Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Farida ambaye pia ni msanii wa filamu nchini, alisema kuwa ameishi na mume wake kwa miaka tisa lakini kadiri siku zinavyokwenda, ndivyo upendo unavyopoa na kitendo cha kufikia uamuzi wa kuwa na mapenzi na Diamond na kuchora tattoo zake ili kujibu mashambulizi kwa mumewe ambaye naye alijichora jina la mwanamke wake mgongoni.
“Binafsi nilikuwa nampenda sana mume wangu, lakini kitendo cha kuwa anakuja na hawara zake nyumbani kwa nyakati tofauti, huku nikiwapikia bila kujua, kilinifanya na mimi niwe na hasira hasa baada ya kumuona mume wangu