Week Hot newz
-
Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa...
-
Teach me, Lord Jesus, to be generous: to serve You as You deserve; to give, not counting the cost; to fight, not heeding the wound...
-
Uchunguzi wa mwili wa Askofu Józef Wesolowski, umekamilika na matokeo kwamba amekufa kifo cha kawaida. Kuf...
-
Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki limezindua tovuti yake inayotoa habari muhimu kuhusu mchango wa Kanisa Katoliki katika sekta ya elimu ...
-
Reading 1, Romans 6:19-23 19 I am putting it in human terms because...
-
NA OSCAR ASSENGA, TANGA-Tanzania.Gazeti Mtanzania. KATIBU wa Chama cha Watu Wenye Albino Mkoa wa Tanga (TAS), Mah...
-
Mpendwa mwana wa Mungu, tuko tena pamoja katika ile habari ya furaha ndiyo kushirikishana mapendo ya Mungu kwa njia ya meza y...
St. Joseph yakumbuka watoto yatima
na Paskal Linda-Dar es salaam
SHULE ya Msingi St. Joseph iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo, imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandalwa kilichopo Mbweni Vijibweni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Msaada huo wenye thamani ya sh milioni tatu uliotolewa kwa watoto 92 wanaolelewa na kituo hicho, ni chakula, sabuni, sukari, vinywaji baridi, mafuta ya kupikia na nguo.
Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa msaada huo juzi, Mkurugenzi wa shule hiyo, Christa Rweyemamu, alisema uamuzi wa kusaidia kituo hicho ulifikiwa kupitia kitengo cha klabu ya huduma ya jamii ya shule hiyo na kuwashirikisha wazazi.
“Tulishirikisha wazazi ambao waliitikia kwa moyo mmoja na tukafikia mchango wa vifaa hivi na fedha taslimu sh 600,000 ambazo zitasaidia kulipia ada za watoto,” alisema.
Akitoa shukrani, mmiliki wa kituo hicho, Halima Mpeta, alisema wamefarijika na msaada kwa watoto hao ambao umetokana na ushawishi wa watoto wenzao
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni