SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeihamisha mechi ya kuwania tiketi ya fainali za Kombe la Dunia kwa wanawake wenye umri chini ya miaka 20 kati ya Tanzania ‘Tanzanite’ na Afrika Kusini ‘Amajita’ kutoka Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza hadi Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Tanzanite inajiandaa kuikaribisha Amajita Desemba 7 katika mechi ya kwanza ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia zitakazopigwa mwakani nchini Canada, baada ya kuwang’oa Msumbiji kwa jumla ya mabao 15-1.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Saad Kawemba kwa niaba ya ofisa habari, shirikisho lake limeamua kufanya mabadiliko ya uwanja kutokana na CCM Kirumba kutokuwa na ubora stahili.
Kawemba alisema licha ya jitihada zilizofanyika katika kuufanyia marekebisho, bado jaribio la kuwahi muda sahihi kuelekea mechi hiyo haliwezi kuzaa matunda, kutokana na ubovu wa vyumba vya kuvalia na miundombinu.
“Tunaposema vyumba vya kuvalia tunajumuisha vyoo, bafu na sehemu ya kupumzikia wachezaji. Hali katika vyumba vya Kirumba ni mbaya ikiwamo ukosefu wa umeme na aina ya matangazo yasiyohitajika kwa mechi rasmi kutokana na sababu za kiudhamini,” alisema Kawemba.
Aliwataka wakazi wa Kanda ya Ziwa kuwa wavumilivu kutokana na uamuzi huo wa TFF, huku akiwataka kuvuta subira kwani safari ya Tanzanite ni ndefu na kama itafanikiwa kukitoa kikosi cha Amajita, wanaweza kurejea huko kwa mechi zijazo.
“Kama itafanikiwa kuitoa Afrika Kusini, Tanzanite itaingia raundi ya tatu na ya mwisho, wakati huo naamini maboresho Kirumba yatakuwa yamefikia pazuri, hivyo tunaweza kurejea Mwanza kwa mechi ya nyumbani,” alisisitiza Kawemba.
Amajita inayonolewa na Maqsood Chenia, ilitinga raundi ya pili baada ya kuwang’oa vijana wenzao wa Botswana kwa mabao 7-2.
Timu mbili kutoka Afrika zitafuzu kwa fainali za Dunia, zitakazofanyika mwakani kuanzia Agosti 5 hadi 24.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
-
NA MWANDISHI WETU, MWANZA AZAM FC wameshindwa kuibuka na ushindi katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, baada ya kula...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni