Mpendwa msikilizaji wa Neno la Mungu kipindi tafakari masomo Dominika, tayari tuko katika Dominika ya 32 ya mwaka C wa Kanisa, ni Dominika ambayo kwayo tunafunga wiki ambamo tuliwakumbuka na kuwaombea marehemu wetu.
Na kwa hakika Neno la Mungu ambalo tunalitafakari Dominika hii lina jambo la pekee linalogusa marehemu na nyakati za mwisho. Ujumbe wa Neno la Mungu kwa ufupi ni kwamba Mungu ni Mungu wa wazima na si wa wafu.
Mpendwa msikilizaji, katika Injili tunayoitafakari tunakutana na baadhi ya Masadukayo ambao kwa kawaida ni kikundi cha watu wanganganizi wa mila zao, wasiosadiki katika ufufuko wa wafu, wenye kushika utawala wa pesa katika masinagogi na mahekalu na kwa namna hiyo walikuwa wameshikamana na urka wa kikuhani. Watu hawa mpendwa msikilizaji, wanaweka swali mbele ya Bwana, swali ambalo mantiki yake ni kutaka kuangusha mafundisho ya Bwana juu ya UFUFUKO wa wafu!
Katika mantiki hiyo Masadukayo wanakuja na hadithi amabayo hatuna uhakika kama ni ya kweli ama ni ya kutunga. Hadithi yagusa mwanamke aliyeolewa na wanaume saba ndugu ambao walikuwa wakirithishana kadiri ya sheria ya Musa na kadiri ya hadithi hiyo hakupata mtoto na wanaume hawa! Kama kawaida naye mwisho alikufa. Sasa swali mtego kwa Bwana linakuja likisema huyu mama katika ufufuo wa wafu atakuwa mke wa nani? Pamoja na hilo unaona jinsi ambavyo Masadukayo ni wajanja, wanatumia Biblia kusimamia hoja yao!
Mpendwa mwana wa Mungu, katika kujibu swali hilo, Bwana atahakikisha ukweli wa ufufuko na kisha atakemea mtizamo wa Kisadukayo unaogusa ulimwengu wa vitu, badala ya ulimwengu wa ufufuko, ulimwengu wa Kimungu. Bwana atasema mara moja kuwa katika ulimwengu ujao yaani ufufuko kwa wale wateule wa Mungu, hakuna kuoa wala kuolewa, hakuna kifo tena bali wote watakuwa kama malaika, na kwa vile ni wana wa ufufuko basi ni wana wa Mungu.
Katika hili Bwana anaweka mbele yetu maisha mapya, maisha baada ya ufufuko uhakika wa imani yetu. Ndiyo kusema maisha ya ufufuko si mwendelezo wa raha za kidunia, yaani kunywa na kula bali ni maisha tofauti, yenye thamani tofauti. Ni kweli mwanadamu daima anasubiri ukamilifu wa maisha yake lakini ni lazima atambue kuwa si mwendelezo wa mambo ya kidunia bali ni zawadi ya kimungu, ni upendo upeo, mastahili ya msalaba wa Kristo.
Mpendwa msikilizaji, jambo hili tulilosikia, laweza kupelekea kufikiri je kuna haja gani ya kuwa na vifungo vya mapendo ya kindoa, kama haya mambo hayana nafasi katika ufufuko? Kwa hakika haina maana kwamba kifungo cha mapendo kama hayo hakitakuwepo, bali kitakuwa katika kipimo cha ukamilifu tofauti na kipimo cha leo! Katika barua ya Mtakatifu Yohane twasoma “Wapenzi sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa, lakini twajua yakuwa atakapodhirishwa tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo! IYn 3:2.
Kumbe maisha ya mapendo tuyaishiyo hapa duniani yatakuwa katika ukamilifu wake ambao hatuwezi kuutambua kwa macho bali kwa imani thabiti katika mausia ya Bwana.
Mpendwa msikilizaji, Injili tunayoitafakari inagusa maisha ya mtu na hasa mashaka yake katika maisha ya kila siku. Kwa hakika tangu karne za kwanza za Kanisa mpaka leo bado kuna Masadukayo na bado kati yetu waamini na wasio waamini tunajiuliza hivi huyu ndugu yangu aliyekufa ni kweli anawenda mbinguni? Je, ataendelea kunipenda kama ambavyo ninafikiri mimi? Je mwili wake utaungana na roho, na ni kwa namna gani? Kwa uwepo wa maswali haya kunafajionesha katika kulia na kuomboleza mmoja anapotoweka kwa njia ya kifo, ndiyo kusema hatuzoei kifo!
Basi ndugu yangu mpendwa, katika sehemu ya mwisho ya kifungu hicho cha Injili ya Luka, Bwana anajibu shida yetu sisi tulio na imani akisema: lakini yakuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionesha katika sura ya kijiti hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahim una Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo, naye si Mungu wa wafu bali wa walio hai!
Mpendwa msikilizaji jambo la ufufuko ni kiini na kilele cha imani yetu, imani ambayo ni mwanga. Ili kujenga msimamo huo lazima mmoja ajenge uthabiti katika imani kama asemavyo Baba Mtakatifu Francisko kuwa, Imani ni alama za maandalizi ya kuelekea katika mji wa ahadi unaoandaliwa na Mungu kwa binadamu. Mji ambao ni wa wazima na si wa wafu. Na kwa kutambua hili, tunaweza kuona kwamba, kwa kila binadamu imani humwangazia binadamu juu ya mahusiano yake na Mungu na wanadamu wenzake. Kwa kusadiki namna hii kunatuondolea wasiwasi na kutupa tumaini ya kwamba tutaurithi uzima wa milele. Tumsifu Yesu Kristo.
Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya, C.PP.S.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni