Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
TANZIA:Askofu John Simalenga afariki dunia!
Kanisa la Anglikani Tanzania limepata pigo la kufiwa na Askofu John Simalenga (60) wa Dayosisi South West Tanganyika iliyopo Njombe, Mkoani Iringa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Katibu mkuu wa Kanisa Anglikani Tanzania Canoni Dk. Dickson Chilongani alisema kuwa Kanisa limepata pigo kubwa kutokana na kifo cha Askofu Simalenga ambaye aliugua kwa muda mfupi.
Alieleza kuwa kifo cha Askofu Simalenga kimetokea Novemba, 24, 20013 muda mfupi baada ya kuruhusiwa kutoakatika hospitaliya ya kanisa hilo iliyopo Njombe. Alisema kuwa askofu alianza kuumwa alikwenda hospitali kwa ajili ya kupima afya yake na alipofika hospitali ilibainika kuwa alikuwa na maralia pamoja na sukari kupanda hadi kufikia 30 huku shinikizo la moyo kuwa juu.
Canon Dk. Chilongani alisema kuwa baada ya madaktari kubaini kwamba Askofu anasumbuliwa na matatizo hayo alipewa dawa na kuruhusiwa kwenda nyumbani wakitegemea kuwa dawa hizo zingemsaidia kutuliza magonjwa ambayo alibainika kuwa nayo. Alisema kinyume na matarajio ya madaktari, Askofu Simalenga baada ya kurudi nyumbani hali ilibadilika ghafla na kufariki dunia majira ya saa 11 alfajiri.
Marehemu Askofu John Simalenga alizaliwa tarehe 30 Novemba 1953 na kufariki dunia tarehe 24 Novemba 2013. Alisema Kanisa Anglikani linaendelea na taratibu za maandali ya utaratibu wa mazishi ya mwili wa askofu huyo ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa taarifa kwa wachungaji pamoja na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni