Week Hot newz

St. Joseph yakumbuka watoto yatima





na Paskal Linda-Dar es salaam




SHULE ya Msingi St. Joseph iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo, imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandalwa kilichopo Mbweni Vijibweni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Msaada huo wenye thamani ya sh milioni tatu uliotolewa kwa watoto 92 wanaolelewa na kituo hicho, ni chakula, sabuni, sukari, vinywaji baridi, mafuta ya kupikia na nguo.

Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa msaada huo juzi, Mkurugenzi wa shule hiyo, Christa Rweyemamu, alisema uamuzi wa kusaidia kituo hicho ulifikiwa kupitia kitengo cha klabu ya huduma ya jamii ya shule hiyo na kuwashirikisha wazazi.

“Tulishirikisha wazazi ambao waliitikia kwa moyo mmoja na tukafikia mchango wa vifaa hivi na fedha taslimu sh 600,000 ambazo zitasaidia kulipia ada za watoto,” alisema.



Akitoa shukrani, mmiliki wa kituo hicho, Halima Mpeta, alisema wamefarijika na msaada kwa watoto hao ambao umetokana na ushawishi wa watoto wenzao

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni