Baraza la Maaskofu Katoliki Angola, Sao Tome na Principe linasema, sera za utoaji mimba ni mauaji ya watu wasiokuwa na hatia, ni kinyume cha Amri za Mungu; utamaduni na utambulisho wa wananchi wa Angola. Wananchi wanakumbushwa kwamba, maisha ya
binadamu ni matakatifu tangu pale mtoto anapotungwa mimba tumboni mwa mama yake hadi mauti ya kawaida yanapomfika kadiri ya mapenzi ya Mungu.
Hakuna mtu mwenye mamlaka yanayomruhusu kuwapokonya wengine zawadi ya uhai kwa kisingizio chochote kile. Ni jukumu na dhamana na wanafamilia, wahudumu wa sekta ya afya na wanasiasa kutoruhusu wala kushabikia sera za utoaji mimba na badale yake, wawe mstari wa mbele kulinda na kutetea zawadi ya uhai kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Maaskofu wanasema kwamba, kadiri ya mila na tamaduni za wananchi wa Angola katika ujumla wao, vitendo vya utoaji mimba havikubaliki kamwe kwani ni kielelezo cha mkosi katika familia. Hii ni changamoto kwa waamini na watu wenye mapenzi mema kusimama kidete kulinda na kutetea Injili ya uhai, kwani sera dhidi ya Injili ya uhai ni kutaka kusababisha majanga katika Jamii
.
Ni matumaini ya wananchi wa Angola kwamba, wabunge wao watasimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya uhai na kamwe hawatakubali kushinikizwa ili kuunga mkono sera za utoaji na vizuia mimba.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni