NDUGU yangu, ninatumaini nimekufikisha mahali pazuri. Hiyo ndiyo
historia ya mshazari wa Kanisa la Wasabato. Kifupi haina mashiko na
mtiririko wa kimantiki. Hata hivyo baada ya kuzaliwa kimtindo namna
hiyo, Kanisa la Wasabato halikubaki moja kifikra na kimtazamo.
Ukilichungulia ndani, Kanisa la Wasabato ni Muungano wa Vikundi vitatu
vya Waadventisti; Kikundi cha Bw. Hiram Edson, kilichosisitiza zaidi
mafundisho ya huduma ya Yesu Patakatifu pa Patakatifu mbinguni, Kikundi
cha Bw. Joseph Bates, kilichosisitiza zaidi kufuata Sabato ya Agano la

Roseline anadaiwa kuwatelekeza watoto wake wanaoishi na baba yao
Na Paskal Linda-Kenya.
Mwanamke mmoja nchini Kenya
ameamrishwa na mahakama kumlipa mumewe shilingi elfu tatu au dola 35
kama hela za kukidhi mahitaji yake na watoto wake kila mwezi.
Mwanamke huyo kwa jina Roselyn Muyonga, ambaye
anatuhumiwa kwa kuwatelekeza mumewe na watoto wake watatu , huenda
akafungwa miezi mitano jela au kutozwa faini ya shilingi laki mbili
ikiwa atakosa kutekeleza amri ya mahakama.