
Anyolo Askofu, wa Jimbo la Homabay, pia anasema , ziara ya Papa ni ziara ya kichungaji, na hivyo Kanisa litashirikiana na Serikali ya Kenya, katika maandalizi na ufanikishaji.Askofu Anyolo ameeleza na kuomba sala za waamini na msaada wa kihali kwa ajili ya kufanikisha ziara ya Papa nchini Kenya.
Maaskofu wa Kenya katika ziara yao akitume ya kila baada ya miaka mitano katika Ofisi za Idara ya Curia ya Roma na Kiti Kitakatifu , waliyoifanya hapo 13-17th, Aprili, 2015, walitoa mwaliko kwa Baba Mtakatifu alitembelee taifa la Kenya.
Katika ziara hii ya kwanza kwa Papa Francisco kuzuru bara la Afrika, pia atatembelea Uganda na Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni