Week Hot newz

Kanisa linahamasishwa kuwa ni shuhuda wa huruma ya Mungu katika ukweli!

Baada ya Baba Mtakatifu Francisko kuzindua maadhimisho ya Sinodi ya Maaskofu, Kardinali Peter Erdo, mwezeshaji mkuu alitoa tafakari ya utangulizi iliyogawanyika katika sehemu kuu tatu: changamoto, wito na utume wa familia. Hii ni tafakari elekezi inayofumbatwa katika huruma ya Mungu kwa wanandoa wanaoishi katika mazingira magumu ya kifamilia, lakini katika ukweli. Ni mwaliko kwa Kanisa kuendelea kushikamana na familia maskini sanjari na kusimama kidete kulinda maisha tangu pale mtoto anapotungwa mimba tumboni mwa mama yake, hadi mauti inapomfika kadiri ya mpango wa Mungu.

Familia zinakabiliana na changamoto nyingi zinazoendelea kujitokeza katika ulimwengu mamboleo, kati ya changamoto hizi ni: uhamiaji, ukosefu wa haki msingi za kijamii, ujira kiduchu usiokidhi mahitaji msingi ya familia; nyanyaso na ukatili dhidi ya wanawake; mazingira magumu ya kazi; utoaji mimba kwa shuruti; mimba za chupa, idadi ndogo ya watoto wanaozaliwa; hamu ya kupata mtoto kwa gharama yoyote ile na madhara yake.
Mambo yote haya yanapelekea taasisi ya familia kuwa dhaifu, kiasi kwamba, baadhi ya watu wanakuwa wagumu kufanya maamuzi machungu katika maisha. Baadhi ya wanandoa wanaonesha utashi wa kuwa na haki zao binafsi, hali inayopelekea ubinafsi wa kutupwa, kiasi cha kushindwa kutambua mipaka kati ya ndoa na familia. Jamii ambayo kwa sasa inajikita katika suala la ulaji inashindwa kutambua tofauti kati ya tendo la ndoa na dhamana ya uumbaji ambayo wanandoa wamekabidhiwa, kiasi cha kugeuza maisha ya binadamu kuwa kama bidhaa.
Kardinali Erdo anaendea kukaza kwa kusema, ndoa na familia ni mambo ambayo yana mwambata mwanadamu katika hija ya maisha yake na hivyo kusaidia katika mchakato wa kurithisha tunu msingi za maisha ya kijamii na kwamba, ndoa inasimikwa katika udumifu ambao kimsingi ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na wala si mzigo kama wanavyodai baadhi ya watu.
Kutokana na ukweli huu, Kanisa linapenda kusimama kidete kulinda, kutetea na kudumisha tunu msingi za maisha ya ndoa na familia, kielelezo cha Jumuiya inayojikita katika maisha yanayofumbata upendo. Familia kama Kanisa la nyumbani linajikita katika msingi wa Sakramenti ya Ndoa, mahali ambapo, wanafamilia wanajifunza kujikita katika kutafuta na kudumisha mafao ya wengi.
Kardinali Erdo anasema kwamba, kuna haja kwa Mama Kanisa kuhakikisha kwamba, anatoa majiundo makini ya awali na endelevu kwa wanandoa watarajiwa, kwa kugusa mambo msingi katika maisha yao: kiroho, kimwili na Kikanisa. Wakleri waandaliwe vyema ili waweze kuwasaidia wanandoa katika makuzi yao, hususan waweze kuwa makini kuwasaidia wanandoa wanaoishi katika mazingira magumu ya kifamilia, daima wakijitahidi kuwasaidia waamini hao kwa kuzingatia huruma na haki. Hii ni changamoto kubwa kwa Wakleri na wahudumu wa Neno la Mungu, wanaopaswa kuanza kutafuta mfumo mpya wa Katekesi na shuhuda kwa kuonesha uaminifu na ukweli mfunuliwa kutoka kwa Kristo.
Dhamana ya familia ni pamoja na kuendelea kushirikiana na taasisi nyingine, hasa katika maeneo ambayo dhana na uelewa wa familia haushibani wala kuendana na Mafundisho ya Kanisa au mpango wa Mungu katika maisha ya binadamu. Lengo ni kusaidia kuonesha umuhimu wa familia katika jamii. Familia za Kikristo anakaza kusema Kardinali Erdo, zinapaswa kuonesha mshikamano wa dhati kwa familia maskini, familia zisizokuwa na fursa ya ajira; zinazokabiliwa na magonjwa au ambazo zimejikuta zikifilisika kwa kutumbukia katika mchezo wa kamali. Familia za Kikristo ziwe mstari wa mbele kuzisaidia familia zinazoishi katika vita na machafuko ya kisiasa, kijamii na kidini.
Kwa namna ya pekee kabisa, Kanisa linahamasishwa kuwa karibu zaidi na familia ambazo zimejeruhiwa, kwa kuzionjesha huruma na ukarimu pamoja na kuzisaidia kutambua ukweli wa maisha ya ndoa na familia. Kilele cha hali ya juu kabisa cha huruma ni kusema ukweli katika upendo, kwani upendo wa kweli unaunganisha, unabadilisha, unainua na kutoa mwaliko wa toba na wongofu wa ndani.
Kardinali Erdo anasema kwamba, huruma inajikita katika wongofu kwa mdhambi kutambua mapungufu yake, jambo linalohitaji majiundo makini, ili kutambua mpango wa Mungu katika maisha ya mwanadamu hususan kwa wanandoa waliotengana na kuamua kuoa au kuoana tena. Majimbo yatenge vituo vya kuwasikiliza wanandoa wanaokabiliana na changamoto katika maisha na utume wao. Huu uwe ni mwanzo wa hija ya msamaha na upatanisho pale inapowezekana. Kwa wale waliooa na kuachika na baadaye wakaamua kuoa au kuolewa wanapaswa kusaidiwa kwa kuzama katika mikakati ya kichungaji inayobainisha kweli za maisha ya ndoa kadiri ya Mafundisho ya Kanisa sanjari na huruma inayotolewa na Mwenyezi Mungu kwa msamaha wa dhambi, unaojikita katika toba na wongofu wa ndani.
Kardinali Erdo anasema kwa wanandoa wanaotamani kupokea Ekaristi Takatifu wanapaswa kufuata hija ya toba itakayowawezesha kupokea Sakramenti ya Upatanisho, bila kusababisha makwazo. Sakramenti ya Kitubio inaweza kutolewa kwa wale wanaotaka kufanya mabadiliko ya kweli katika maisha kwa kuzingatia kanuni maadili, utu wema na wajibu wa wahusika; mambo yanayohitaji majiundo makini ya dhamiri ya wahusika.
Kanisa linahamasishwa kuwa na mbinu mkakati makini kwa ajili ya kuwasaidia mashoga; kwa kuonesha heshima bila kuwabagua, lakini watambue kwamba, ndoa za watu wa jinsia moja si sehemu ya mpango wa Mungu kwa binadamu katika maisha ya ndoa na familia. Kanisa halitakubali shinikizo kutoka katika mashirika ya kimataifa kama sehemu ya masharti ya msaada wa kiuchumi hususan kwa nchi changa zaidi duniani.
Kardinali Peter Erdo katika tafakari yake elekezi anakazia kwa namna ya pekee Injili ya uhai inayopaswa kulindwa, kutetewa na kudumishwa tangu pale mtoto anapotungwa mimba hadi mauti ya kawaida inapomfika kadiri ya mpango wa Mungu. Kanisa linapinga kwa nguvu zote vitendo vya utoaji mimba na kifo laini kwa kukumbatia Injili ya uhai. Ni mwaliko kwa Kanisa kuendelea kutoa huduma kwa watoto wanaotelekezwa na wazazi wao; kwa kuwasaidia wanawake wanatoa mimba na familia zihakikishe kwamba, zinaendelea kuwahudumia wagonjwa wao. Kanisa litaendelea kuwahudumia wagonjwa: kiroho na kimwili.
Kardinali Erdo anawahamasisha waamini kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kama kielelezo cha mshikamano wa upendo unaofumbata Injili ya uhai dhidi ya utamaduni wa kifo. Kanisa linaendelea kuwataka wanandoa kuwajibika barabara kwa kuzingatia mpango wa uzazi kwa njia ya asili. Kanisa linapaswa kila wakati kuwa ni kielelezo cha huruma ya Mungu kwa waja wake na kumbe, wazazi ni wahusika wa kwanza wanaowajibika kutoa malezi makini kwa watoto wao. Wawe makini kuangalia elimu inayotolewa kwa watoto wanapokuwa shuleni.
Kardinali Peter Erdo anahitimisha tafakari elekezi kwa kulitaka Kanisa kutubu na kuongoka, ili liweze kuwa hai kama mtu binafsi na kama jumuiya ya waamini. Tayari kushuhudia huruma ya Mungu kwa binadamu.
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

Je wajua:Miujiza ya Bwana Mtume Muhammad S.A.W!

Hakika Muujiza mkubwa kuliko yote wa Bwana Mtume S.A.W ni hii Quraan tukufu ambayo haibadiliki kama vitabu vyinginevyo na kila zama zikenda ndio inafahamisha zaidi kinyume na vitabu viandikwavyo na mwanadamu ambavyo kila siku zikipita hubidi kufanyiwa marekibisho fulani ili viweze kwenda na wakati.

Muujiza mkubwa wa Bwana Mtume Muhammad S.A.W ni Quraan tukufu lakini kuna Miujiza mengi aliifanya ingawa hayadhukuriwi lakini hayo aliyoyatenda yalikuwa ni Miujiza hata kwa kule kusema kutakuwa na jambo fulani litakuja kutokea huo nao ni Miujiza, kwani utapoangalia Taarifu nilisema Miujiza hudhihiri katika baadhi ya mikono ya Mitume, hiyo ni sawa na hata kule kutabiri kuelezea kitachotokea nako huko kunakuwa Miujiza.

Wasomi mbali mbali waliweza kuyanukulu hayo akiwemo Ibn Taymiyyah, Al-Jawab as-Sahih li man Baddala Din al Masih iliyoelezwa na Ibn Kathir, Tarikh na Adh-Dhahabi, Tarikh al-Islam , Ibn Hajar Fathul Bari {6/582). Vile vile rudia Khayru-d-Din Wanili, Mujazat al-Mustapha 
(kopi ya 3, iliyochapishwa Maktaba as-Sawadi Jeddah).

Vitabu vingi vimeelezea juu ya Miujiza ya Bwana Mtume Muhammad S.A.W na baadhi ya miujiza ni kama ifuatayo:
·                     Kupasuka kwa mwezi
·                     Maji kuchuruzika katika pacha ya vidole vyake
·                     Kuongeza chakula kidogo kuwa chingi
·                     Jiwe kumsalimu
·                     Kuzungumza kwa mguu wa kondoo aliyona sumu
·                     Mti kutembea na kumfikia yeye Bwana Mtume
·                     Kondoo tasa kumfanya atoe maziwa
·                    Kulirejesha jicho la Qatidah bin an-Numan kwa mkono baada ya kudondoka na kurejea jicho hilo hali ya kawaida
·                    Alilitemea mate jicho la Syd Ali baada ya kuvimba na jicho hilo kurudia hali yake ya kawaida
·                    Kubashiri kabla ya tokeo la vita vya Badr kwa kusema hapa ndipo watapokufa wanaomshirikisha "Allah" na kuwataja baadhi yao kwa majina
·                     Alibashiri kuwa utajiri wa Chosroes utaangukia mikononi mwa waislam na utajiri huo utatumiwa kwa manufaa ya waislam, pamoja na kusema kuwa Wa-Farsy na Wa-Roma mali zao zitaangukia mikononi mwa waislam na Suraqah bin Malik atavaa kivazi cha Chosroes
·                     Alifahamisha kuwa Hassan bin Ali atapatanisha makundi yaliokuwa yaki talifiana baina ya waislam
·                     Alieleza kuwa Sa’d bin Abi Waqqas ataishi na hivyo vikundi vilivyokuwa viki talifiana na baadhi yao watafaidika na wengineo watadhurika
·                     Alibashiri siku aliyokufa Najash wa Ethopia na siku ya kuuwawa kwa al-Aswad al-Ansi akiwa yupo Yemen
·                     Alibashiri kutekwa kwa Turks, kutekwa kwa Iraq na Syria
·                     Alieleza kuwa Ammar bin Yassir atauwawa na wavamizi na hapo taifa la kiislam litagawanyika katika makundi (madheheb) na kupigana baina yao
·                     Alibashiri kuwa Ruwayfi bin Thabit kuwa ataishi umri mrefu na ikawa hivyo
·                     Alibashiri kuanza kwa moto mkubwa kutokea sehemu za Hijjaz yakawa hayo
·                     Alifahamisha kuwa Thabit bin Qays, kuwa ataheshimika na kusifiwa na atakufa kama shahidi yakawa hayo kwani alisifika na kuuwawa sehemu ikijulikana kama al-Yamamah
·                     Alibashiri juu ya misukosuko ya Sayyidna Uthman RA na yakatokea
·                     Aliwaeleza wakeze kuwa "Aliyemwepesi wa kutoa sadaka kati yenu ndio atayenifwata mwanzo, baada ya kufa kwangu". Aliyekufa mwanzo akawa ni Zaynab bint Jahsh (ra) huyu ndio kati ya wake wa Mtume aliyekuwa mwepesi wa kutasadak na ndio aliyekufa mara tu baada ya Bwana Mtume kufariki
·                     Mtume alimuelezea Anas kuwa atakuwa tajiri na kuwa na watoto wengi na vile vile ataishi umri mrefu. Inafahamishwa kuwa Anas aliishi zaidi ya miaka mia na ziada, na hakutokea kati ya Ansar aliyekuwa tajiri zaidi yake na aliwazika watoto wake wa idadi ya 120 kabla ya kutokea kwa Hajjaj nchini Basra (sahih Bukhari 1982)
·                     Aliomba moja kati ya Umar asilimu kwa kuupa nguvu uislam na Syd Umar Bin Khatab alisimu na uislam kushika nguvu
·                     Baridi ilishtadi na akamtuma Hudhayfa kwenda kufanya upelelezi akiwa hana nguo nzito za kumzuia baridi na akaomba awe hahisi baridi, na ikawa katika kipindi chote alichotumwa baridi inavuma naye kutohisi kabisa
·                     Alimuombea Ibn Abass awe ndio kigingi cha elimu ikawa hivyo
·                     Aliomba mvua kunyesha wakati wa ukame, na wakati anaomba hayo kulikuwa shwari mawingu kutoenekana na mara alipomaliza dua yake mawingu yalijikusanya na mvua kuanza kumiminika.
·                     Aliwaombea Abu Talha na mkewe Umm Sulaym waruzukiwe kizazi chema pale walipokutana katika usiku, matokeo yake alizaliwa Abdullah, na Abu Talha kupata watoto wengine 9 na wote wakawa wasomi
·                     Alimuombea Umm Qays bint Muhsin dada wa Ukkasha aishi umri mrefu haiaminiki kuwa alitokea mwanamke kuishi umri mrefu au kutaokea mwanamke ataoishi umri mrefu zaidi ya bibi huyu. Imepatikana kwa msaada wa
http://www.mawaidha.info/muujizawamtume.htm
 
Tukutana Jumatano ijayo kwa Je wajua...!
Tunamuomba "Allah" atufanikishe na haya "Amin"

Daily Reading for Wednesday, October 7th, 2015

Reading 1, Jonah 4:1-11 1 This made Jonah very indignant; he fell into a rage.
2 He prayed to Yahweh and said, 'Please, Yahweh, isn't this what I said would happen when I was still in my own country? That was why I first tried to flee to Tarshish, since I knew you were a tender, compassionate God, slow to anger, rich in faithful love, who relents about inflicting disaster.
3 So now, Yahweh, please take my life, for I might as well be dead as go on living.'
4 Yahweh replied, 'Are you right to be angry?'
5 Jonah then left the city and sat down to the east of the city. There he made himself a shelter and sat under it in the shade, to see what would happen to the city.
6 Yahweh God then ordained that a castor-oil plant should grow up over Jonah to give shade for his head and soothe his ill-humour; Jonah was delighted with the castor-oil plant.
7 But at dawn the next day, God ordained that a worm should attack the castor-oil plant -- and it withered.
8 Next, when the sun rose, God ordained that there should be a scorching east wind; the sun beat down so hard on Jonah's head that he was overcome and begged for death, saying, 'I might as well be dead as go on living.'
9 God said to Jonah, 'Are you right to be angry about the castor-oil plant?' He replied, 'I have every right to be angry, mortally angry!'
10 Yahweh replied, 'You are concerned for the castor-oil plant which has not cost you any effort and which you did not grow, which came up in a night and has perished in a night.
11 So why should I not be concerned for Nineveh, the great city, in which there are more than a hundred and twenty thousand people who cannot tell their right hand from their left, to say nothing of all the animals?'

Responsorial Psalm, Psalms 86:3-4, 5-6, 9-10

3 take pity on me, Lord, for to you I cry all the day.
4 Fill your servant's heart with joy, Lord, for to you I raise up my heart.
5 Lord, you are kind and forgiving, rich in faithful love for all who call upon you.
6 Yahweh, hear my prayer, listen to the sound of my pleading.
9 All nations will come and adore you, Lord, and give glory to your name.
10 For you are great and do marvellous deeds, you, God, and none other.

Gospel, Luke 11:1-4

1 Now it happened that he was in a certain place praying, and when he had finished, one of his disciples said, 'Lord, teach us to pray, as John taught his disciples.'
2 He said to them, 'When you pray, this is what to say: Father, may your name be held holy, your kingdom come;
3 give us each day our daily bread, and forgive us our sins,
4 for we ourselves forgive each one who is in debt to us. And do not put us to the test.'

St. Artaldus

Image of St. Artaldus

Facts

Feastday: October 7
Birth: 1101
Death: 1206

Artaldus (also called Arthaud) was born in the castle of Sothonod in Savoy. At the age of eighteen, he went to the court of Duke Amadeus III, but a year or two after, he became a Carthusian at Portes. After many years, being a priest and an experienced and holy religious, he was sent by the prior of the Grande Chartreuse to found a charterhouse near his home, in a valley in the Valromey significantly called "the cemetery". Here Artaldus established himself with six of his brethren from Portes. The community was no sooner well settled down, than there buildings were destroyed by fire, and St. Artaldus had to begin all over again. He chose a fresh site on the Arvieres River, and his second foundation was soon built and occupied. But a Carthusian cell could not contain the ever-increasing reputation of Artaldus: like his master St. Bruno, he was consulted by the Pope, and when he was well over eighty, he was called from his monastery to be bishop of Belley, in spite of his vehement and reasonable protest. However, after less than two years of episcopate, his resignation was accepted, and he thankfully returned to Arvieres, where he lived in peace for the rest of his days. During his last years, he was visited by St. Hugh of Lincoln, who had come into France, and who, while he was prior of the charterhouse of Witham, had induced Henry IIto become a benefactor of Arvieres. The Magna vita of St. Hugh records a gentle rebuke administered by Hugh when Artaldus asked him for political news in the presence of the community who had turned their backs upon the world to give themselves entirely to God. The cultus of St. Artaldus, called simply Blessed by the Carthusians, was confirmed for the diocese of Belley in 1834. He was 105 years old when he died and his feast day is October 7th.

Alex Msama wasaidie Moses Josiah na Elizabeth Josiah!


Pichani juu Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, Alex Msama.

Malkia wa muziki wa gospel nchini bibie Rose Muhando hatimaye amemaliza kurekodi album yake mpya ya sauti pamoja na kurekodi nyimbo mbili kwenye video huko nchini Afrika ya kusini chini ya kampuni ya Sony Music Entertainment ya Afrika ya kusini.

Kwa mujibu wa taarifa alizotoa mwimbaji huyo hii leo amesema amekamilisha nyimbo tatu zilizokuwa zimebakia katika kukamilisha album hiyo ya sauti ambayo hata hivyo hajaitaja jina. Mwimbaji huyo ambaye aliingia mkataba na kampuni hiyo ya kimataifa mapema mwaka jana, tayari amepata mafanikio makubwa kwenye medani ya muziki wa injili nchini tokea atoe album yake ya kwanza ya ''Mteule uwe Macho'' hadi yasasa ya ''Utamu wa Yesu''.

Hapana shaka kwamba album mpya itakuwa na kiwango kikubwa zaidi cha usikivu si kwenye sauti tu pia muziki wake utakuwa umerekodiwa kwenye viwango vikubwa kitu ambacho kitalifanya jina la Kristo lizidi kutangazwa si Tanzania tu bali maeneo mbalimbali duniani. Kila la kheri Rose Muhando.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2012/08/rose-muhando-akamilisha-album-mpya.html#sthash.kcdnx4hg.dpuf
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, Alex Msama umefanikiwaa kukutana waimbaji wa nyimbo za Injili hapa nchini Tanzania Moses Josiah na Elizabeth Josiah wa jijini Mwanza? wanaotamba sana Afrika Mashariki na Kati nyimbo Ukitaka na   Ruadha inmitelona.
              Mwimbaji Elizabeth Josiah

Batarokota Online kutoka jijini Mwanza inakuunganisha na wasanii hawa hasa ukiangalia nyimbo yao kupitia youtube https://www.youtube.com/watch?v=RndmI6GMOPA , 

Waimbaji hawa Moses Josiah na Elizabeth Josiah wana album kamili ya DVD  yenye nyimbo nane ambazo ni wewe ni Mungu, Tazama, Ruadha inmitelona,Bwana wa Mabwana,Mwambie Yesu,Galilaya, Ukitaka yeye ndio na Mambo yameona mengi ambayo ndio imechukua jina la album. 

Macho yameona mengi inerekodiwa katika studio za EX2 Studio iliyo maeneo ya Mecco jijini Mwanza nchini Tanzania. Na albamu hii ilikamilika mwaka 2014 , lakini mpaka sasa DVD imekamilika ila wasambazaji ndio tatizo ili iweze kutufikia uku mitaani.



Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, Alex Msamanaomba wasaidie waimbaji hawa ili tuweze kuzipata DVD.
 Pichani kutoka kushoto Msanii wa bongo fleva na nyimbo asili ya Kitanzania Batarokota akiwa na mwanamziki wa nyimbo za injili Moses Josiah

Huruma ya Mungu ipewe kipaumbele cha kwanza!



Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha, mjini Vatican, Jumanne, tarehe 6 Oktoba 2015 kwa kukazia huruma ya Mungu. - OSS_ROM
NA PASKAL LINDA- VATICAN.
Baba Mtakatifu Francisko katika mahubiri yake kwenye Kikanisa la Mtakatifu Martha kilichoko mjini Vatican, Jumanne ya jana, tarehe 6 Oktoba 2015 amekaza kusema, ni vigumu kwa huruma ya Mungu kuweza kupenya katika moyo mgumu wa kiongozi wa Kanisa, changamoto kwa watu kama hawa ni kuhakikisha kwamba, wanakimbilia huruma ya Mungu badala ya kujikita katika mawazo, sheria na taratibu walizojiwekea wenyewe!
Liturujia ya Neno la Mungu inaomwonesha Yona alivyokuwa na shingo ngumu kukubaliana na maagizo ya Mwenyezi Mungu, lakini hatimaye, anasalimu amri na kutoka kifua mbele kuanza kutangaza mapenzi ya Mungu, akiwataka wananchi wa Ninawi kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Kutokana na mahubiri haya, wananchi wa Ninawi wakatubu na hatimaye, wakafanikiwa kuonja huruma, msamaha na upendo wa Mungu katika maisha yao.
Lakini nabii Yona hakufurahia sana kuona Mwenyezi Mungu akiwaonjesha huruma na msamaha wananchi wa Ninawi. Alitaka Mwenyezi Mungu awashikishe adabu. Hii ndiyo historia ya maisha ya Yona anasema Baba Mtakatifu inayojikita katika sura kuu tatu: Sura ya kwanza inamwonesha Yona akikaidi utume aliokabidhiwa na Mwenyezi Mungu; Sura ya pili ni utii unaooneshwa na Yona kiasi cha kumjalia kufanya muujiza wa wananchi wa Ninawi kutubu na kumwongokea Mungu. Sura ya tatu inaonesha pia ukakasi katika kupokea huruma na msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Nabii Yona pamoja na safari yote ya maisha ya kiroho hakupenda kumwona Mwenyezi Mungu akiwasamehee wananchi wa Ninawi baada ya kutubu na kumwongokea Mungu, kwani alidhani kwamba, kazi yake ilikuwa bure. Hapa Yona aliweka mbele mawazo, sheria na kanuni zake, akasahau kuambata huruma ya Mungu. Baba Mtakatifu anakaza kusema, haya Yesu Kristo hakueleweka vyema na watu wa nyakati zake, alipokazia kwa namna ya pekee huruma katika maisha na utume wake. Kwa njia hii akasigana na wakuu wa Makuhani na Walimu wa sheria. Walishindwa kuelewa kwanini Yesu alimsamehe yule mwanamke aliyefumaniwa akizini! Wakashikwa na bumbuwazi kumwona akila na kushirikiana na watoza ushuru pamoja na wadhambi.
Wote hao walisahau kwamba, huruma na msamaha vilikuwa ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Yesu, jambo linalojidhihirisha kwa namna ya pekee hata katika Zaburi, inayowaalika waamini kumngoja Bwana kwani Bwana ni mwingi wa huruma na msamaha, kwake wokovu unapatikana. Baba Mtakatifu Francisko anawataka viongozi wa Kanisa kuwa na moyo wa wenye huruma na mapendo na kamwe wasiifanye mioyo yao kuwa migumu kiasi cha huruma ya Mungu kushindwa kupenya katika maisha ya watu; changamoto katika maisha, utume na huruma ya Mungu.
Baba Mtakatifu Francisko anasema, wakati huu Mama Kanisa anapojiandaa kwa ajili ya kuzindua na hatimaye kuadhimisha Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, iwe ni fursa ya kumwomba Yesu Kristo ili aweze kuwasaidia waja wake kutambua kwamba, Mwenyezi Mungu anataka rehema na wala si sadaka. Waendelee kuomba  Mwenyezi Mungu ili awakirimia huruma, ili kuponya dhambi na mapungufu yao ya kibinadamu!

‘Magufuli ni injini ya mabadiliko Tanzania’

INGAWA baadhi ya wanasiasa wanatumia neno mabadiliko kama kaulimbiu katika mikutano ya kampeni za uchaguzi, Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli anaonekana kuwa ndio injini ya mabadiliko ya kweli.

Katika mikutano yote ya Kampeni za kusaka kura za urais, Magufuli anahubiri mabadiliko na kusisitiza nia yake ya kuwa na Tanzania mpya.
Magufuli anataka Tanzania ya viwanda; itakayotokomeza umasikini kwa kutengeneza ajira kutoka asilimia tisa hadi asilimia 40. Hataki kuongoza serikali ambayo inakamua wazalishaji wadogo, kwa kuwatoza ushuru na kodi anazozitaja kuwa ni za hovyo. Anataka kuongoza mabadiliko ambayo yatawezesha mama lishe, wamachinga , wakulima, waendesha pikipiki za abiria maarufu kama bodaboda, kufanya shughuli zao bila kubughudhiwa.

Ni mgombea ambaye amekuwa akijinadi kwa kutumia kaulimbiu ya ‘Magufuli kwa Mabadiliko’. Katika mikutano ya kampeni kwenye maeneo mbalimbali nchini, amekuwa akiweka bayana anavyochukia ufisadi na mafisadi. Amekuwa akitaja msimamo wake pia namna anavyochukia uzembe na watumishi wazembe , wakiwemo wala rushwa wanaonyonya watu wanyonge.

Magufuli anasema wazi kuwa hana hofu ya kunyimwa kura na kundi hilo la watu.
Isitoshe, anaamini mafisadi na wazembe wanamchukia kwa msimamo wake. Hata hivyo, anaamini, wapo watu wazuri ambao ndiyo wengi ; wanaopenda kupata serikali adilifu na yenye viongozi waadilifu waweze kutendewa haki na kunufaika na matunda ya nchi yao. “Baraza langu la mawaziri litakuwa dogo na lenye watu waadilifu…,” anasema Magufuli.
Ameahidi kuboresha kilimo na kwa kuhakikisha anaongeza thamani ya mazao mbalimbali hatimaye wakulima wanufaike kwa bei nzuri itakayowawezesha kumudu mahitaji yao. “Sizungumzi uongo wala kuwapamba kwa kutaka kura…kazi ya kwanza ya serikali yangu itakuwa kusimamia bei ya tumbaku… kuna makato mengi na wanunuzi wengi wanaringa,” ni kauli aliyoitoa wilayani Sikonge katika mkoa wa Tabora.
Akiwa mkoani Kagera, Magufuli alieleza azma yake ya kuboresha zao la kahawa na kueleza kuwa hakubaliani na hatua ya wananchi kuuza mazao nje ya nchi kwa kuwa kitendo hicho kinadidimiza uchumi wa ndani na kuimarisha wa nchi jirani. Anasema endapo ataingia madarakani atapunguza kodi zilizowekwa kwenye zao la kahawa ambazo zinatajwa idadi yake inafikia 26. Vile vile anaona ujenzi wa viwanda vya kusindika kahawa, ni suluhu nyingine ambayo itawezesha zao hilo kupanda bei.
Pamoja na masuala mengine, anaahidi serikali yake itatoa elimu bure kuanzia Darasa la Kwanza hadi Kidato cha Nne. Kwa ujumla, yako mambo mengi mapya ambayo Magufuli na CCM kwa ujumla, wanaamini yatapatikana katika uongozi wa serikali awamu ya tano. Pamoja na mikakati hiyo, Magufuli anakiri awamu zilizopita chini ya marais wanne, zimefanya kazi nzuri inayomwezesha kuendeleza juhudi za kuwaletea maendeleo makubwa Watanzania.
Miongoni mwa mafanikio ya awamu zilizopita , ni pamoja na kuweka msingi imara wa amani na usalama wa nchi.

Ujenzi wa barabara, usambazaji huduma ya umeme, ujenzi wa zahanati, ni maeneo mengine ambayo mgombea urais huyo wa CCM amekuwa akikiri kwamba umekwenda vizuri kiasi cha kumwekea msingi mzuri wa kuleta mabadiliko makubwa zaidi chini ya serikali yake.
Wakati Magufuli na chama chake wakiamini katika falsafa hiyo ya mabadiliko wapo wanasiasa wanaobeza mabadiliko hayo. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, anasema mabadiliko ndani ya CCM yaliendelea na hatua ya kupeleka chama kwa wananchi. Kupitia Sekretarieti ya CCM, ikiongozwa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, aliyeteuliwa mwaka 2012 kuiongoza, alianza ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya chama.
Katika ziara hiyo iliyodumu miezi 28 kabla ya kuhitimishwa Julai mwaka huu , alibaini mambo yanayokera wananchi kwa ajili ya kuyafanyia kazi. Nape anaweka wazi kwamba, katika kuzungukia nchi nzima, walibaini miongoni mwa kero za wananchi ni rushwa, urasimu serikalini pamoja na dhuluma. Akiwa kwenye mkutano wa kampeni za mgombea urais, Mjini Iringa hivi karibuni, Nape anakiri kwamba, wapo watu wachache walitumia CCM vibaya kutokana na kuiba na kukimbilia kujificha kwenye chama.
“Chama chetu kikaanza kunyooshewa vidole…tukazunguka, tulipomaliza, tukaenda Dodoma tukasema tutafute mtu atakayeleta mabadiliko ya kweli kwenye utendaji wa serikali,” anasema Nape. Kwa mujibu wa Nape, katika orodha ya wagombea, hawakuona mwingine bali Magufuli. “Mabadiliko tunayoyataka ndani ya serikali, mabadiliko tunayoyataka ndani ya CCM, tutayapata kwa Magufuli. Magufuli ni chachu ya mabadiliko tunayoyataka,” Nape anasisitiza.
Baadhi ya wanasiasa wakongwe, wakiwamo Mawaziri wakuu wastaafu, John Malecela na Jaji Joseph Warioba, wanakiri Magufuli ndiye mtu sahihi wa kuleta mabadiliko nchini. Malecela ana imani kwamba CCM aliyoiacha Mwalimu Julius Nyerere bado iko imara na itaendelea kuimarika chini ya uongozi wa Magufuli. Kwa upande wake, Jaji Warioba anasema nchi ina kila sababu ya kumchagua Magufuli kwa kuwa ni mzalendo, anayehubiri amani muda mwingi.
“Wengine wanaona kama ni utani,” anasema Jaji Warioba mjini Dodoma hivi karibuni na kusisitiza kuwa anaamini Magufuli ataunganisha na kuimarisha umoja wa nchi. Jambo lingine linalomshawishi Jaji Warioba kuona Magufuli anafaa na ni chachu ya mabadiliko, ni kutokana na uadilifu na msimamo wake dhidi ya ufisadi. Jaji Warioba anasema, kipindi hiki panahitajika mtu mwadilifu kutokana na ufisadi kuwa tatizo kubwa nchini. “Magufuli ndiye mwenye uwezo huo,” Jaji Warioba anasisitiza.
Katika kudhihirisha nia na msimamo wake wa kuwezesha mabadiliko hayo, Magufuli katika mikutano yake, ameweka bayana kwamba hatakuwa na mchezo na wazembe, wala rushwa na mafisadi. Chini ya falsafa yake ya mabadiliko, Magufuli anachosisitiza ni kazi. Anaunga msimamo wa CCM kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Kinana ambaye baada ya kutembelea nchi nzima, alitoa karipio kwa viongozi wa chama na serikali, akiwataka waachane na kasumba ya kukaa maofisini, badala yake waende kwa wananchi wajue matatizo yao na wayafanyie kazi.
“Mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya tokeni ofisini, achanane na tai, viyoyozi nendeni mkakae na watu wa vijijini hao ndiyo wanaowalipa mishahara,” ni kauli aliyoitoa Kinana mjini Mwanza wakati akihitimisha ziara yake nchi nzima. Katika hotuba yake ya kuhitimisha ziara, Kinana aliweka bayana kwamba lengo ni kuhakikisha CCM inarudi kwenye misingi yake, aliyoiacha Mwalimu Nyerere.
Akionesha namna ambavyo Magufuli ni tunda la mabadiliko ndani ya chama, Nape anasisitiza katika kuhakikisha CCM inarudi kwenye misingi hiyo, tangu awali waliweka msimamo wa kuepuka wagombea wanaonunua uongozi. Hata kabla ya kura ya maoni, Nape akiwa kwenye mkutano wa mwisho mjini Mwanza, aliweka wazi kwamba chama hakikuwa tayari kukubali kupitisha mtu anayenunua uongozi.
Kwa ujumla, hoja iliyopo ni kwamba, pamoja na chama kupitisha mtu anayetarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika nchi, pia chenyewe kimejizatiti kuridhia mageuzi hayo kwa namna tofauti. Njia mojawapo ambayo imeshawekwa bayana, ni CCM kubadilisha mfumo kwa kutoruhusu Waziri Mkuu kuwa mwenyekiti wa wabunge wake katika Bunge ili kuepusha utamaduni uliokuwa umejengeka wa kupitisha kila kinacholetwa na serikali bungeni.

Elizabeth Josiah na Moses Josiah - Ukitaka

JESUS Film Swahili, Kenya- Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote...