja na watu kupoteza mwelekeo katika maisha ya kiroho. Hapa kuna haja ya kuwa na mikakati makini kwa kuona ukweli wa mambo, ili kujenga na kudumisha, udugu na mshikamano.

Mwishoni, Baba Mtakatifu Francisko amewaomba Maaskofu wa Italia kumsindikiza katika hija yake ya kitume huko Nchi Takatifu, kama sehemu ya maadhimisho ya jubilee ya Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana, akazungumza pamoja na kusali na Patriaki Anathegoras wa Yerusalemu. Anakwenda huko ili kuwaonjesha mshikamano wa Kanisa kwa ajili ya watu wanaoishi katika eneo ambalo limebarikiwa na Yesu kwa kufa na kufufuka kwake!


Apewa adhabu ya kifo kwa kuolewa na Mkristo!



Mahakama moja nchini Sudan imemkuta na hatia Meriam Yahya Ibrahim Ishaq, mwanamke mwenye umri wa miaka 27 ya kukufuru na kuzini kwa kuwa ameolewa na raia mmoja Mkristo kutoka Sudan ya Kusini na hivyo kuhukumiwa kuchapwa viboko mia moja na kunyongwa hadi kufa!

Adhabu hii imewashtua watetezi wa haki msingi za binadamu, kwa kuitaka Serikali ya Sudan kuheshimu uhuru wa kuabudu kadiri ya Katiba ya nchi iliyotungwa kunako Mwaka 2005.

Mahakama hiyo imetumia "Sharia" za dini ya Kiislam zilizoingizwa nchini humo kunako mwaka 1983 zinazopiga rufuku kwa mwamini wa dini ya Kiislam kuoa au kuolewa na Mkristo. Viongozi mbali mbali wa Jumuiya ya Kimataifa wameitaka Serikali ya Sudan kuingilia kati ili kusitisha utekelezaji wa adhabu hii ambayo ni kinyume cha haki msingi za binadamu.


Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili V ya Pasaka



Ninaendelea tena kuwa nawe katika kipindi cha Liturujia ya Neno la Mungu, tukiwa tayari Dominika ya V ya Pasaka. Ujumbe wa Neno la Mungu umezama katika kuamini kina katika Bwana na kisha kutoa huduma katika jumuiya kama njia ya kukamilisha unachoamini na hivi baadaye kukuwezesha kufika mbinguni. Bwana anaenda huko kutayarisha makao ya kutosha kwa ajili yetu. RealAudioMP3

Katika somo la kwanza: (Mdo, 6:1-7), tunakutana na ongezeko la wanafunzi katika jumuiya ya kwanza, na katika ongezeko hili, kunatokea malalamiko ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu ya huduma pungufu kwa wajane. Basi Mitume wakishauriana na kusali wanaona kuwa haipendezi wao kuacha huduma ya Neno la Mungu na kuhudumu mezani.

Uamuzi unaotolewa ni kuwaambia wanajumuiya ya wa jumuiya ya kwanza wakisema chagueni kati yenu watu 7 wenye karama ya wema, wenye kujawa na roho na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili na sisi tutadumu katika kuomba na kuhudumia lile Neno”. Baada ya ushauri huo wakachaguliwa watu 7 kati yao alikuwako Stefano aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, wakasali na wakawawekea mikono na tayari wakawa mashemasi katika Kanisa.

Mpendwa msikilizaji kwa nini kunatokea malumbano na mikingamo katika Jumuiya ya kwanza? Kwa nini mwandishi anaweka jambo hili mbele yetu? Jambo la kukumbuka katika simulizi hili ni kwamba hapo mwanzo Jumuiya ilikuwa na Waebrania tu na polepole kadiri ya kazi ya kimisionari ilivyokuwa ikisonga mbele, wakajiunga hata Wayahudi wa Kiyunani ambao walikuwa wakitumia lugha ya Kigriki. Wayahudi wa Kiyunani walikuwa na mchanganyiko wa tamaduni kwa maana walikuwa wakiishi nje ya Palestina.

Waebrania ambao hawakuwa na mchanganyiko, wao waliendelea kutumia lugha ya Kiebrania kama kawaida! Basi jumuiya ilivyozidi kuongezeka vilianza kujitokeza vijidharau vya hapa na pale dhidi ya Wayahudi wa Kiyunani na hasa wajane na yatima wao kuhusiana na ugawanyaji wa mali za jumuiya! Kumbuka kuwa, tangu mwanzo walikuwa wameweka mali pamoja. Mambo haya yalianza kujitokeza baada ya miaka 3 hivi. Kilele cha dharau ni malumbano na madai ya kutaka Mitume washiriki katika kuhudumu mezani, ili kuweka haki katika maisha ya jumuiya kila siku.

Basi, shauri hilo likiwafikia Mitume, na Mitume wataamua kwa hekima ya kimungu kuwaweka wakfu watu saba kwa ajili ya huduma hiyo. Mpendwa msikilizaji hiki ndicho chanzo cha ushemasi katika Kanisa Moja,Takatifu, Katoliki na la Mitume.

Mpendwa mwana wa Mungu, tunajifunza nini katika hili? Jambo la kwanza tunajifunza kuwa tangu mwanzo Kanisa limekuwa likikumbwa na matatizo na hivi kuonesha sura mbili za Kanisa: Kanisa la wema na wadhambi. Kumbe hata hivi leo inapotokea purukushani fulani katika Kanisa tusishangae, ni hali ya mwanadamu tangu mwanzo. Wajibu na jambo la kufanya ni kusali na kuomba kwa ajili ya kupatikana suluhu kwa njia ya amani.

Jambo la pili Mitume wametupa mfano bora yaani wakati Kanisa linakua nao wanaona ni vema kushirikisha madaraka waliyokabidhiwa na Mungu kwa wengine, kwa ajili ya faida ya Taifa la Mungu. Wanapoamua jambo hili wanashirikisha jumuiya yote; huu ndio umoja wa Kanisa, ndicho Bwana anachotaka katika kuwa mchungaji mwema. Mitume wanabaki na lengo moja yaani utume wa Neno la Mungu.

Katika somo la Pili: (1Mt Petro 2:4-9) Mt Petro awaalika watu wote kumwendea Yesu Kristu jiwe hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule. Jiwe hili ndo lile jiwe kuu la pembeni ambalo Mungu ndiye mjenzi wake. Mungu anapojenga nyumba yake akisha kuweka jiwe kuu anasonga mbele akitumia mawe mengine, yaani wanadamu ambao Mt Petro anasema “Katika yeye nasi tunaitwa kuwa nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu tena tunaalikwa kutolea daima dhabihu njema zinazokubaliwa na Mungu. Ndiyo kusema Mungu, anajenga nyumba yake kwa kutumia mawe yaliyohai, yaliyojaa upendo! Hawa ni wabatizwa wanaomkubali Kristu na hivi kujenga nyumba ya kiroho yaani Kanisa la Mungu.

Mpendwa msikilizaji yafaa kujiuliza ujenzi huu ulianza lini? Kwa hakika ujenzi umeanza wakati wa ufufuko wa Bwana, maana waashi walilikataa jiwe hai na Mungu akalifanya kwa njia ya ufufuko kuwa jiwe kuu la pembeni. Jambo hili lilishaaguliwa na manabii wa kale “tazama naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule lenye heshima”. Ni kwa jinsi hiyo basi uaguzi huu umekamilika katika ufufuko wa Bwana. Mpendwa msikilizaji kwa kuwa mawe hai ya nyumba ya Mungu, Bwana anatuita daima kuachana na giza na tunaalikwa kuzitangaza fadhili zake daima kwa mataifa ili waweze kuingia katika nuru yake ya ajabu.

Katika Injili: (Yn 14:1-12) Mwinjili anaweka mbele yetu mafundisho ya Bwana aliyoyatoa katika chakula cha jioni siku iliyotangulia kuteswa kwake. Ndiyo kusema anawaachia wosia Mitume na vizazi vyote. Mmoja anaweza kuuliza hivi kwa nini Mama Kanisa ameweka somo hili baada ya Pasaka? Ni kwa sababu moja ya kawaida kwamba wosia husomwa baada ya mwenye kuandika wosia anapokuwa ameondoka duniani!

Katika mafundisho ya Bwana tunaona jinsi Bwana mwenyewe akiwatayarisha wanafunzi wake kwa ajili ya Kupaa kwake. Anasema wasifadhaike bali wawe na imani katika Mungu na yeye mwenyewe, na kisha wakumbuke anaenda kuwatayarishia makao tele ili atakapokuwepo nao wawepo. Jambo la kwenda kutayarisha makao linashangaza kidogo kwa sababu kuna mawazo kwamba tayari pamekwishaandaliwa! Ni kweli, lakini ataka kutuambia suala la kusafiri na ugumu wake linahitaji maandalizi. Kwa sababu hiyo basi, Bwana ataongeza neno akisema huko niendako mwaijua njia!

Mpendwa mwanatafakari, kwa kuwa njia na makao tunayopaswa kuyafikia ni kazi nyeti, mara moja Tomaso atasema hatujui njia! Bwana mkarimu na Mchungaji mwema anamjibu “mimi ndimi njia na ukweli na uzima; mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya mimi”. Hili maana yake nini? Jambo hili lamaanisha lazima kufuata njia ya mapendo, njia ya mateso hadi msalabani na kisha hapo kutakuwa na ufufuko.

Kumbe, matayarisho ya makao yanaanza na msalaba wake na kisha ufufuko furaha ya milele na Baba mbinguni. Ili tuweze kupita katika njia ya Bwana tunahitaji msaada wake na ndiyo maana alisema, nitaenda na kisha nitarudi kuwachukua pamoja nami! Katika kutangaza makao, Bwana ansema nyumbani mwa Baba yake, kuna makao mengi. Bwana ataka kusema nini katika hili? Ataka kusema tukikubali kumfuasa yeye basi kuna wajibu na shughuli za kutosha kama tuonavyo leo katika Kanisa. Nyajibu hizi tunaalikwa kuzifanya kwa mapendo tukishirikiana katika raha na taabu mpaka kufikia mwisho wa nyakati na hapa ndipo kuna kumwona Baba.

Wakati Bwana anatangaza kuwa yeye ni njia ya kwenda kwa Baba, mara moja Filipo anauliza utuoneshe Baba yatutosha! Ombi hili linamwendea Bwana na hata sisi wakristu wa leo. Kwa upande wake Bwana anajibu akisema aliyeniona mimi amemwona Baba, kwa kuwa mimi ni ndani ya Baba na Baba yu ndani yangu. Kwa upande wetu tunapaswa kusema daima aliyemwona Kristu amemwona Baba. Baada ya fundisho hilo lililo gumu kwao, Bwana atawaalika kusadiki hilo na kama hawasadiki basi wasadikini kwa sababu ya kazi zenyewe!

Mpendwa, kwa kumtambua na kumjua Baba haina haja ya kujenga falsafa ya pekee bali ni kuitikia kile ambacho Bwana anasema. Ndiyo kusema inatosha tu kumtazama Kristu yaani Mwana, ambaye ni sura kamilifu ya Mungu. Inatosha kumtazama Mwana, yamaanisha na yatulazimu kusoma Neno la Mungu na kutafakari, kusikia kile anachofundisha kwa njia ya Kanisa, kupambanua namna yake ya kupenda yaani mpende adui yako, namna yake ya kukosoa kunapokuwa na shida au dhambi na mwishoni kuyashika yale yote mema aliyoliachia Kanisa la Kitume.

Mpendwa msikilizaji, katika kusadiki yaani, kuamini kuliko kina Bwana anafungamanisha zawadi, yaani anasema kama mmoja akisadiki ataweza kufanya mambo makubwa katika maisha yake. Hili ni kweli nami nasadiki.

Nakutakieni furaha tele katika Dominika hii ya Pasaka na Mungu azidi kuwa nawe, ukitekeleza mapenzi yake katika maisha yako. Tukutane tena Dominika ijayo. Tumsifu Yesu Kristu. Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya C.PP.S.

Ekaristi Takatifu!

Ndugu msikilizaji wa Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican, tulianza maandalizi ya hija ya kichungaji ya Baba Mtakatifu Francisko katika Nchi Takatifu kwa kukufanualia maeneo muhimu katika historia na maisha ya Yesu. Tumekwishatembelea Bethlehemu mahali alipozaliwa Yesu, tukavuka ng'ambo ya pili ya Mto Yordan, mahali alipobatizwa na leo tuko chumba cha juu, mahali alipoweka Ekaristi Takatifu na kuwataka wanafunzi wake wawe ni watu wa huduma! RealAudioMP3
Karibu Wainjili wote wanatupatia maelezo ya karamu ya mwisho. Katika chumba kilicho juu. Wainjili wanasema kwamba karamu hiyo ilikuwa ya Agano Jipya na la milele.

Katika mazingira hayohayo ya kula Yesu akawaosha miguu wafuasi wake. Kila mwenjili anajitahidi kutoa fundisho la pekee kadiri anavyoona yeye. Hapa sisi tufuate maelezo ya mwinjili Luka. Sote tunafahamu kilichotokea siku ile ya karamu ya mwisho. Maneno ambayo Luka anayoyatumia na ambayo yabidi kuyafanyia tafakuri ni yake tunayoyasikia katika kila misa: “fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” Ni mwinjili Luka peke yake anayesema maneno hayo.

Lengo la Yesu lilikuwa ni kuwaalika wafuasi wake wote kumkumbuka Yeye, yaani daima kurudia kufanya kitendo hicho. Lakini zaidi pia aliwataka wamege mkate na kula ikiwa kama alama ya msingi katika imani yetu. Tendo la kumega mkate ni ufupisho wa maisha yake yote toka kuzaliwa hadi kufa kwake. “Mimi nimejifanya chakula ili kuyalisha maisha.” Ni kama vile angekuwa Bethlehemu inayotembea (mobile bakery).

Luka anataka kutuambia kuwa mnapokuwa katika karamu hii, au mnapokula chakula hiki, mnafanya uchaguzi kama wangu wa kujitoa na kujitolea. Huo ni mwaliko wa kuwa kama Kristu, wa kuwa mkate na kujigawa kwa wengine. Kwa hiyo haitaeleweka kabisa kumwona mkristu baada ya kuadhimisha ekaristi, anashindwa kusaidia wengine.

Hali halisi nyingine inayoonekana humo chumbani, wakati wa sherehe hiyo kuliibuka mabishano mazito hasahasa tungeweza kuyaita mahojiano makali kati ya mitume. Kisa walikuwa wanabishana juu ya ukuu, juu ya kuwa na heshima na cheo kati yao “ni nani anayehesabiwa kuwa mkuubwa.” Yesu akawaambia: “Wakuu wa mataifa huwatawala, na wenye mamlaka juu yao huitwa Wenye fadhili; lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye kuongoza kama yule atumikaye. Mimi niko kati yenu kama atumikaye.” Haya tena ni maneno yanayoletwa na Luka peke yake wakati huu wa mlo. Ni maneno kwa ajili ya kila mtu hasahasa yule anayejiita mkristu. Hayo ndiyo mambo yanayoharibu jumuia za kiristu siku za leo. Kazi ya mtu aliyeshiba ni kutafuta cheo.

Mahojiano hayo ya mitume hayakuishia kwao tu. Mabishano hayo yameletwa hapa kuonesha kuwa yanaweza kumpata kila mmoja katika maisha yake. Hasa kuhusu kujihoji wewe mwenyewe kuhusu kuchagua mambo. Hali kadhalika Yesu Kristu katika maisha yake hapa duniani alikabiliwa na changamoto hii ya kujihoji nafsini mwake.

Mahojiano hayo ya Yesu tutayaona baada ya karamu ya mwisho akiwa kwenye mlima wa Mizeituni. Tunaambiwa kuwa alipatwa na uchungu sana ambao katika Injili ya Kiswahili wanafasiri kuwa ni dhiki. “Yesu akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; ...akajitenga na mitume wake… huko akasali... kwa vile alikuwa katika dhiki... hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchi.”

Alikuwa katika katika dhidi au tuseme alikuwa na hali mbaya sana. Yaani ni kama hali ile anayokuwa nayo mtu kabla ya kufa. Neno hili uchungu pia limetokea katika injili ya Luka peke yake, kwa kiingereza ni "Agony". Maana halisi ya neno hilo agoni lamaanisha mapambano, mashindano au mahojiano makali. Hasa mashindano kama yale ya wanariadha. Yesu aliingia katika mashindano kama hayo.

Toka mwanzo wa maisha yake, Yesu ilimbidi aingie katika mapambano na mashindano na nguvu za shetani. Mapambano hayo hayakwisha katika vishawishi, yaani pale shetani alipomjia Yesu jangwani mara tu baada ya kubatizwa. La hasha, baada ya vishawishi vile tunasikia kuwa shetani alimwacha Yesu kwa muda. “Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.” (Lk. 4:13). Shetani anakuja tena akijua kwamba hapa sasa ni lala salama!

Hapa kuna mapambano makali ya roho yanayomdai Yesu kuwa mwaminifu na inabidi kuyashinda. Yesu anashinda! Kuonesha kwamba hayo yalikuwa ni mashindano makali, Yesu anatoka jasho, hilo kama vile jasho linalomtoka mwanariadha wakati wa mashindano. Kwa hiyo "agony" siyo uchungu bali ni mapambano, kuvutana, ukinzani, ugomvi ndani ya mtu. Mapigano yaliyoko ndani ya mtu.

Katika mapambano hayo Yesu anajiandaa kwa kujitenga na kusali. “Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba.” Anajiweka katika mahusiano na Mungu ili kuweza kuiona mipango ya Mungu. Anajiweka katika mahusiano na Mungu, ili kujua Mungu anao mpango gani kwa ajili yake. Yesu alisali sana na akawahimiza mitume wake kukesha na kusali. “Alipofika mahali pake aliwaambia: ‘ombeni kwamba msiingie majaribuni. Ondokeni, mkaombe msije mkaingia majaribuni.” Sala inamsaidia Yesu. Kisha wanafika malaika kumliwaza. Hiyo ni alama ya kuwa na mawazo ya ndani ya Mungu. Endapo alifikiria kutoroka maisha, kutoroka mateso sasa anaimarika, na kuhiari kuurekebisha ulimwengu. Kwa hiyo ili kushinda mapambano ya ndani ya mtu, yabidi kusali sana. Kuunganisha mipango yako na mipango ya Mwenyewe Mungu.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican inakutakia hija njema na Baba Mtakatifu Francisko huko Nchi Takatifu kuanzia tarehe 24 hadi tarehe 26 Mei 2014 kwa kuongozwa na kauli mbiu " Wote wawe wamoja".

Imetaraishwa na
Padre Alcuin Nyirenda, OSB.