Week Hot newz

Papa Francisko Mwezi Novemba kutembelea Africa

Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki (KCCB), Askofu  Philip Anyolo, ametangaza rasmi juu ya ujio wa Papa nchini Kenya kwamba itakuwa mwezi Novemba 2015.  Hilo limo katika barua yake kwa Waamini Wakristo aliyoitoa kwa niaba ya Maaskofu,tarehe 27, Agosti, 2015.  Askofu Anyolo kasema, "Baba Mtakatifu amekubali mwaliko wa Maaskofu wa kuitembelea  Kenya mwezi Novemba 2015.

Anyolo Askofu, wa Jimbo la  Homabay, pia anasema , ziara ya Papa ni ziara ya kichungaji, na hivyo Kanisa litashirikiana na Serikali ya Kenya, katika maandalizi na ufanikishaji.Askofu Anyolo ameeleza na kuomba sala za waamini na msaada wa kihali kwa ajili ya kufanikisha ziara ya Papa nchini Kenya.

Maaskofu wa Kenya katika ziara yao akitume ya kila baada ya miaka mitano katika  Ofisi za Idara ya Curia ya Roma na Kiti Kitakatifu , waliyoifanya hapo  13-17th, Aprili, 2015, walitoa mwaliko kwa  Baba Mtakatifu alitembelee taifa la Kenya.
Katika ziara hii ya kwanza kwa Papa Francisco kuzuru bara la  Afrika, pia atatembelea Uganda na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni