Week Hot newz

Sheikh Hassan Bashir amwagiwa tindikali!



IMAMU wa Msikiti wa Sawiyatu Qadiria, Hassan Bashir (33) amejeruhiwa vibaya usoni na sehemu ya bega la kushoto baada ya kumwagiwa kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni tindikali.
Akizungumza na akiwa kwenye wodi ya wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru anakopatiwa matibabu, imamu huyo alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya kati ya saa 3:30 na saa 4:00 usiku karibu na Msikiti wa Tindiga, uliopo eneo la Unga Ltd.
Alisema ana maumivu makali sehemu ya uso pamoja na bega la upande wa kushoto.
Sheikh huyo ambaye alikuwa akizungumza kwa shida kutokana na maumivu makali, alisema alikumbwa na mkasa huo muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo na babu yake ambaye pia ni Mwenyekiti wa Msikiti, Ismail Olomi na Mwenyekiti wa Ujenzi, Abdalah Kaduma, juu ya maandalizi ya Maulid yanayotazamiwa kufanyika msikitini hapo.
 “Tulipomaliza kuzungumza mimi nikawa

Maaskofu KKKT Karagwe wacharuka Mchungaji Kanyiginya, kunyimwa dhamana


Mchungaji  Jackson Kanyiginya 

MAASKOFU, wachungaji na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, wamecharuka na kuvamia Kituo cha Polisi cha Karagwe wakipinga Mchungaji wao, Jackson Kanyiginya, kunyimwa dhamana katika mazingira tata na kuswekwa rumande.
Mchungaji huyo ambaye jana alipandishwa kizimbani kwa kosa la kumpiga mfanyabiashara, Joseph Gareba, alinyimwa dhamana baada ya Mwendesha Mashitaka, Meja Juma Litafa, kuzikataa barua za wadhamini hadi azifanyie uhakiki.
Akizungumza na gazeti hili kutoka Karagwe jana, Askofu mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe, Bagonza, alisema mchungaji Jackson  alikuwa kwenye mkutano na viongozi wote wa kanisa hilo kwa ajili ya kufanya mafungo.
Alisema akiwa katika kituo cha mafungo, alipata wito wa polisi wa kumtaka afike mahakamani juzi kwa ajili ya kujibu kesi iliyofunguliwa kwa siri ya

Sunday Gospel Feb 16 2014



In this week's edition of There's More in the Gospel than Meets the Eye, Jill Bevilacqua and Seàn-Patrick Lovett bring us readings and reflections for the Sixth Sunday of the Year.
Listen: RealAudioMP3

Gospel Mt 5:20-22A,27-28,33-34, 37

Jesus said to his disciples:
“I tell you, unless your righteousness surpasses
that of the scribes and Pharisees,
you will not enter the kingdom of heaven.

“You have heard that it was said to your ancestors,
You shall not kill; and whoever kills will be liable to judgment.
But I say to you,
whoever is angry with brother
will be liable to judgment.

“You have heard that it was said, You shall not commit adultery.
But I say to you,
everyone who looks at a woman with lust
has already committed adultery with her in his heart.

“Again you have heard that it was said to your ancestors,
Do not take a false oath,
but make good to the Lord all that you vow.
But I say to you, do not swear at all.
Let your ‘Yes’ mean ‘Yes,’ and your ‘No’ mean ‘No.’
Anything more is from the evil one.”



Text from page http://en.radiovaticana.va/news/2014/02/13/sunday_gospel_feb_16_2014/en1-772758
of the Vatican Radio website

Miaka 83 tangu kuanzishwa kwa Radio Vatican



Radio Vatican, Mama wa Radio zote duniani, tarehe 12 Februari 2014 imeadhimisha kumbu kumbu ya Miaka 83 tangu ilipoanzishwa. Inajivunia kuwa ni kati ya wadau wakuu wa Shirikisho la Watangazaji Barani Ulaya, EBU ambalo tarehe 13 Februari 2014 linaadhimisha Siku ya Radio Duniani. Kwa namna ya pekee, Jumuiya ya Kimataifa kwa mwaka huu, inajielekeza zaidi katika kuangalia mchango wa wanawake katika medani mbali mbali za maisha.

Watangazaji wanawake kutoka Radio Vatican wamekuwa mstari wa mbele kwa kuwa ni sauti ya wanawake wasiokuwa na sauti kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Radio Vatican katika mtandao wake imeandaa programe mbali mbali zinazoonesha mchango wa Radio Vatican katika kuwawezesha wanawake Barani Afrika, Asia na Amerika.

Hizi ni programme zinazoonesha ujasiri wa wanawake katika kukabiliana na changamoto mbali mbali za maisha: katika masuala ya maendeleo endelevu, haki na amani duniani. Ukitaka kufaidi zaidi unaweza kutembelea katika tovuti rasmi ya Radio Vatican kwa anuani ifuatayo: www.radiovaticana.va
Unaweza pia kuwashirikisha jirani zako.

Mwaka Mmoja watimia Baba Mtakatifu Benedikto 16, alipotangaza rasmi kung'atuka

Ilikuwa ni tarehe 11 Februari 2013, Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, alipotangaza rasmi kwamba, kwa hiyari yake mwenyewe na utashi kamili ameamua kung'atuka kutoka madarakani, ili kutoa nafasi kwa Makardinali kuweza kumchagua Khalifa mwingine wa Mtakatifu Petro.

Maneno haya yakaushangaza ulimwengu. Kwa Kanisa hili likawa ni tukio la kinabii, ili kutoa nafasi kwa Mama Kanisa kuendelea kufanya mageuzi ya kina katika maisha na utume wake, Mwenyezi Mungu akipewa kipaumbele cha kwanza; waamini wakijikita kutangaza Habari Njema ya Wokovu katika ulimwengu wa utandawazi na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Akachaguliwa Baba Mtakatifu Francisko ambaye ameamua kuendeleza mageuzi yaliyokuwa yameanzishwa na Papa mstaafu Benedikto wa kumi na sita katika maisha na utume wa Kanisa kwa kukazia uaminifu kwa Kristo na Kanisa lake, bila kumezwa na malimwengu, mambo ambayo yamelisababishia Kanisa kujikuta linaandamwa na kashfa mbali mbali. Maaskofu mahalia wamepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, wanatekeleza utume wao wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza watu wa Mungu kwa ujasiri na moyo mkuu.

Kuna waamini ambao bado wana madonda makubwa katika mioyo yao, jambo la msingi kwa Kanisa ni kujikita katika mchakato wa uponyaji na upatanisho, ili Kanisa liweze kusonga mbele kwa ari kubwa zaidi katika azma yake ya kuwatangazia watu Injili ya Furaha.

Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita, aliona kashfa ya matumizi haramu ya fedha iliyokuwa inalinyemelea Kanisa kwa kutumia migongo ya wajanja wachache ndani ya Kanisa. Vatican ikatunga na kuridhia sheria inayopiga vita utakatishaji wa fedha haramu inayoweza kutumika kugharimia vitendo vya kigaidi. Papa Francisko anaendelea kukazia umuhimu na dhamana ya wanawake katika maisha na utume wa Kanisa.

Kanisa linamshukuru na kumpongeza Papa mstaafu Benedikto wa kumi na sita, kwa ujasiri na uamuzi wake wa busara wa kung'atuka kutoka madarakani, ili aweze kupata nafasi kubwa zaidi ya kusali na kutafakari.



Papa mstaafu Benedikto XVI kwa sasa ana utume wa sala na tafakari; uamuzi wake ni ushuhuda wa kinabii!

Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican, anabainisha kwamba, Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto wa kumi na sita kwa sasa anautumia muda wake mwingi kwa ajili ya kusali na kutafakari na kwamba, uamuzi wake wa kung'atuka kutoka madarakani ni wazo ambalo alilitafakari, akasali na kulipembua kwa kina na mapana yake, hatimaye,

Mradi wa miaka 5 kwa ajili ya huduma kwa waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi wazinduliwa nchini Tanzania

Mfuko wa Msamaria mwema, unaosimamiwa na Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya kwa kushirikiana na Idara ya afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na Kampuni ya Gilead Sciences kutoka Marekani, wamekubaliana kimsingi kusaidia juhudi za kupambana na ugonjwa wa Ukimwi mkoani Shinyanga, kwa kusaidia juhudi za kupima virusi vya Ukimwi kwa wananchi 120, 000 pamoja na kuwapatia dawa za kurefusha maisha wale watakaokuwa wameathirika.


Makubaliano hayo yamefikiwa Jijini Dar es Salaam, tarehe 11 Februari 2014 katika Maadhimisho ya Siku ya 22 ya Wagonjwa Duniani. Huu ni mradi wa miaka mitano kwa ajili ya kupima virusi vya Ukimwi na kutoa dawa za kurefusha maisha. Ni mradi unaozingatia taaluma, maadili, usafi pamoja na mafunzo kwa walengwa watakaofaidika na mradi huu, kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa watoto yatima.

Mradi huu utaendelea kuongeza nguvu katika kuwahudumia wagonjwa wa Ukimwi, juhudi zinazofanywa na Jimbo Katoliki la Shinyanga katika Vituo vya Afya vya: Ngokolo, Bugisi, Buhangija na Mija. Mradi utatoa ufadhili kwa ajili ya mafunzo ya hali ya juu kwa wahudumu wa sekta ya afya, ili kuweza kutekeleza wajibu wao barabara pamoja na kuendelea kujikita katika mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi na maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto.

Wananchi watakaogundulika kuwa na maambukizi ya Ukimwi watapewa dawa za kurefusha maisha anasema Askofu mkuu Zygmunt Zimowski, Rais wa Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya. Mradi unapania pamoja na mambo mengine, kudhibiti maambukizi ya virusi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto, kama sehemu ya huduma makini inayotolewa na Kanisa katika kumhudumia mtu mzima: kiroho na kimwili, kama sehemu ya mwendelezo wa agizo la Kristo katika kuwahudumia wagonjwa.

Askofu mkuu Zygmunt Zimowski, amemkumbuka kwa namna ya pekee, Marehemu Askofu Aloysius Balina wa Jimbo Katoliki Shinyanga, aliyefariki dunia mwezi Novemba 2012. Aliamini kuhusu mafanikio ya mradi huu katika kuwahudumia watanzania waliokuwa wameathirika kwa ugonjwa wa Ukimwi. Ni mradi wa pekee, unaojumuisha Mfuko wa Msamaria Mwema, Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya pamoja na Kampuni ya Gilead.

Lengo li kuhakikisha kwamba, Kanisa Katoliki linashiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Ukimwi ambao umekuwa ni chanzo cha vifo na upotevu wa nguvu kazi nchini Tanzania.

Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa Duniani, yalianzishwa kunako mwaka 1992 na Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili, ambaye hapo tarehe 27 Aprili 2014 anatarajiwa kutangazwa kuwa Mtakatifu. Siku ya Wagonjwa Duniani inalenga pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, wagonjwa wanapata huduma bora pamoja na kuishirikisha Familia ya Mungu katika huduma kwa wagonjwa, kwani wagonjwa bado wanayo nafasi ya pekee katika maisha na utume wa Kanisa.

Kanisa linawahamasisha watu wa kujitolea, ili waweze kuwashirikisha jirani zao upendo, kwa kuwaonjesha upendo. Kanisa linapania pia kutoa majiundo makini ya kitaaluma na kimaadili kwa wahudumu wa sekta ya afya.

Umejiandaaje na Valentine’s day?


URAFIKI na Mahusiano ndio jina la safu hii mpenzi msomaji. Ni matumaini yangu umzima na unaendelea vema kukabiliana na shughuli mbambali za ujenzi wa taifa hili.

Nami bila hajizi nakukaribisha katika safu hii ili twende sambamba katika kuzungumzia suala la Siku ya Wapendanao (Valentine’s day), ambayo sherehe yake ni Ijumaa ya wiki ijayo – Februari 14.
Kwa kawaida huwa kuna sherehe nyingi na wengine kuwatumia zawadi wahusika kama familia na marafiki, na mojawapo ni hii Siku ya Wapendanao.

Hakuna binadamu yeyote duniani anayeishi duniani bila kukwaruzana na mtu yeyote, iwe rafiki au ndugu.
Hivyo hakuna kitu cha kukufanya uwe na wasiwasi juu ya siku hiyo kwamba utafanya nini kwa uwapendao au umpendae.
Unaweza kuifanya Siku ya Wapendanao iwe nzuri kwako. Kabla ya kufanya chochote; kwa maana kwamba ikiwa bado siku kadhaa hadi ifikie siku hiyo, tembelea maduka ya kadi na utazame aina mbalimbali za kadi.

Njia hii haitokufanya usahau kupata kadi nzuri na pia itakuepusha kukurupuka na kununua kadi ambayo haina mvuto wa kipekee.
Bila shaka wazo kubwa zaidi la zawadi ambalo huwepo miongoni mwa watu wengi ni maua.
Zawadi hizi pia huweza kutumiwa hata kwa walioajiriwa, yaani kwa wafanyakazi wa taasisi au kampuni fulani.

Hata hivyo, watu pia huwa wanasherehekea Siku ya Wapendanao kwa kuja na mitazamo tofauti na kutafakari ni zawadi gani inafaa kumtumia mtu.
Unaweza kuonyesha ukaribu na urafiki kwa wafanyakazi wenzako kwa kununua maua na kuwapa zawadi lengo likiwa ni kuonyesha upendo.
Lakini kwa wapenzi mbali na kupeana zawadi za maua yanayoonyesha upendo, pia wanaweza kutoka ‘out’ kwa ajili ya kwenda sehemu kubadilisha mawazo na kufanya siku hiyo iwe nzuri kwao.
Kama umepanga Siku ya Wapendanao ibaki kuwa kumbukumbu kwa ninyi wapendanao (wapenzi), usisahau kuhusisha zawadi zitokazo kwa sonara, kwani hakika ni chaguo zuri.

Kwa mfano unaweza kununua kimojawapo kati ya vitu vinavyopatikana sonara kwa lengo la kuboresha upendo wenu.
Epuka kuwa na kisirani pamoja na kumkera umpendae au uwapendao kwani kwa hakika utakuwa umeifanya siku hiyo kuwa mbaya kwako.

St. Jerome Emiliani

St. Jerome Emiliani
St. Jerome Emiliani
Feastday: February 8
1481 - 1537

Jerome Emiliani lay chained in the dark dirty dungeon. Only a short time before he had been a military commander for Venice in charge of a fortress. He didn't care much about God because he didn't need him -- he had his own strength and the strength of his soldiers and weapons. When Venice's enemies, the League of Cambrai, captured the fortress, he was dragged off and imprisoned. There in the dungeon, Jerome decided to get rid of the chains that bound him. He let go of his worldly attachments and embraced God.

Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya tano ya Kipindi cha Mwaka wa A wa Kanisa




Tunaendelea na kipindi chetu tafakari Neno la Mungu masomo Dominika ya V ya mwaka A. Masomo yanatualika kuwa chumvi na mwanga wa dunia. Katika somo la kwanza, Nabii Isaya anatualika kuwalisha na kuwavika maskini.
Katika kutenda kazi hiyo tunakumbuka Heri walio maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao. Kwa njia ya Nabii Isaya, Bwana anatangaza matokeo ya kazi njema hiyo, akisema nuru itakuzukia kama asubuhi na afya yako itakuwa njema na haki daima itakutangulia. Nabii Isaya haishii katika hayo bali pia anatangaza kuwa sala ya mwenye kutenda huduma kwa walio maskini itasikikika daima na hapa ndipo kuna furaha timilifu katika mapenzi yake Mwenyezi Mungu. 


Uaguzi wa Nabii Isaya unakuja wakati Waisrael wametoka utumwani Babilonia katika karne ya 5KK. Katika kipindi hicho, Waisraeli walitarajia kuwa mateso yangekuwa yamekwisha, lakini badala yake yaliendelea. Basi kwa kuwa katika nyakati za kale kama kulitokea shida fulani watu walifunga, ni katika mlengo huo basi, Waisraeli walifunga na kusali ili maisha yao yaweze kukaa sawasawa. Pamoja na jambo jema hilo la kufunga shida iliendelea yaani matajiri waliendelea kuwanyonya maskini. 


Ni katika madhulumu haya Waisraeli walianza kumlalamikia Mungu, kwa nini mambo hayabadiliki na hivi wakaanza kusema haina haja ya kufunga! Hapa ndipo sasa Nabii Isaya anakuja na jibu akisema Mungu hana kosa lolote, isipokuwa sala na kufunga kwenu hakufikii kiwango cha kumpendeza Mungu. Mungu anataka sala na kufunga kuliko na mzizi katika huduma kwa maskini na wenye taabu mbalimbali katika jumuiya yenu. Mpendwa sala yako ikoje?

Katika Somo la Pili Mt. Paulo anazidi kutangaza nguvu ya Mungu ambayo huongoza wahubiri wa Neno lake. Ndiyo kusema hakuna mhubiri anayeweza kujitapa yakwamba anatangaza injili kwa nguvu zake mwenyewe. Anawaalika Wakorinto watambue kuwa Neno na ujumbe wa Mungu haulali katika ufasaha na hekima ya kibinadamu kama watu wenye hekima katika kizazi hicho cha Wakorinto bali ni nguvu ya Msalaba wa Kristo mfufuka. Yeye mwenyewe anakiri kuwa hakuja kuonesha hekima yake bali kumjua Kristu tu na ndiyo shime yake. Ndiyo kusema anakiri udhaifu wake ambao utamruhusu aombe msaada toka kwa Mungu. 



Katika kitabu cha Matendo ya Mitume 20:9 inaonekana Mt. Paulo alipokuwa anahubiri kuna baadhi walianza hata kusinzia na kijana mmojawapo alianguka kupitia dirishani toka gorofa ya tatu! Ataka kusema nini? Ataka kusema ufasaha hauna nguvu bali Mungu mwenyewe katika Roho Mtakatifu. Na kama ingekuwa ufasaha ni wa maana, basi kijana huyu asingeingia katika shida ya usingizi. Hili halikumtisha Mt. Paulo bali Injili iliendelea kuhubiriwa na kuenea katika Ukorinto yote. Mpendwa unayenisikiliza Neno lenyewe lina nguvu bila madoido yetu, yafaa kuwa na imani thabiti.

Katika Injili ya Matayo, ujumbe na mwaliko ni ”kuweni chumvi na nuru”, na kwa namna hiyo kuangaza mbele ya watu na watu wayaone matendo yenu na wamtukuze Mungu. Mwinjili anatumia mfano wa chumvi na nuru, ambazo ni alama tumika katika nyakati za kale. Chumvi humaanisha mambo kadhaa: chumvi huleta radha kwenye chakula na hivi toka zamani ilimaanisha hekima na busara. Hata hivi leo utasikia watu wakisema, jamaa ana chumvi katika kichwa chake, wakimaanisha ana hekima na busara katika utendaji wake. Ndiyo kusema Wafuasi wa Kristo lazima watoe maneno yaliyo ya maana yaani yaliyojaa hekima ya kimungu na si bulaabulaa!

Jaribu kufikiri kama Neno la Mungu lisingekuwa Neno la furaha wapi tungepata matumaini! Wapi tungepata kutambua kuvumilia taabu na madhulumu katika maisha yetu! Wakristo ni lazima watoe radha ya kikristo ili maisha ya watu yawe ni maisha ya furaha na matumaini.

Mpendwa msomaji, chumvi si tu radha bali pia hutumika kutunza vyakula vizioze! Wakristo kwa maana hiyo lazima wawe watunzaji wa maisha ya watu katika ulimwengu huu. Uwepo wa Wakristu katika ulimwengu ni msaada ili mwanadamu asianguke katika unyanganyi na ufisadi na hivi dunia ikaangukia katika kuongozwa na misingi ya shetani.

Mpendwa msomaji, kwa kawaida chumvi haipotezi radha yake, sasa iweje Bwana aseme chumvi iliyoharibika? Bwana katika hili ataka kutuambia kuwa kama mhubiri anaacha kumtegemea Mungu na hivi anaweka mambo yake mbele basi ile hali ya Injili uchafuliwa ingawa Injili yenyewe hubaki, lakini kuna uozo huo ambao huchelewesha kasi yake.
Mpendwa mwana tafakari Bwana anatumia mfano wa mwanga akitaka waamini wawe mwanga unaoangaza wengine ili waweze kuona. Kama ambavyo jua huangaza ili tuone vema basi nasi vivyohivyo kwa wengine. Mwanga unao wajibu wa kuangaza kumbe hatuweki macho yetu kwenye mwanga bali kwa kile chema kinachotendwa na mwanga.

Wakristo si mwanga bali wanategemewa kutenda yaliyomema yaani matendo ya mwanga. Wakristo kwa vyovyote vile lazima wabaki wamejificha, kwa sababu ukitazama jua moja kwa moja utaharibu macho, kumbe tunachotakiwa kuona ni hospitali, vituo vya watoto yatima, shule na mambo yote mema yaani matendo ya mwanga. Mpendwa ni kwa njia ya matendo haya Injili ya Bwana inasonga mbele kwa kasi mpaka miisho yote ya dunia.
Nikutakie furaha na matumaini katika kuwa mwanga na chumvi ya dunia. Tumsifu Yesu Kristo.

Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya C.PP.S.

Mwenyeheri Yohane Paulo II kutangazwa kuwa Msimamizi wa Siku za Vijana Duniani



Baba Mtakatifu Francisko anawaalika vijana kujiandaa kikamilifu kwa ajili ya Maadhimisho ya Siku ya 29 ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2014 itakayoadhimishwa katika ngazi ya Kijimbo, Jumapili ya Matawi, ambayo kwa Mwaka huu inaadhimishwa hapo tarehe 13 Aprili.

Hii ni siku ambayo Maaskofu watazungukwa na umati wa vijana kutoka katika majimbo yao ili kufanya tafakari ya kina kuhusu kauli mbiu ya inayoongoza Maadhimisho haya: "Heri walio maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao". Hii ni sehemu ya muhtasari wa mafundisho makuu ya Yesu yanayopatikana katika Heri za Mlimani. 



Baraza la Kipapa la Walei linasema, huu ni ujumbe ambao unatolewa kwa mara ya kwanza kwa vijana na Baba Mtakatifu Francisko tangu alipochaguliwa kuwa Khalifa wa Mtakatifu Petro. Ni mwendelezo wa changamoto ya majiundo endelevu iliyoanzishwa na Mwenyeheri Yohane Paulo II na kuendelezwa kwa ari kubwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita.

Papa Francisko bado anakumbuka ule umati wa vijana kutoka sehemu mbali mbali za dunia uliomzunguka wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013 iliyofanyika mjini Rio de Janeiro. Baba Mtakatifu anaendeleza yale majadiliano ya kina kati yake na vijana yaliyoibuliwa wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani.

Kumbe, ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Kijimbo kwa Mwaka huu, ni sehemu ya maandalizi ya hija ya maisha ya kiroho, itakayofanyika katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa, kabla ya vijana hawajajimwaga kuelekea Jimbo kuu la Cracovia, Poland, kwa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2016.

Wachunguzi wa mambo wanasema, vijana watafunika Poland, ikizingatiwa kwamba, hizi zitakuwa ni mwendelezo wa utenzi wa sifa na shukrani kwa Mwenyezi Mungu baada ya Mwenyeheri Yohane Paulo II kutangazwa kuwa Mtakatifu. Tema zilizochaguliwa na Baba Mtakatifu katika kipindi cha miaka mitatu kutoka katika Heri za Mlimani zinazonesha jinsi ambavyo Baba Mtakatifu Francisko anavyothamini sehemu hii ya Injili kuwa ni kiini cha maisha ya Wakristo, mwaliko wa kuyamwilisha katika vipaumbele vyao vya maisha ya kila siku!

Baba Mtakatifu katika ujumbe kwa Siku ya Vijana Duniani anapenda kuwakumbusha vijana wa kizazi kipya kwamba, hii ni njia ambayo Yesu mwenyewe amewaonesha wafuasi wake, mwaliko wa kumfuasa katika maisha yao yote bila ya kujibakiza hata kidogo. Kumwilisha Heri za Mlimani kwa vijana wa kizazi kipya anasema Baba Mtakatifu ni kazi kweli kweli! 



Huu nimwaliko wa kumfuasa Kristo na kushikamana naye kwa dhati, tayari kutolea ushuhuda wa mabadiliko yanayobubujika kutoka katika undani wa maisha ya mwamini. Baba Mtakatifu anawachangamotisha vijana kutokubali kupata furaha ya mpito kwa mambo ya juu juu tu, bali wahakikishe kwamba, wanajitaabisha kutafuta furaha ya kweli inayobubujika kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Katika ujumbe wake, Baba Mtakatifu anafafanua kwa kina na mapana maana ya umaskini wa roho kadiri ya mafundisho ya Yesu, ambaye aliuchagua mwenyewe na hatimaye kuutolea ushuhuda katika maisha na utume wake hapa duniani, mwaliko kwa vijana kuiga mfano wa maisha ya Mtakatifu Francisko, aliyekuwa tajiri wa kutupwa, lakini akaacha yote na kuukumbatia ufukara wa Kiinjili. Hii ndiyo changamoto kubwa iliyoko mbele ya vijana wa kizazi kipya na wala si maji kwa glasi!

Baba Mtakatifu Francisko anawaalika vijana kutubu na kumwongokea Yesu Kristo, huku wakijitahidi kuishi maisha yanayosimikwa katika kiasi, wakitafuta mambo msingi katika maisha yao pamoja na kujenga mshikamano wa upendo na maskini pamoja na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii. Maskini ni sehemu ya Fumbo la Mwili wa Kristo linaloendelea kuteseka, mwaliko kwa kila mwamini kuhakikisha kwamba, anaguswa na umaskini, taabu na mahangaiko ya jirani zake; kwa njia hii vijana wanaweza kuwa kweli ni walimu wa maisha, kwa kuwamegea wengine utajiri wa maisha ya kiroho na kiutu unaobubujika kutoka katika undani wa maisha yao.

Baba Mtakatifu Francisko anasema, kuna uhusiano mkubwa kati ya tema iliyoongoza Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013 huko Rio de Janeiro "Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi..." na kauli mbiu ya mwaka huu yaani, "Heri walio maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao". Ufukara wa Kiinjili ni muhimu sana katika ujenzi wa ufalme wa Mungu sehemu mbali mbali za dunia. Ni ufukara unaojionesha katika hali ya kawaida pasi na makuu, kiasi cha kuweza kuwa ni chachu ya Uinjilishaji Mpya.

Baba Mtakatifu anawakumbusha vijana wa kizazi kipya kwamba, hapo tarehe 22 Aprili 2014, Kanisa litafanya kumbu kumbu ya Miaka 30 tangu Msalaba wa Jubilee ya Mwaka wa Ukombozi ulipoanza kutembezwa sehemu mbali mbali za dunia. Hizi zilikuwa ni juhudi za Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili kwa ajili ya Kanisa, tangu wakati ule, Msalaba umekuwa ni sehemu ya hija ya maisha ya vijana wa kizazi kipya.

Kwa hakika, baada ya Mwenyeheri Yohane Paulo II kutangazwa kuwa Mtakatifu, Kanisa litaendelea kumshukuru Mungu kwa kumtangaza rasmi kuwa ni Msimamizi wa Maadhimisho ya Siku za Vijana Duniani. Mwenyeheri Yohane Paulo II alikuwa ni muasisi na mhamasishaji mkuu wa Siku za Vijana Duniani, hadi leo hii, tukio hili linaendelea kuwa na mvuto na mashiko makubwa katika maisha na utume wa Mama Kanisa miongoni mwa vijana, kwa kutambua kwamba, vijana ni jeuri na matumaini ya Kanisa kwa sasa na kwa siku za usoni!

Daily Reading for Friday, February 7th, 2014



Reading 1, Sirach 47:2-11

2 As the fat is set apart from the communion sacrifice, so was David chosen out of the Israelites.
3 He played with lions as though with kids, and with bears as though with lambs.
4 While still a boy, did he not slay the giant and take away the people's shame, by hurling a stone from his sling and cutting short the boasting of Goliath?
5 For he called on the Lord Most High, who gave strength to his right arm to put a mighty warrior to death and assert the strength of his own people.
6 Hence they gave him credit for ten thousand, and praised him while they blessed the Lord, by offering him a crown of glory.
7 For he destroyed the enemies on every front, he annihilated his foes, the Philistines, and crushed their strength for ever.
8 In all his activities he gave thanks to the Holy One Most High in words of glory; he put all his heart into his songs out of love for his Creator.
9 He placed singers before the altar, melodiously to sing;
10 he gave the feasts their splendour, the festivals their solemn pomp, causing the Lord's holy name to be praised and the sanctuary to resound from dawn.
11 The Lord took away his sins, making his strength ever greater; he gave him a royal covenant, and a glorious throne in Israel.

Responsorial Psalm, Psalms 18:31, 47, 50, 51

31 For who is God but Yahweh, who is a rock but our God?
47 the God who gives me vengeance, and subjects whole peoples to me,
50 He saves his king time after time, displays his faithful love for his anointed, for David and his heirs for ever.

Gospel, Mark 6:14-29

14 King Herod had heard about him, since by now his name was well known. Some were saying, 'John the Baptist has risen from the dead, and that is why miraculous powers are at work in him.'
15 Others said, 'He is Elijah,' others again, 'He is a prophet, like the prophets we used to have.'
16 But when Herod heard this he said, 'It is John whose head I cut off; he has risen from the dead.'
17 Now it was this same Herod who had sent to have John arrested, and had had him chained up in prison because of Herodias, his brother Philip's wife whom he had married.
18 For John had told Herod, 'It is against the law for you to have your brother's wife.'
19 As for Herodias, she was furious with him and wanted to kill him, but she was not able to do so,
20 because Herod was in awe of John, knowing him to be a good and upright man, and gave him his protection. When he had heard him speak he was greatly perplexed, and yet he liked to listen to him.
21 An opportunity came on Herod's birthday when he gave a banquet for the nobles of his court, for his army officers and for the leading figures in Galilee.
22 When the daughter of this same Herodias came in and danced, she delighted Herod and his guests; so the king said to the girl, 'Ask me anything you like and I will give it you.'
23 And he swore her an oath, 'I will give you anything you ask, even half my kingdom.'
24 She went out and said to her mother, 'What shall I ask for?' She replied, 'The head of John the Baptist.'
25 The girl at once rushed back to the king and made her request, 'I want you to give me John the Baptist's head, immediately, on a dish.'
26 The king was deeply distressed but, thinking of the oaths he had sworn and of his guests, he was reluctant to break his word to her.
27 At once the king sent one of the bodyguard with orders to bring John's head.
28 The man went off and beheaded him in the prison; then he brought the head on a dish and gave it to the girl, and the girl gave it to her mother.
29 When John's disciples heard about this, they came and took his body and laid it in a tomb.

St. Moses


St. Moses




Died: 372

Arab hermit and bishop who is called “the Apostle of the Saracens.” He lived in the desert regions of Syria and Egypt, caring for the local nomadic tribes. When the Romans imposed peace upon the Saracens, Queen Mavia, the Saracen ruler, demanded that Moses be consecrated a bishop. He accepted against his will and maintained the peace between the Saracens and Rome. The Saracens were a nomadic people of the Syro-Egyptian desert so designated by the Romans.

Kila mtu anapaswa kupata huduma makini ya afya!

Askofu mkuu Zygmunt Zimowski, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya wafanyakazi katika sekta ya afya katika ujumbe wake kwa Maadhimisho ya Siku ya Dawa Kitaifa nchini Italia na katika baadhi ya Nchi za Ulaya inayoadhimishwa hapo tarehe 8 Februari, 2014 anasema, kuna haja kwa Serikali pamoja na wadau mbali mbali kuhakikisha kwamba, watu wanapata huduma sawa ya afya, mahali popote pale walipo, lakini maskini, watoto na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii wapewe kipaumbele cha kwanza.

Askofu mkuu Zimowski anasema, katika nchi 90 duniani,

SAUTI ZA BUSARA: Ni zaidi ya Tamasha la burudani

TAMASHA la Sauti za Busara ni miongoni mwa machache ambayo yamejenga historia kutokana na kuutangaza na kuuendeleza muziki wa Tanzania nje ya mipaka yake, ambako mwaka huu litafanyika kuanzia Februari 13 hadi 16. Mbali na burudani, Tamasha la Busara ambalo ni la 11 mwaka huu tangu kuanzishwa, limekuwa kiunganishi kizuri kwa wasanii wa hapa nyumbani na wale wa kimataifa, jambo linalotoa nafasi ya kubadilishana ujuzi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Sauti za Busara Promotions, Simai Said Mohamed, anasema lengo la kuandaa tamasha hilo ni kuwaleta watu pamoja na kuonyesha utajiri wa muziki wa kisasa, ambao umebuniwa katika nchi za Afrika Mashariki, nchi nyingine kutoka barani Afrika na kwingineko duniani.

Mohamed anasema, tamasha hilo linalojulikana kama ‘Tamasha Rafiki Katika Sayari’ ni la kimataifa linalosherehekea muziki wa Kiafrika kila mwaka na kwamba vikundi 32 vitafanya maonyesho jukwaani ndani ya Ngome Kongwe visiwani Zanzibar.
Anasema vikundi hivyo vimechaguliwa kutokana na maombi zaidi ya 560 na vinawakilisha nchi 19, zikiwemo za Afrika Mashariki, Afrika Kusini na Magharibi, maeneo ya Mto Nile, pia kutoka Puerto Rico na inatarajiwa zaidi ya wasanii 200 watafika Zanzibar kufanya maonyesho ya muziki.
Mwenyekiti huyo anawataja miongoni mwa wasanii maarufu kutoka Tanzania watakaoshiriki Tamasha la Sauti za Busara 2014 kuwa ni pamoja na Jhiko Manyika ‘Jhikoman’, mwanamuziki anayejulikana kwa muziki wake wa reggae, ambaye atazindua ziara yake ya kuitembelea dunia jukwaani wakati wa onyesho lake.

Wasanii wengine kutoka hapa nchini ni Ashimba,Batarokota, Swahili Vibes, Hoko Roro, Seven Survivor, Abantu Mandingo, Segere Original na Kazimoto, anayemshirikisha Jackie Kazimoto kutoka ‘The Internationally-Acclaimed’, Jagwa Music.
Anasema tamasha hilo pia litamkaribisha mwanamuziki mkongwe aliyefanikiwa kimuziki kutoka nchini Ghana, Ebo Taylor, pia atakuwepo Sona Jobarteh, mwanahistoria kutoka Gambia na ‘Jupiter and Okwess International’ mwanamuziki mwenye mafanikio kutoka Jamhuri ya Watu wa Congo, ambaye anapasua anga katika fani ya muziki Afrika na kwingineko duniani.
Mwenyekiti huyo anawataja wasanii watakaopamba tamasha hilo na nchi zao kwenye mabano kuwa ni Jhikoman, Ashimba, Hoko Roro, Seven Survivor, Abantu Mandingo, Segere Original, Kazimoto (Tanzania),  Swahili Vibes, Baladna Taarab, Tausi Women’s Taarab, Rajab Suleiman & Kithara ft. Derya Takkali (Zanzibar),  Joel Sebunjo ft. Lenna Kuurmaa (Uganda), Moyize (Rwanda),  Ricky na Marafiki (Kenya).

Wengine ni Ebo Taylor (Ghana na Ujeruman),   Jupiter & Okwess International (DRC),  Joe Driscoll and Sekou Kouyate (USA na Guinea),  The Nile Project (Nile Basin), Noumoucounda Cissoko (Senegal), Oy (Ghana na Uswisi), Addis Acoustic Project (Ethiopia), Sona Jobarteh (Gambia na Uingereza), Tarabband (Misri na Sweden), Majestad Negra (Puerto Rico), HAJAmadagascar and The Groovy People ft. Werner Puntigam (Madagascar, Ufaransa na Australia), Tritonik (Mauritius), Kara Sylla Ka (Senegal na Uswisi), Dizu Plaatjies & The Ibuyambo Ensemble (Afrika Kusini), Street Rat and Body Mind & Soul (Malawi),  Moyize (Rwanda), Ricky na Marafiki (Kenya), Waldemar Bastos (Angola na Portugal) na wengineo wengi kutoka nchi mbalimbali.

Mohamed anaongeza kuwa kwa upande mwingine, mwaka huu burudani ya muziki itajumuisha ‘paredi’ siku ya ufunguzi, pia kutakuwa na ‘Movers & Shakers’ (kongamano la wataalamu), na uonyeshaji wa filamu ndefu za muziki za Kiafrika ambazo zimeshinda tuzo mbalimbali.
“Kwa kushirikiana na wafadhili wa miradi HIVOS, pia tutautambulisha mradi mpya unaojulikana kama ‘Santuri Safari’, mradi ambao utaangalia zaidi jukumu la DJ kwa wakati huu na kuangalia jinsi ya utamaduni wa DJ katika kukuza muziki wa Afrika Mashariki,” anasema.
Mohamed anasema DJ waalikwa, wazalishaji wa muziki, wataalamu wa sauti, waandaaji wa matamasha na wataalamu wa sanaa kutoka ukanda wa Afrika, watajumuika pamoja Zanzibar na kufanya kazi pamoja na kupata mafunzo.

“Tunaona hii ni fursa adimu kushirikiana na kuangalia kuibuka kwa vitu vya kisasa vinavyotokea katika muziki wa elektroniki na utamaduni wa MaDj, na kuangalia jinsi ya kuukuza muziki kikanda na katika anga la kimataifa kwa wakati huu na kwa miaka ijayo,” anasema.
Anasema, kutakuwa na muziki kipindi cha jioni wakati wa jua kuzama maeneo ya mjini na Ijumaa na Jumamosi kutakuwa na burudani ya muziki Ngome Kongwe baada ya kumalizika kwa maonyesho ya moja kwa moja jukwaani.
Anasema, pia tamasha hilo linakuza mambo mbalimbali kupitia ‘Buasara Xtra’ kwa kujumuisha matukio ya maonesho, ambako kwa pamoja hutoa fursa kwa wasanii wazawa kuonyesha kazi zao na kuwafanya wageni watembelee maeneo mengine ya Kisiwa cha Zanzibar.
Anasema zaidi ya Watanzania 150 huajiriwa kila mwaka kama wafanyakazi wa tamasha na pia kwa upande wa kukuza na kulinda muziki na utamaduni wa Zanzibar, Sauti za Busara inatumia nafasi iliyonayo katika kuuthamini muziki wa Bara zima la Afrika, kukuza amani, kujenga jamii ya pamoja Afrika Mashariki na kukuza utalii wa kitamaduni.
“Kwa kila siku kiingilio katika tamasha ni bure kabla ya saa 11 jioni kwa Watanzania wote, na baada ya hapo kiingilio ni sh 5,000 pia ukitaka maelezo zaidi, unaweza kutembelea www.busaramusic.org na kwamba
Busara Promotions ni taasisi inayowezeshwa kwa mwaka mzima na Ubalozi wa Norway,” anasema.
Mohamed, anatoa shukurani kwa Bodi ya wadhamini na wafadhili kama Hivos, Goethe-Institut, the Embassy of the United States of America, Swiss Agency for Development and Cooperation, African Music Festivals Network, Zanzibar Unique, Memories of Zanzibar, Ultimate Security, Ubalozi wa Ufaransa, Southern Sun Hotel, Azam Marine, Ubalozi wa Ujerumani na SMOLE II.

St. Teresa of Avila - Doctor of the Church



St. Teresa of Avila - Doctor of the Church
Feastday: October 15
Patron of Headache sufferers, Spanish Catholic Writers
1515 - 1582

Less than twenty years before Teresa was born in 1515, Columbus opened up the Western Hemisphere to European colonization. Two years after she was born, Luther started the Protestant Reformation. Out of all of this change came Teresa pointing the way from outer turmoil to inner peace.
Teresa's father was rigidly honest and pious, but he may have carried his strictness to extremes. Teresa's mother loved romance novels but because her husband objected to these fanciful books, she hid the books from him. This put Teresa in the middle -- especially since she liked the romances too. Her father told her never to lie but her mother told her not to tell her father. Later she said she was always afraid that no matter what she did she was going to do everything wrong.
When she was five years old she convinced her older brother that they should, as she says in her Life, "go off to the land of the Moors and beg them, out of love of God, to cut off our heads there." They got as far as the road from the city before an uncle found them and brought them back. Some people have used this story as an early example of sanctity, but this author think it's better used as an early example of her ability to stir up trouble.
After this incident she led a fairly ordinary life, though she was convinced that she was a horrible sinner. As a teenager, she cared only about boys and clothes

Mchango wa Kanisa Katoliki katika sekta ya elimu unaweza sasa kupatikana kwenye tovuti!

Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki limezindua tovuti yake inayotoa habari muhimu kuhusu mchango wa Kanisa Katoliki katika sekta ya elimu ya juu, sehemu mbali mbali duniani. Hii ni sehemu ya utekelezaji wa Itifaki iliyoridhiwa kati ya Vatican na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, UNESCO katika masuala ya sekta ya elimu kimataifa kwa kutambua na kuthamini vyeti mbali mbali vinavyotolewa na Vyuo vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu zinazoongozwa na kumilikiwa na Kanisa Katoliki.

Hii ni fursa kwa Vatican kuendelea kuchangia kwa kina na mapana katika sekta ya elimu kwa kutoa habari zinazoonesha mchango wa Kanisa ili kushirikishana na nchi nyingine ambazo tayari zimekwisharidhia Itifaki hii pamoja na UNESCO. Tovuti ya Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki kwa sasa lina sehemu kuu mbili: Sehemu ya kwanza inazungumzia Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki na majukumu yake kwa ujumla.

Sehemu ya pili imesheheni hati na nyaraka mbali mbali zinazoweza kufanyiwa rejea na wasomi kuhusu: Hekima ya Kikristo na Hati ya Kanisa kuhusu Vyuo Vikuu vya Kikatoliki. Tovuti hii inaonesha uhusiano wa kimataifa kati ya Baraza la Kipapa la Taasisi mbali mbali katika sekta ya elimu. Watumiaji wa tovuti hii wanaweza pia kupata takwimu na habari kutoka katika "Pango hifadhi ya Nyaraka za Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki". Ukitaka kufaidi zaidi unaweza kutembelea Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki kwa anuani ifuatayo: www.educatio.va


Miili 8 yapatikana mgodini A. Kusini


Mgodi wa Doornkop uko Magharibi mwa Johannesburg.
Maafisa wa shughuli ya uokoaji nchini Afrika Kusini wanasema kuwa wamepata miili 8 ndani ya mgodi walimokuwa wamekwama wachimba migodi hao baada ya moto kuzuka na kuangukiwa na mawe wakiwa ndani ya mgodi huo.
Kwa mujibu wa serikali, Mfanyakazi mmoja angali hajapatikana katika mgodi wa Doornkop, Magharibi mwa Johannesburg.
Awali wachimba migodi wanane walipatikana wakiwa hai katika chumba kimoja chini ya ardhi ambak